Walevi awakosi sababu ya kulewa

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
Tuseme ukweli, walevi wana kipaji cha hali ya juu cha ubunifu. Wakati sisi wengine tunahangaika kutafuta sababu za maana za kufanya maamuzi maishani, wao hawana muda wa mawazo magumu—maisha ni mepesi tu: Kila siku ni sababu ya kunywa.

Jumamosi? Ni siku ya kupumzika.
Jumapili? Yesu alikunywa divai.
Jumatatu? Stresi za kazi zimeanza.
Jumanne? Watoto wanazingua.
Jumatano? Ni katikati ya wiki, tunavuka mto wa tabu.
Alhamisi? Weekend inaonekana kule mbele.
Ijumaa? Yesu ameruhusu.

Na unadhani kisingizio kinaishia hapo? Hapana. Kuna wale watajitetea na sayansi, eti bia ina madini ya chuma, inasaidia damu. Mwingine atasema pombe huongeza furaha na kupunguza msongo wa mawazo. Ukitaka kuwashtua, waulize lini hawanywi. Hakuna atakayejibu.

Kwa walevi, hakuna siku isiyofaa kwa kinywaji. Na kama huamini, tafuta mlevi mmoja umwambie hakuna sababu ya kunywa leo. Utapewa maelezo yenye ushahidi wa kihistoria, kidini, kisayansi, na hata kifalsafa.

Kwa hiyo, msione ajabu ukikutana na jamaa anakunywa Jumanne mchana na anakwambia:
"Aisee, watoto wa mtaani wanapiga kelele sana. Hata mimi nina haki ya utulivu."

Ndio maana walevi hawashindwi, kwao maisha ni mepesi, sheria ni kisingizio, na kalenda ni msamiati wa wasioelewa maana ya raha.
 

Attachments

  • 00520697_c1bff8d12a6c19ad74952725152f1364_arc614x376_w2172_us1-3661773833.jpg
    295.6 KB · Views: 2
  • 2013_10_19_043427_0_image001-768x431-2183247751.jpg
    59.4 KB · Views: 3
  • 20-of-the-funniest-photos-of-drunk-people-5-2567767107.jpg
    45.2 KB · Views: 3
  • Amazing+Funny+Drunk+Kids+%2818%29-2638513617.jpg
    52.4 KB · Views: 1
  • drunks-1-936856129.jpg
    34.6 KB · Views: 2
  • th-1081309426.jpg
    18.8 KB · Views: 3
  • image1898068883-4299-eb424caefa3c738df5e378ba8850528b@1x-3199474670.jpg
    112.3 KB · Views: 2
Mimi mwenyewe niko Bar sahizi na kesho ni kazini. I was super tired nikaamua nijiwashe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…