Wale wa hizi enzi tukutane hapa

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
38,657
Reaction score
44,759
Naomba Mods msiufute uzi huu wala kuuhamishia mjuako, binafsi hizi picha zimevuta taswila ya mambo mengi akiwepo mzee pekee aliyekuwa na duka mtaani kwetu, ilikuwa ukienda kununua bidhaa anakuuliza chenji yako ni kiasi gani?

Ukishindwa hesabu kama unasoma madarasa ya kuanzia Std 3 na kuendelea unakula konzi za maana ndipo uhudumiwe RIP Mzee Phano

 
Kodak imenikumbusha nlikua nahitaji picha passport naenda kwa camera man kapiga picha anamaliza ananiambia uje uchukue baada ya mwezi asee nlimchukua nkaenda nae home nkamwambia piga picha kila unachoona hapa ili huo mkanda ujae picha nazihitaji week ijayo daah technolojia imetutoa mbali sana unapewa picha na nega unapandikiwa nyuma ya picha mpaka kesho nazo
 
Kipindi Cha mafuta ya OKI late eighties and early nineties ukimwi ulikua haukopeshi. Ukijisahau hujavaa miezi mitatu nywele Ni kipilipili, mapele, kuharisha, midomo kuchubuka bila kumsahau kukonda ndani ya wiki mbili na baridi kwa sanaaa.
 
AlhamduliLlah nilikuwepo.
 
nlimchukua nkaenda nae home nkamwambia piga picha kila unachoona hapa ili huo mkanda ujae picha nazihitaji week ijayo daah technolojia imetutoa mbali
🤣
 
Enzi hizo ukisikia kingora kinalia unajua asilimia kubwa atakuwa ni Raisi wa nchi anapita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…