Walifungiwa app za mikopo walichokifanya ni kubadilisha majina ya hizo app na bado wanaendelea kufanya utapeli

Walifungiwa app za mikopo walichokifanya ni kubadilisha majina ya hizo app na bado wanaendelea kufanya utapeli

chrispny

Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
71
Reaction score
12
Habari wana JF.

Kuna suala linaloendelea juu ya app za kukoposhe ONLINE. Hii mikopo imekaa kiunyonyaji sana.
Mtu anakopa pesa online anapewa lakini mwisho wa siku usumbufu unakuja kwa watu ambao hawahusiki na huo mkopo.

Nimekuwa nikipokea message kutoka kwa hawa jamaa wakidai nimewekwa kama mdhamini wa huyo mtu anayedaiwa.SWALI LA MSINGI:Wakati mnamkopesha kwanini hamkunipigia simu kufanya confirmation?

Hawa jamaa ni waongo sana. Wanachofanya wakati mtu anakopa wana acces phone book na baadae wananza kutuma message kwa watu ambao kimsingi hawahusiki.

Nimeona BOT walisema hawa jamaa hawatambuliki na wako kinyume na sheria lakini walichofanya ni kubadilisha majina ya hizo app na bado wanaendelea kufanya utapeli na kuleta usumbufu kwa watu ambao hata hawausiki na mikopo yao.

Wito wangu kwa wizara ya fedha, BOT na TCRA.

Hawa wafungie hizi app zote hadi wakifuata muongozo uliotolewa kuwa wanatakiwa wasajiliwe na BOT.ili watambulike kisheria.
TCRA BOT
 

Attachments

Back
Top Bottom