Wale tuliopanga malengo Januari na hatujatimiza tukutane hapa, mwaka unaisha huu

Wale tuliopanga malengo Januari na hatujatimiza tukutane hapa, mwaka unaisha huu

Nilipanga Mengi But Ukweli ni Kwamba Asilimia Kubwa Ya Malengo ya Kwenye Dairy Hayatimii Kama Unahitaji Malengo Yako Yatimie plan on your mind Dhen Yawe rolling Katika mind Yako Every Day Every Moment Uta Move On.
 
Mm nashukuru mungu mkopo ulikuwa unsniumiza kichwa wa bank umeisha japo malengo yangu yote yamekwenda na maji
 
Nashukuru Mungu malengo yng yanakwenda vzr maana bd napumua na cna ulemavu.Thanx God m alive!!
 
Mipango yangu 2/5 nimeifanya japo imefeli ila sitachoka kujaribu hio mitatu iliobakia sijaitekeleza kosa kubwa ni kukosa adabu na fedha...natumai kuna watakao jifunza kutokana na makosa yangu...2018 naingia na kifutio kurekebisha makosa
 
Atleast lengo moja limetimia lingine ndo naruka nalo mwishoni mwa huu mwaka....ila naamini ntafanikiwa [emoji4]
 
Aisee kati ya mwaka ambao nimefanya Zero ni huu yani malengo yangu yote yamazingua nimefungua biashara nimekula loss za kutosha .
Mungu nijalie mwaka ujao nitimize malengo yangu na kufidia ya mwaka huu.
 
Lengo moja nlitimiza ila LA Pili bado nahitaji maombi zaidi
 
Ndoto ya kiwanja na kununua Bajaji iliingiwa na Kamdudu,bado namfaidisha tu Father House kwa Kodi ila Mungu mwema,tuombe uzima tuvuke mwakani na kujipanga upya.
 
Tuendelee kumshukuru Muumbaji kwa yote
2018 inakuja

Ushauri
Malengo yapangwe kulingana na kipato na yawe yenye uhalisia

Unaweza kuyanga ktk maeneo matano
1. Elimu ....kuongeza elimu

2. Kazi ...kupanda cheo au kufungua au kuboresha biashara

3. Family ...kuwa na familia au kupata mtoto

4. Akiba ya fedha mwisho wa mwaka

5. Nyumba au kiwanja
Nilijiwekea malengo mengine ila nilipata mengine;
Nilipanga kusoma master,ila mwanamke niliekua namchukulia kama wa kuondolea genye alinibadilisha maisha maana alinitafutia kazi nzuri,yenye maslahi zaidi ya niliyokua nafanya,amenisaidia kutafuta viwanja zaidi ya vitano na zaidi nimejikuta nimeamua kumuoa na kama nielimu tumeshauriana tufanye kwanza kazi kwa ajili ya kufungua mradi wetu mpya hapo mwakani ndio tufikirie mambo ya shule
 
MICHANGO IMEKUWA MINGI MNO, YAANI KILA MWEZI LAZIMA UVURUGE BAJETI KISA FULANI ANAOA AU ANAOLEWA. YAANI INABIDI UWEKE KWENYE BAJETI YAKO PESA YA MCHANGO.
MWAKANI KWA KWELI NATEGEMEA KUPATA HATERS WENGI SANA, NA QUIT KUTOA MINGANGO.
NITATOA MINGANGO YA CONDOLENCE PEKEE.
Kuna kitu kimoja au viwili hivi vilikuwa miongoni mwa malengo yangu ya mwaka nafikiri sitafanikiwa kuvitimiza.
 
MICHANGO IMEKUWA MINGI MNO, YAANI KILA MWEZI LAZIMA UVURUGE BAJETI KISA FULANI ANAOA AU ANAOLEWA. YAANI INABIDI UWEKE KWENYE BAJETI YAKO PESA YA MCHANGO.
MWAKANI KWA KWELI NATEGEMEA KUPATA HATERS WENGI SANA, NA QUIT KUTOA MINGANGO.
NITATOA MINGANGO YA CONDOLENCE PEKEE.
Kuna kitu kimoja au viwili hivi vilikuwa miongoni mwa malengo yangu ya mwaka nafikiri sitafanikiwa kuvitimiza.
Mimi nina mwaka sasa sichangii
Labda ugonjwa
Pia nimejitoa kwenye vyama vya wafanyakazi

Nitajiunga mwaka 2025
Mwenyezi Mungu akitupa uzima tele
 
Nilijiwekea malengo mengine ila nilipata mengine;
Nilipanga kusoma master,ila mwanamke niliekua namchukulia kama wa kuondolea genye alinibadilisha maisha maana alinitafutia kazi nzuri,yenye maslahi zaidi ya niliyokua nafanya,amenisaidia kutafuta viwanja zaidi ya vitano na zaidi nimejikuta nimeamua kumuoa na kama nielimu tumeshauriana tufanye kwanza kazi kwa ajili ya kufungua mradi wetu mpya hapo mwakani ndio tufikirie mambo ya shule
Nakushauri soma shule jioni
Ziko nyingi mno siku hizi
 
Nashukuru Mungu january nilipanga nipate kazi na ilivyofika march niliweza kuajiriwa, ..
 
Back
Top Bottom