Walimu tusitumie madhaifu ya wazazi kutukana watoto pale wanapokosea

Walimu tusitumie madhaifu ya wazazi kutukana watoto pale wanapokosea

robbyr

Senior Member
Joined
Apr 8, 2017
Posts
129
Reaction score
221
7c5b6f409f9dd9fa1d5cbd6898465f49.jpg

Picha: Pinterest

Upendo wa mwalimu si kumfundisha mtoto tu bali hata kulinda heshima na hisia za mtoto kwa kuweka siri au faragha za wazazi wake.

Usitumie makosa ya mtoto na kufananisha na matendo ya mzazi au wazazi wake hasa yale ambayo si chanya kwenye jamii kwani kwa picha yake na jinsi anvyojitambulisha mbele yake inaweza kuharibika kwa kushindwa kujiamini na hata kujihisi hawezi kufikia ndoto yake.

Ila unaweza kutumia mambo yale chanya wazazi wanayofanya kwenye jamii ili kumuonyesha na yeye anaweza kufikia ndoto yake na kutoa mchango bora kama wazazi katika jamii na taifa kama atazingatia nidhamu, bidii n. k

Asante.
 
Back
Top Bottom