Wakuu nifanyeje nilijue draft?

Wakuu nifanyeje nilijue draft?

Wasalaam wakuu.

Nimejaribu njia nyingi, kuangalia tutorials,Kucheza online, kudownload checkers, kucheza na watu lakini mara nyingi naishia kula za uso tu.

Hivi hakuna app ya kunifunza strategies step by step?

Kila siku nachekwa kijiweni hadi naona aibu kuomba mechi.
Wee umejuaje linaitwa drafti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unatakiwa ucheze mechi nyingi sana...na ujue michezo yote kwa maana ya kwamba BRITISH na FRENCH ,CHINESE sio saana...kwa mfano ukiwa kanda ya ziwa inayochezwa sana ni FRENCH (Mbele na Nyuma)...ukienda Pwani na Nyanda za juu kusini ni BRITISH (Mbele tu)...na unapocheza draft unacheza madraft mawili (la kwako na la mwenzio) ...
Sema kibongo bongo tunachanganya sana sheria....British kingi lake halitembei mbali yani haliruki mbali ila linakula mbele na nyuma.
Spanish ndo tunayocheza pwani uku
ila sehem tofauti utakuta draft board limegeuzwa
 
[emoji23][emoji28][emoji23][emoji23][emoji2]....wewe wakujua drafti wewe,kwa kichwa kipi??

Bhange si ya kila mtu...acha bange mkuu.

Naona unashindana na ulivyoviumba??[emoji23]
[emoji28][emoji28] Sio dhambi kushindana mkuu siunajua tena mimi ndo mtunga sheria So siwezi kutenda dhambi
 
Usiguse kete kabla haujawa na uhakika wa kuicheza.

Ukiona mambo yanashindikana ibia.

Yakikwama kabisa mwezio akipanga kwenye vyumba vyeusi wewe panga zako kwenye vyeupe.

Ukila makofi uje ufungue uzi.
 
Usiguse kete kabla haujawa na uhakika wa kuicheza.

Ukiona mambo yanashindikana ibia.

Yakikwama kabisa mwezio akipanga kwenye vyumba vyeusi wewe panga zako kwenye vyeupe.

Ukila makofi uje ufungue uzi.
Acha Bangi bro..ila huu mchezo una ujinga Sana muda mwingine mi huwa nacheza mpaka nahisi kuumwa kichwa.unawaza kete zako unawaza za mwenzako,siku ukiamka ovyo unawaza na maisha hapo happy,yaani ujinga tu.
 
Acha Bangi bro..ila huu mchezo una ujinga Sana muda mwingine mi huwa nacheza mpaka nahisi kuumwa kichwa.unawaza kete zako unawaza za mwenzako,siku ukiamka ovyo unawaza na maisha hapo happy,yaani ujinga tu.
Ushindi mbinu
 
Anzia chini,

Kisha njoo na watu wa level yako,

Kisha panda waliokuzidi kidogo halafu tafuta mabingwa.

Kanuni kubwa ni kucheza kete za mwenzako.
Kucheza na Akili yake.

Fikiria Kuwa yeye akicheza Ile Mimi nitacheza hii.

Fikiria hata michezo minne mbele
Hizi ndio principles za kuwa bingwa wa draft,hata mimi ni mtaalamu wa huu mchezo.
Ukiona na hizi mbinu umetumia halafu bado hujui basi ujue una kichwa kizito yaani hata shule maana yake ulikuwa kilaza.
Mada imeisha hiyo
 
Lakini kwa mtoto kuelewa na kumasta ni rahisi sijui kwann
Watoto hawana mambo mengi kichwani,hawana mawazo yoyote zaidi ya kwenda shule,kurudi nyumbani,kula,kucheza.
Ila mtu mzima kichwa kina mawazo mengi ndio maana inakuwa hivyo.
Lakini kama maisha yako umeyaseti vizuri unaenda kazini kila siku ukirudi unapitia kijiweni na unazingatia vizuri basi baada ya miezi 6 au 12 unakuwa mtaalamu kiasi fulani.
 
Uhusiano upo tena mkubwa

Kuna watu wana akili sema wameaminishwa ni wajinga hivyo wameishi maisha yao yote wanaamini ni wazito darasani...

Namjua mtu ambaye alikuwa kati ya mwisho darasa la kwanza mpk la 5 halafu la sita na darasa 7 ndo anakuja kuwa kinara mnagombania nafasi za mwanzoni.Ni wasababu wamechelewa kujua uwezo wao


Kuna watu wana uwezo ila wanaamini hawana hao ndo wanakujaga kuwa wazuri kwenye draft wakati darasani ni wabovu.Kama unalijua draft vzr utakubaliana na mimi mwenye uwezo mdg wa kufikiria hawezi kuwa bingwa wa draft...
Nakazia hapa umeongea point sana.
Ila hapo kwenye mtu ulimsema hapo alikuja kuwa kinara darasa la 6 na 7 ni kama umenisema mimi vile isije ikawa tulisoma shule moja,ulisoma wapi mkuu?
 
Kuna ushindi unaitwa Super,mchezo mmoja unapigwa 12.
Wataalam wengi wapo uswahilini.mtu anashinda kijiweni kutwa nzima kwa mwaka ancheza draft.
Na wengi uwa ni madalali,mishen town muda mwingi wanakaa kucheza draft.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Madalali ndio wengi sana,utakuta anacheza draft huku anasikilizia simu yake iite akapige mchongo.
Ukiwaiga unaingia chaka vibaya
 
Nakazia hapa umeongea point sana.
Ila hapo kwenye mtu ulimsema hapo alikuja kuwa kinara darasa la 6 na 7 ni kama umenisema mimi vile isije ikawa tulisoma shule moja,ulisoma wapi mkuu?

Hahaha inawezekana kabisa
 
Wasalaam wakuu.

Nimejaribu njia nyingi, kuangalia tutorials,Kucheza online, kudownload checkers, kucheza na watu lakini mara nyingi naishia kula za uso tu.

Hivi hakuna app ya kunifunza strategies step by step?

Kila siku nachekwa kijiweni hadi naona aibu kuomba mechi.
Sijui nikusaidiaje aiseee....
 
Back
Top Bottom