Walaji wa kitimoto tujuzane kijiwe kipi kizuri kwa hapo ulipo

Walaji wa kitimoto tujuzane kijiwe kipi kizuri kwa hapo ulipo

Sio mpiga debe wa yeyote ila kuhusu mbuzi, ukila mbuzi wa pale Corner Lounge pale Jeshini Tabata kuelekea Kisukuru/External, utakubali kuanzia Soweto mpaka unamaliza Tbt hakuna zaidi yao ingawa Soweto inaniita kwa nyama ya Kanga tu, juisi freshi inajazwa sukari kama ugomvi, vingine ni kawaida mno. The Great, Ale Bush, KB, Last Call, Baraccuda, pale kinyerezi kwa yule dada wa bandari, Kitambaa cheupe, Forty Forty n.k kwa tabata wajipange, Centre Point hotel pale Bima wanatengeneza mbuzi nzuri ila vipande vya mifupa vimezidi. Cluh Africa imekuwa ya kimazoea zaidi, hizo ndio kwa uchache kwa eneo hilo la tbt.
Nitaenda hapo jeshini leo nikaone mambo yao, nashukuru sana kwa ushauri mkuu.
 
Kwa Mpiganaji Rujewa ni kiboko yaani, lakini funga kazi ni kwa Mapunda Igawa maeneo ya Fulumi hapo unapata kitimoto ya kubanikwa na kuroast mchicha kwa pembeni.
 
kiti moto ni haramu-najisi (HARMFUL)

Mwisho mbaya wa walao nguruwe katika Biblia


14Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia,

nanyi mtastawi kama majani;

mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake,

bali ghadhabu yake kali

itaonyeshwa kwa adui zake.

15Tazama, Bwana anakuja na moto,

magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli,

atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali,

na karipio lake pamoja na miali ya moto.

16Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake

Bwana atekeleza hukumu juu ya watu wote,

nao wengi watakuwa ni wale

waliouawa na Bwana.

17 Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini,

wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja

na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja, asema Bwana

  • Marejeo: Isaya 66:14-17
  • Imechapishwa: 18/01/202
Isaya 65
1 Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu,

2 Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe;

3 watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali;

4 waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;

5 watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.
Madahii haikuhusu
 
siku utaenda kutibiwa moyo ndo utajua hii mada inanihusu. hii kiti moto ni source mojawapo ya magonjwa ya moyo
muumbaji wake kasema ni najisi( harmful) wewe ni nani upingane naye
Nawajua watu kibao ambao hawali kitimoto na wanaugua magonjwa ya moyo, hii nayo unaielezeaje[emoji848][emoji848]

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Nipeni machimbo ya Kigamboni Mi najua Shamba Pub Na Rombo
IMG_20201010_125900.jpg
 
Nipeni machimbo ya Kigamboni Mi najua Shamba Pub Na Rombo View attachment 1595690
Mwambie Mtengenezaji aongeze (Pilipili ya kupika) na pia atengeneze style fulani ya kachumbari ambayo itajumuisha (Vitunguu kuvikatakata vipande vidogo +pili pili zilizokatwa vipande vidogo + mchuzi wa ndimu au aweke Vinegar) kwamba vinegar inakuwa kama mchuzi ambapo vipande vidogo vidogo vya kitunguu na pilipili zipo ndani yake.

Mtainjoy sana wateja wake, Take it.
 
Mwambie Mtengenezaji aongeze (Pilipili ya kupika) na pia atengeneze style fulani ya kachumbari ambayo itajumuisha (Vitunguu kuvikatakata vipande vidogo +pili pili zilizokatwa vipande vidogo + mchuzi wa ndimu au aweke Vinegar) kwamba vinegar inakuwa kama mchuzi ambapo vipande vidogo vidogo vya kitunguu na pilipili zipo ndani yake.

Mtainjoy sana wateja wake, Take it.
Hayo mambo nayapata chimbo gani mzee
 
Back
Top Bottom