Wakuu, njoo tujielimishe kuhusu hisa za Vodacom

Sasa nikitaka kununua nafanyaje?
Process
Inabidi uwasiliane na Broker, atakupa fomu utajaza kwa kuweka taarifa zako pamoja na picha. Ukishafungua akaunti inaitwa CDS utaweza kuanza kununua hisa. Mwombaji anaweza kutuma maombi ya hisa kupitia menyu ya M-Pesa (kwa kutumia *150*00#). Wateja wa mitandao mingine wanaweza wakatumia Maximalipo kufanya manunuzi yao.
 
Mkuu kama tayari una account unaweza ukanunua Hisa nenda bank NMB nafikiri ndio watakuwa wamechukua uwakala,
ambapo hisa moja ni Tsh. 850.
NBC ndio wamechukua uwakala, but kuna baadhi ya mawakala wamewapa Mabenki mengine uwakala. Mfano Orbit Securities wamewapa Benki nyingine japo na wao still wanahusika.
 
Unaweza sio lazma nbc
Waombaji ambao hawajawa na akaunti ya hisa (CSD) watatakiwa kujisajili ili kupata akaunti waweze kununua hisa. Usajili huo unaweza kufanyika kupitia orodha (menu) ya M-Pesa au Maximalipo.
 
Sisi majaji tuna acc CRDb,naweza kwenda nunua hisa bila husisha benki?
 
mi nwenyewe nineshakumbana nao, nilichoelewa wale hawajui chochote mpaka pale nilipoamua kuonana na Afisa ndio akanipa elimu kidogo.
 
Asante sana mtoa mada.Bila shaka una shule nzuri na ni mwalewa sana.
Mada kama hizi za kujuzana kimaendeleo ndizo zitakiwazo.
Wanajamii someni hiiyo mada, ni muhimu sana kiuchumi awe mtu mmoji au Kalindi. Achaneni na mambo lawa kwa serikali! Kueni wabunifu kwa maendelio yenu
 
CDS kwa kirefu ni nini?
Ni account ya nini?
Naifungua wapi, kwa garama ya sh ngapi?
Broker pia nampata wapi
Sorry kwa maswali mengi
 
Thanks japo tunaongelea DSE
 

Evelyn Salt

Kila wakala anayehusika na kuuza hisa hizo ana hizo fomu na hakuna gharama yoyote kujaza.

Mmoja wa wakala ni Orbit Securities wako Golden Jubilee Towers
 
...bei hiyo ya sh.850 kwa hisa moja ni kubwa sana...haswa ukizingatia bei za hisa kule DSE zimeshuka mno mno...huu si wakati muafaka kuwekeza kwenye hisa maana mfumo wa uchumi kwa utawala huu umevurugika sana....mfano ni hisa za CRDB ambazo mwaka jana kipindi kama hiki zilikuwa sh.400...leo zimeshuka hadi sh.185...hii ni mbaya sana...

...unaweza kununua hisa kwa sh.850 toka voda lakini ukashindwa kuziuza kwa bei ya juu ya hiyo...maana msingi wa faida kwenye biashara ya hisa ni kununua hisa kwa bei ya chini na kuziuza kwa bei ya juu ili kupata faida....vinginevyo hamna sababu ya kununua hisa kama huwezi kutengeneza faida..

..watu watasema hisa ni sehemu ya uwekezaji wa baadae...hili linakuwa kweli endapo mwelekeo wa soko la hisa ni chanya kule DSE...lakini kwa hali ilivyo sasa...soko la DSE liko doro mno...na wa kumlaumu ni JPM...
 
Kuna mtu aliniambia hisa wananunua wazee wenyewe hela benk et kwa kijana mdogo ni bora uzungushe hizo senti zako cuz return ya share ni ndogo sana
 
Kwanini msiuze hisa kupitia voda pesa na pia muwe na app yenye kufanya mambo yote ya hisa na gawio na kuonyesha grafu ya kibiashara ya voda na grafu yenye kuonyesha bei ya hisa kupanda na kushuka kwake
 
Hiyo menu mbona inaitaji sanduku la post hizi huduma za kizamani za hadi mtu uwe na sanduku la post zanini
 
Hisa mil560 ?? Nani ana mamlaka ya kuweka idadi ya hisa zinazouzwa mfano voda wakisema wanauza hisa mil 8000 = bil8 kwa sh850 kila hisa huo utakuwa ufisadi kwa pesa za wananchi nisawa mm niwe na biashara ya genge niuze hisa mil 4 kila hisa sh 500 ??? Mm namashaka sana na biashara ya hisa kama siyo ufisadi wa kimataifa na kuzidi kuyanufaisha makampuni kwa kuwanyonya wananchi
 
kuna mahali nilisikia kwamba kama kampuni inapata hasara ,wanaokua wa kwanza kupata hasara au hata kupoteza hisa zao ni wale wenye hisa ndogo katika kampuni husika.naomba kufafanuliwa hapa
 
mimi naamini kuwekeza kwa kununua hizi hisa kuna faida voda ni linakua sana kuingiza hasara sidhani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…