Wale Matapeli wa "ile pesa tuma kwenye namba hii" Wanakula na baadhi ya wahudumu wa mitandao ya simu

Hawana makosa kwasababu! Usajili ni taarifa, zikiingizwa taarifa za uongo mfumo utazipokea!
Uongo unapikwa kuanzia kwenye nyaraka za usajili
Uongo kwenye NIDA namba? Sema yupo mjuzi kule mtandaoni anakorokochoa laini inakubali kufanya kazi bila NIDA
 
..ni wachache tutakaokuelewa
 
Sio kweli. Mi sijawahi kuongea ishu yoyote ya hela kwenye simu lakini ninatumiwa hizo meseji kila siku. Pia wafanyakazi wa kampuni za simu hawawezi kusikiliza maongezi ya wateja.
 
Unakuta kijana ana michepuko 5, lazima atume data kwa wahuni.
 
Acha uongo. Kwahiyo tukipiga simu na kuongea na mama zetu wanatusikiliza kwa kuwa tumetaja mama. Chai hii imrpoa mkuu na haina sukari.
Ww utakuwa mwewe tu lkn jamaa kaongea fact na huo ndio ukweli, kuna matamshi wameyaset kimkakati kama yakijirudia Rudia kama alivyosema mtoa mada basi line yako inakuwa taped na manjagu wanaanza ku concentrate kujua what a next word coming from ur mouth.

So people must be careful
 
Kwa takwimu za TCRA, Watanzania Milioni 20 wanatumia simu. So wametape na kuweka kusikiliza Neno Mama kwa hao watanzania 20M. Nyie watoto ebu jaribuni kuficha nyuchi za akili zenu. Mnajidharirisha na huu ujuha wenu.
 
Sio Tz tu, bado nchi nyingi hazina resources za kusikiliza kila call , kila dakika. Idadi ya watumia mitandao ni kubwa mno kuliko idadi ya hao wahudumu.

Resources zitazo tumika kukusikiliza ni ghali kuliko ki 50 chako. Ukiona mtu kasikizwa ilikuwa ni mlolongo n plan zilifanywa kupata taarifa.

Kuna privacy nyingi n technology bado ndogo hapa bongo, maybe with application of Ai technology n blockchain.

Wale wanafanya random guessing, hizo text zimeingia ktk simu hata kwa watu wasio n planz za kutumiana fedha.

Hawana tofauti na zile sms za waganga, vipiiii na wao wanasikia mazungumzo yako ukiwa unatafuta mganga [emoji780].

Wangeweza kusikia convo za watu basi ,hela zingepigwa nyingi tena sio hizi za tuma ktk number hiii. Kuna blackmailing, kuna wenye kujifanya prophets, wangang, majambazi kote wangekuwa wanannunua info.. Go and think again.
 
 
NINACHOJUA, NA NDIVYO ILIVYO.
Hakuna watoa huduma, wenye kusikiliza mawasiliano ya wateja, HAKUNA.
Watumiaji wa simu za mkononi wamefikia 35 million (angalia takwimu za TCRA).
Kwamba sio rahisi kwa mtu kusikiliza simu za maelfu ya wateja,SIO RAHIS!

SABABU ZA TAARIFA ZA WATEJA KUVUJA
Kampuni za simu zote zimebinafsisha vitengo vya huduma kwa wateja kwa makapuni mengine.
Kituo chake cha kazi ni hapo kwenye kampuni ya simu, ila mwajiri wake ni mwingine.
kumbuka hao wafanya kazi wana access za system nyingi za hizo kampuni, hawa sasa ndio wanavujisha.
Mfano wanaweza kuvuta (download) taarifa za wateja wale wenye kuweka salio kubwa mara kwa mara/wenye matumizi makubwa ya simu.
Hata ukitaka kujua kama mke wako anatoka njia kuu we tafuta hawa wadau, taarifa zake utazipata.
 
Hili ni kweli sana ukiwa na Hela usumbufu ni mwingi sana
 
Voda na airtel ndiyo mayapeli wamejazana kuomba pesa huko kwenye line zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…