Wakuu naomba Connection ya Kinglion Kibaha

Wakuu naomba Connection ya Kinglion Kibaha

Ngumbaru

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2018
Posts
495
Reaction score
677
Habari wakuu?

Ndugu zangu mimi naishi Misugusugu Kibaha, hivi karibuni nimeanza kuona dalili za ukame kwenye kampuni ninayofanya kazi, jana nikaona niombe ruhusa kazini ili niingie zangu mtaani kucheki mazingira.

Nyumba ninayoishi kuna vijana wanafanya mishe za ujenzi viwandani, kwenye stori zetu za kila siku hawa vijana walishawahi kunidokezea kuhusu uwepo wa viwanda vingi eneo la Zegereni Kibaha. Sasa siku ya jana nikaamua kuingia maeneo ya Zegereni-Kibaha, eeeh bwana eeeh huku kuna viwanda vingi sana na wenyeji wa haya maeneo wanakuambia viwanda vinajengwa kila kukicha.

Ndugu zangu habari za kutafuta kazi uzisikie tu kwa wenzio, hii kitu sio poa kabisa, jana nimetembea mpaka nikajionea huruma, nimegonga sana mageti ya viwanda, oyaaah Mungu awatie nguvu vijana wanaotafuta ajira kwa mtindo wa kuzunguka viwandani na maofini.

Tufupishe stori, katika kutembea kwangu nikafanikiwa kufika kwenye kiwanda kimoja kikubwa sana, ni kiwanda ambacho kipo kwenye hatua za mwisho za ujenzi lakini kimeshaanza uzalishaji. Askari niliyemkuta getini aliniambia kile kiwanda wanatengeneza mabati na pikipiki, nilizunguka viwanda vingi lakini hiki ndio kiwanda pekee ambacho askari wake aliniruhusu kuingia hadi ndani.

Nilimuuliza kuhusu utaratibu wa kuomba ajira pale kiwandani, alinijibu kuwa kwasasa kazi zinazopatikana pale ni kazi za ujenzi tu, ila kuna taarifa kuwa mwezi wa kwanza au mwezi wa pili mwakani kiwanda kitaajiri watu, baada ya stori za hapa na pale na yule askari nilichukua namba zake za simu nikatembea zangu. Yule askari aliniambia kiwanda kinaitwa KINGLION.

Sasa tuje kwenye lengo la uzi, jamii forums ina wanachama wengi sana, kama kuna mwanachama wa JF una mamlaka au connection KINGLION ZEGERENI - KIBAHA, fanya maarifa unishike mkono nije nikae pale maisha yaende, kiwanda bado kipya kabisa.
 
Habari wakuu?
Ndugu zangu mimi naishi Misugusugu Kibaha, hivi karibuni nimeanza kuona dalili za ukame kwenye kampuni ninayofanya kazi, jana nikaona niombe ruhusa kazini ili niingie zangu mtaani kucheki mazingira.
Nyumba ninayoishi kuna vijana wanafanya mishe za ujenzi viwandani, kwenye stori zetu za kila siku hawa vijana walishawahi kunidokezea kuhusu uwepo wa viwanda vingi eneo la Zegereni Kibaha. Sasa siku ya jana nikaamua kuingia maeneo ya Zegereni-Kibaha, eeeh bwana eeeh huku kuna viwanda vingi sana na wenyeji wa haya maeneo wanakuambia viwanda vinajengwa kila kukicha.
Ndugu zangu habari za kutafuta kazi uzisikie tu kwa wenzio, hii kitu sio poa kabisa, jana nimetembea mpaka nikajionea huruma, nimegonga sana mageti ya viwanda, oyaaah Mungu awatie nguvu vijana wanaotafuta ajira kwa mtindo wa kuzunguka viwandani na maofini.
Tufupishe stori, katika kutembea kwangu nikafanikiwa kufika kwenye kiwanda kimoja kikubwa sana, ni kiwanda ambacho kipo kwenye hatua za mwisho za ujenzi lakini kimeshaanza uzalishaji. Askari niliyemkuta getini aliniambia kile kiwanda wanatengeneza mabati na pikipiki, nilizunguka viwanda vingi lakini hiki ndio kiwanda pekee ambacho askari wake aliniruhusu kuingia hadi ndani.
Nilimuuliza kuhusu utaratibu wa kuomba ajira pale kiwandani, alinijibu kuwa kwasasa kazi zinazopatikana pale ni kazi za ujenzi tu, ila kuna taarifa kuwa mwezi wa kwanza au mwezi wa pili mwakani kiwanda kitaajiri watu, baada ya stori za hapa na pale na yule askari nilichukua namba zake za simu nikatembea zangu. Yule askari aliniambia kiwanda kinaitwa KINGLION.

Sasa tuje kwenye lengo la uzi, jamii forums ina wanachama wengi sana, kama kuna mwanachama wa JF una mamlaka au connection KINGLION ZEGERENI - KIBAHA, fanya maarifa unishike mkono nije nikae pale maisha yaende, kiwanda bado kipya kabisa.
Connection ni huyo huyo Mlinzi ishi nae
 
Mishahara ya wachina ni midogo. Kuna kazi za kulipana kwa siku (chini ya 10,000) kwa mwezi 150,000-300,000, sijui kwa sasa kama wamepandisha au kushusha. Labda upate kazi kwa elimu kubwa au ulipwe kwa commission. Pia kama kiwanda hakiuzi bidhaa mishahara inachelewa.
 
Nilikuwepo hapo wiki iliyoisha kiwanda cha kinglion niliitwa nikafanye interview ya umeme ila kwenye mshahara tulishindwana.

Namba ya hr wa hapo sikuisave mpk niitafute maana kuna namba nyingi ambazo sikusave nimewasiliana nao sana

Ofisi yao kubwa ipo makumbusho ghorofa kubwa kabisa kwa juu limeandikwa kinglion.Na hapo ndio kuna mahr wa kibongo na wafanyakazi wengi(ukifika hapo na ukiwapata unaweza ukapata mwanga zaidi)

Hapo kibaha kuna hr wa kichina tu na mchina mmoja wa kubagain pesa anaongea mpk kiswahili
 
Nilikuwepo hapo wiki iliyoisha kiwanda cha kinglion niliitwa nikafanye interview ya umeme ila kwenye mshahara tulishindwana.

Namba ya hr wa hapo sikuisave mpk niitafute maana kuna namba nyingi ambazo sikusave nimewasiliana nao sana

Ofisi yao kubwa ipo makumbusho ghorofa kubwa kabisa kwa juu limeandikwa kinglion.Na hapo ndio kuna mahr wa kibongo na wafanyakazi wengi(ukifika hapo na ukiwapata unaweza ukapata mwanga zaidi)

Hapo kibaha kuna hr wa kichina tu na mchina mmoja wa kubagain pesa anaongea mpk kiswahili
Salary ilikua ngapi?
 
Ukifanikiwa huko naomba unishtue na Mimi mkuu Nije nijeribu bahati Yangu
 
Hao jamaa nimewahi kupiga nao kazi za sales miaka kadhaa nyuma huko. Ni wachina,wabahili sio poa.mshahara kwa vibarua ulikua unachezea 180k kama sikosei.
 
Habari wakuu?

Ndugu zangu mimi naishi Misugusugu Kibaha, hivi karibuni nimeanza kuona dalili za ukame kwenye kampuni ninayofanya kazi, jana nikaona niombe ruhusa kazini ili niingie zangu mtaani kucheki mazingira.

Nyumba ninayoishi kuna vijana wanafanya mishe za ujenzi viwandani, kwenye stori zetu za kila siku hawa vijana walishawahi kunidokezea kuhusu uwepo wa viwanda vingi eneo la Zegereni Kibaha. Sasa siku ya jana nikaamua kuingia maeneo ya Zegereni-Kibaha, eeeh bwana eeeh huku kuna viwanda vingi sana na wenyeji wa haya maeneo wanakuambia viwanda vinajengwa kila kukicha.

Ndugu zangu habari za kutafuta kazi uzisikie tu kwa wenzio, hii kitu sio poa kabisa, jana nimetembea mpaka nikajionea huruma, nimegonga sana mageti ya viwanda, oyaaah Mungu awatie nguvu vijana wanaotafuta ajira kwa mtindo wa kuzunguka viwandani na maofini.

Tufupishe stori, katika kutembea kwangu nikafanikiwa kufika kwenye kiwanda kimoja kikubwa sana, ni kiwanda ambacho kipo kwenye hatua za mwisho za ujenzi lakini kimeshaanza uzalishaji. Askari niliyemkuta getini aliniambia kile kiwanda wanatengeneza mabati na pikipiki, nilizunguka viwanda vingi lakini hiki ndio kiwanda pekee ambacho askari wake aliniruhusu kuingia hadi ndani.

Nilimuuliza kuhusu utaratibu wa kuomba ajira pale kiwandani, alinijibu kuwa kwasasa kazi zinazopatikana pale ni kazi za ujenzi tu, ila kuna taarifa kuwa mwezi wa kwanza au mwezi wa pili mwakani kiwanda kitaajiri watu, baada ya stori za hapa na pale na yule askari nilichukua namba zake za simu nikatembea zangu. Yule askari aliniambia kiwanda kinaitwa KINGLION.

Sasa tuje kwenye lengo la uzi, jamii forums ina wanachama wengi sana, kama kuna mwanachama wa JF una mamlaka au connection KINGLION ZEGERENI - KIBAHA, fanya maarifa unishike mkono nije nikae pale maisha yaende, kiwanda bado kipya kabisa.

Kama waweza kaa Karibu kwa kuchukuwa hata kazi ya Ujenzi, itakuwa rahisi kuongia wakianza kuajiri
 
Nilikuwepo hapo wiki iliyoisha kiwanda cha kinglion niliitwa nikafanye interview ya umeme ila kwenye mshahara tulishindwana.

Namba ya hr wa hapo sikuisave mpk niitafute maana kuna namba nyingi ambazo sikusave nimewasiliana nao sana

Ofisi yao kubwa ipo makumbusho ghorofa kubwa kabisa kwa juu limeandikwa kinglion.Na hapo ndio kuna mahr wa kibongo na wafanyakazi wengi(ukifika hapo na ukiwapata unaweza ukapata mwanga zaidi)

Hapo kibaha kuna hr wa kichina tu na mchina mmoja wa kubagain pesa anaongea mpk kiswahili
Fanya maarifa tupate hiyo namba mkuu.
 
Back
Top Bottom