Wale Wanasimba SC Wanafiki kama Haji Manara na mliokuwa mkimtetea wakati wenye Akili tulishamshtukia mnahama nae au?

Wamezingua sana.
 

U T O P O L O [emoji2937]
 
Sikutegemea kitu kama hiki kinaweza kutokea.Mpenzi wa Simba ahamie Yanga au wa Yanga kuhamia Simba? Manara atakuwa na roho tofauti sana.
Ni opportunist bila shaka. Kwake, fedha ndiyo kila kitu! Utu na heshima yake, vinafuatia.
 
Ni kweli kabisa na kuna mtu anaitwa Gentamycin nae alitukanwa sana humu baada ya kumshtukia yule kirusi,, asee kumbe ni kweli kabisa yule alikuwa ni nyoka.
 
Kama kweli una akili timamu,naomba unijibu hili swali hapo chini.

Baada ya Manara kufukuzwa Simba Sc kea tuhuma za usaliti, ulitegemea akae bila kazi Ili uonyeshe mapenzi yake kwa Simba Sc ambayo ilishaonyesha kudharau utumishi wake kwa miaka yote ile?

Ikiwa angeamua kukaa bila kazi Ili akuridhishe wewe na mashabiki wengine wachawi kama wewe, ungewajibika kuihudumia familia yake kwa miaka yote?

Ukifatilia kwa makini, mashabiki wengi wa Simba Sc walitaka jamaa aadhirike Ili waendelee kumcheka, kinachowauma sio yeye kwenda Yanga kinachowauma ni yeye kupata chaka jingine ilihali mlitaka awe ahehae kwakua mliamini kuwa Simba Sc ndo kila kitu kwake.
 
Haya Leo hii unayoita Chuki yangu Kwake imekuwa ni ya Faida au Hasara? Je, niliyoyasema yamethibitika au hayajathibitika? Utabakia hivyo hivyo na Ujuha wako.
Always Chuki ni hasara.
 
Kutoka Twitter ya mtangazaji mahiri wa michezo Tanzania Shaffih Dauda, kuhusu Haji Manara na wapenzi wa soka Tz, "Wale waliompenda Haji, tayari yupo Yanga na wale wanaoipenda Simba basi yenyewe ipo na itaendelea kuwepo, Mjifunze sana kuupenda mpira kisha timu, mkipenda watu watawashangaza sana"
 
Mbona wachezaji,makocha,viongozi wanahama?Kwanini isiwe manara?Kama aliyekuwa CEO wa Simba yuko Yanga,inakuwaje ajabu kwa msemaji?
Kikubwa maslahi,mpira ni fedha!
Hapo hakuna cha usaliti wala nini,ni jambo la kawaida kwenyw mpira!
 
We mpuuzi sana..Nijibu nilivyokuuliza kulingana na ulivyosema, hakuna anayepinga Haji kufanya kazi Taasisi nyingine kwa weledi na misingi ya kazi, ila je alivyokuwa anafanya kazi, Azam, Simba, GSM

Ni sawa tu kufanya kazi Vodacom, Tigo, Airtel?
Nyie ndio Rage alikuwa anawazungumzia. Huduma aliyekuwa anaitoa kwa Simba ni tofauti na huduma alizokuwa anazitoa kwenye hayo makumpuni mengine. Simba alikuwa msemaji wa club huko kwingine alikuwa siyo msemaji ila kutangaza biashara zao.
Kwa wenye akili huwa wanafanya hivi, kama hawataki mfanyakazi wao afanye kazi na wapinzani wao, sharti hili huliweka kwenye mkataba wa ajira na saa nyingine huvuka kuwa hata akiacha baada ya miaka flan hatafanya kazi na wapinzani wa mwajiri husika.
Simba haikuwa na sharti la hivi, hivyo ukisikia mtu anasema Haji kakiuka maadili, huyo hajitambui.
 
Hawa watu ni wajinga sana, yaani walitegemea Haji asifanye kazi tena baada ya kufukuzwa hapo Simba!!.Halafu mjini aishije?
 
Upigiwe saluti kwa huu ujinga wako? Manara kwenda kufanya kazi Yanga ndio inathibitisha kua alikua anaisaliti Simba? tumia akili japo kidogo ili usiendelee kujidharaulisha hapa,

Ulitaka akae tu bila kazi? Mpira ni pesa,Messi kaenda PSG kwa pesa,Luis Figo alitoka Barcelona kwenda Madrid kwa pesa,

Dogo tafuta hela bila kuogopa kusemwa na watu au watu watakuchukuliaje! usiishi kwa kutaka kumfurahisha kila mtu,hutoweza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…