Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imetangaza kuanza Usajili wa Wakusanyaji na Wachakataji wote wa Taarifa Binafsi nchini ambapo imetoa muda wa miezi 6 kuanzia leo Aprili 10, 2024 kwa wahusika kukamilisha zoezi hilo
Watoa Huduma hizo wanapaswa kutekeleza wajibu huo kwa kufuata Kifungu Namba 14(1) cha Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Namba 11 ya mwaka 2022
Wakusanyaji na Wachakataji wote wanatakiwa kufanya Usajili kupitia Tovuti ya Tume ambayo ni
www.pdpc.go.tz na kwa msaada zaidi wasiliana nao kwa 0718462536, 0744057652, 0615779070 au kwa Barua Pepe
helpdesk@pdpc.go.tz
View attachment 2959804