Wale wote wanaotumia bidhaa za kampuni ya Xiaomi tukutane hapa ili kupeana ujanja

Kuna "simu roho ya paka" haifi, hapa unashauri nini?
Itumie all the time ,nakaa nafikiria hizi pesa tunazonunulia simu !! Tukumbuke ipo siku tutaziacha simu zetu pendwa na kwenda nchi za mbali yaani ardhini ,Tukumbuke kutenda mema ndo fadhila zetu , Hizi pesa tunazomwaga kununua kila aina ya simu tungewasaidia wasiojiweza zisingetusaidia kama amali huko Tuendako??? WEMA NI AKIBA LAKINI SIMU HATA UITUMIE VIPI HAINA WEMA MBINGUNI.[emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]
 
MKUU HUJANILEEWA VZR , MAANA YANGU UKIWA NA SIMU INAYOKIDHI USITUMIE PESA KUNUNUA SIMU NYINGINE , KISA ETY UNAHAMIA KWENYE VERSION ZA KISASA..
 
Kifo ni lazima mkuu! Kikubwa tuishi katika maisha ya kumpendeza Muumba. Ni kweli simu tutaziacha, hatuzikwi nazo. Ila kifo kisikuzuie kutimiza ndoto zako na wewe fanya yote utakayoyaona ni mazuri ilimradi usikufuru tu! Wote tungekuwa na mawazo kama yako tusingefanya shughuli zozote za maendeleo kuogopa kifo!

Mfano: Eti usioe mke mzuri eti ukifa utamuacha, sasa watu tusioe wake wazuri!?[emoji4] .
Kikubwa ya Dunia yabaki kuwa ya Dunia na ya Mungu yabaki kuwa ya Mungu.
 
[emoji3][emoji3][emoji3]@Mr.Mobile daaah nimekusalute sana bigup kwa maoni yako mazuri ..
 
Pia cheki Xiaomi Mi 9 SE ndio mpinzani mkubwa wa Samsung Galaxy A50.
Sawa mkuu ila Samsung Galaxy A50 ina nini hasa cha tofauti, watu wengi wanarate 50/50 kama midrange, Na nikiangalia huu uzi naona positive reviews kuhusu Xiaomi
 
Sawa mkuu ila Samsung Galaxy A50 ina nini hasa cha tofauti, watu wengi wanarate 50/50 kama midrange, Na nikiangalia huu uzi naona positive reviews kuhusu Xiaomi

Uzuri wa Samsung ni ile 24 Month warranty, tofauti na hizi Xiaomi ni 12 Month warranty, pia nina recommend Xiaomi Mi 9 SE kwa sababu unafuu wa bei ukilinganisha na Samsung Galaxy A50,... Xiaomi ni kampuni wanayojitahidi kwenye ubunifu wa software na kuweka hardware bora kabisa lakini still inabaki kuwa nafuu!
Kuhusu pros & cons ni vitu vya kuangalia wewe mwenyewe unapenda kipi kati ya hizo simu mbili, kila simu ina muzuri yake na mapungufu yake.
 
afu vp kuhusu sony z5 premium naombeni ushaur naitaji niagize nimeona sio ghar kidg.?
 
afu iv inawezekana kuagiza mzg kwa kutumia sanduk la post la mtu/ taasisi. afu ukaipata.?!
 
oi braza em tuelekeze unawezaje kutuma kitu bila sanduku la posta
Mkuu ni vilevile tu kama unavyonunua ukiwa na sanduku ila pale kwenye address nimeandika namba zangu za simu badala ya sanduku la posta maadam ni standard shipping basi utaudirect Mzigo wako ufike posta
Mimi niliudirect ofisi kuu za posta zilizopo posta mpya DARESSALAAM post code 17000

Unapewa track namba mzigo ukifika posta watakupigia, kikubwa namba za simu ulizoweka ziwe hewani

Jina utakaloandika kwenye mzigo lifanane na jina kwenye kitambulisho cha atakayepokea mzigo pale posta
 
Mzigo ulipofika posta walikutumia msg?

Maana mimi wamenirudisha wanadai watanitumia msg ili nikachukue mzigo wangu utakapofanyiwa kazi, tracking inaonesha mzigo umewasili posta tangu tarehe 2 mwezi huu
(Sina Sanduku la posta)
Mizigo ya tarehe 2 ilikua haijafanyiwa kazi,wameanza kuitoa Jana (tarehe 9),nadhani ukienda kuanzia leo utaukuta tayari.
Jana nilifata simu na me ilifika tarehe 2 hiyohiyo
 

MI MAX 2 storage 128GB BEI GANI
 
Card yangu bancabc ili expire nikacreate mpesa mastercard kwa muda tu.
Refund inatakiwa iingie kwenye card directly hayo mambo ya kupiga simu Huduma kwa wateja sio kabisa
Mkuu kumbe refund zinaingia fresh bila hata kuwapigia au kusumbuana na Customers service asee!!
Leo Nimecheck salio la card nikagundua mpunga umeongezeka nikasema ngoja nisake statement nikaipata yaani kitu kumbe kiko fresh hiki.
Ukiona kimya ujue suala Lako liko processed refund zitaingia tu.
Kingine nilichogundua ni kwamba hii Huduma ya mpesa virtual card siyo bure bali kila transaction ufanyayo online wanachota kiasi fulani

πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†Hapo nilipozungushia red rectangular ndio refund zenyewe na screenshot za chini ndio disputes zilizo refundable πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡





Cc:- Mr. Mobile
 
Ninavyojua wanakata 4% kila malipo yanapofanyika
 
Okay, safi sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…