Wakuu nisaidieni mke

Paul dybala

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2023
Posts
524
Reaction score
2,097
Wakuu, mimi nimechoka kupiga puli, nimechoka kulala peke yangu, nimechoka kuvaa nguo za kurudia, nimechoka kula kwenye mgahawa naogopa kulea watoto nikiwa mzee, mtu mwenye dada au ndugu wa kike tupeane connection mimi niko tayari kuoa.

Umri wangu miaka 32.

Kazi bado sina ila najishughulisha na vibarua kiwandani.

Nimelia sana wakuu.
 
Mkubwa, pole sana kwa sababu unaishi kwa kutizama watu wanasema nini juu yako. Ndugu yangu, maisha hayaendi hivyo. Hivi uliwahi kujiuliza mwanaume ambaye amefungwa jela miaka 30, wakati huo ana miaka 22, hajaoa wala hana mtoto, aje kutoka jela akiwa na miaka 52? Hivi huyu hajakata tamaa? Lakini wewe upo huru uraiani unashindwa kupambana. Siku zote, kutangulia siyo kufika. Bali angalia maisha yako pasipo kuhusisha maisha ya mtu mwingine.

Jitahidi kuwa na hofu na Mola Mlezi, fanya maombi mara kwa mara, fanya mazoezi ya afya, fanya kazi kwa juhudi na malengo. Hakika, Mola Mlezi atakubariki. Kila la kheri.

#Roca Fella
 
Nenda kwa wazazi wako wakutafutie sio hapa JF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…