Wakuu, njoo tujielimishe kuhusu hisa za Vodacom

CDS ndio nini
Haya Mimi nahitaji kujua
Inakwambia vipi mkuu. Pole

 

Kama najisajili kwa kutumia simu (*150*36#) bado ntahitaji kujaza hiyo fomu unayosema unaweza kunitumia??
 
Duh... ngoja nisubirie majibu ya wadau maana ndo nlikuwa kwenye mchakato wa kujisajili.
 
Kama najisajili kwa kutumia simu (*150*36#) bado ntahitaji kujaza hiyo fomu unayosema unaweza kunitumia??
Nadhani kupitia Usajili huo huo wanaweza kukutumia Fomu ukajaza. Njia zote ni sawa angalia utakayo weza na rahisi kwako
 
Duh... ngoja nisubirie majibu ya wadau maana ndo nlikuwa kwenye mchakato wa kujisajili.
Sijawahi kujuta tangu nianze kununua hisa na kwa sasa nime nunua za kutosha kwa kuwa ndio biashara ninayoiweza naamini hao walio kushauri uachane nazo hawazijui. Lakini kama ukiwa na WASI WASI kwa kuwa zikiingia sokoni mwezi ujao tar 16 bei ilivyo panda utaiona kupitia simu yako ya kiganjani utagundua wamekukosesha fedha. Itakulazimu kusubiri hadi za Airtel, Tigo, Zantel na Halotel zikitangazwa kwani nazo zitauzwa mwaka huu (kwa mujibu wa sheria ya Bunge 25%)
 
mimi naamini kuwekeza kwa kununua hizi hisa kuna faida voda ni linakua sana kuingiza hasara sidhani
Hivi unafikri kwanini Wanasema Kwenye Tangazo lao . Kuwa Soko la Hisa Linachangamoto Nyingi. Uwasiliane na Mshauri wako wa Kifedha??
 
jamani hii biashara ya kununua hisa mbona inakuwa na mapassword mengi kama vile mtu anataka kujiunga na free mason.
 
Kuna mtu aliniambia hisa wananunua wazee wenyewe hela benk et kwa kijana mdogo ni bora uzungushe hizo senti zako cuz return ya share ni ndogo sana
return inategemea na performance ya shirika inaweza kuwa kubwa au ndogo au isiwepo kabisa iwe ni hasara....kwa mfano hisa za CRDB sasa hivi hakuna return ni loss tu
 
Kwanini mkuu?
Faida ya voda inashuka kila mwaka sana sana mwaka juzi iliporomoka sana kutokana na halotel kuingia kazini, na Airtel Money na Tigopesa kuwa na huduma sawa na za voda.
Kampuni ya Mtandao inayoingiza faida kila nwaka kwa kukua ni Halotel Pekeake.

Hizo nyingne huwezi tabiri kama zitapata mauzo.

Alafu pia ukicheki kua serikali inelazimisha kampuni za mitandao wauze shares zao.

Sio kua Voda walihitaji mtaji. Hapana.
 
return inategemea na performance ya shirika inaweza kuwa kubwa au ndogo au isiwepo kabisa iwe ni hasara....kwa mfano hisa za CRDB sasa hivi hakuna return ni loss tu
[emoji15] ikiwa hakuna faida.imekula kwako.hata ile hela yako hairudi?
 
Haya Mimi nahitaji kujua
Quoted "
CDS au "Central Depository System" ni mfumo wa kompyuta unaotomiwa na CDSC kuweka akaunti za hisa kwa njia ya kielectroniki. Akaunti hizi huwa zimefunguliwa na wamiliki hisa kwa hivyo, mara kwa mara, CDS hutumika kubadilisha hisa kutoka akaunti moja hadi nyingine wakati hisa zinaponunuliwa na kuuzwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam.

Hivyo basi, kila mmiliki hisa katika kampuni zilizosajiliwa katika DSE ni lazima awe na akaunti ya CDS illi kuweza kushiriki katika kununua na kuuza hisa."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…