Walimu wa kiswahili wa shule za sekondari kuna mahali mnafeli pakubwa

Ashakum si matusi, ila nachelea kusema hao walimu wa lugha ni vilaza kupitiliza. Maana kuna jamaa kadhaa ni walimu wa lugha na nipo nao kwenye kundi sogozi lakini wao wenyewe wana changamoto kubwa katika uandishi wa Kiswahili, hawaelewi matumizi sahihi ya "Z" na "Dh", yaani pakuweka "dhana"anaweka "Zana" na kinyume chake, hawana weledi wa matumizi ya "h", sehemu ya kusema "habari" inawekwa "abali", "asubuhi" itaandikwa "hasubui".
Binafsi naona miaka kadhaa ijayo kiswahili sanifu kitapotea kwa kasi kama hizi lugha za asili
 
Kiswahili ni janga hadi maprofessor na maPhD na MSc Kibao kwenye Whatsapp groups wanaandika hovyo masela wangu nawachana Utopolo mwingi imagine graduate wa chuo kikuu anaandika uchuro hovyo
 
Najiuliza kitu kimoja wao kama walimu huwa kuna barua mbali mbali za kikazi nani huwa anawaandikia?
 
Kiswahili ni janga hadi maprofessor na maPhD na MSc Kibao kwenye Whatsapp groups wanaandika hovyo masela wangu nawachana Utopolo mwingi imagine graduate wa chuo kikuu anaandika uchuro hovyo
Sasa ndio maana Dw na BBC wakenya ni weng kuliko waTz
 
Sasa ndio maana Dw na BBC wakenya ni weng kuliko waTz
Hahaha ya DW na BBC tatizo ni English competences na Tasnia hio ilikuwa kwaajili ya vilaza walokosa options, mass communication walikuwa wanaenda kusoma wenye pass mbovu za A'level na vilaza wa O'level
 
Hahaha ya DW na BBC tatizo ni English competences na Tasnia hio ilikuwa kwaajili ya vilaza walokosa options, mass communication walikuwa wanaenda kusoma wenye pass mbovu za A'level na vilaza wa O'level
Ni kweli mzee. Sasa na kibongo bongo kuna media kubwa zinaleta kiswahili-kingereza(kiswa kinge) Yan wanauzi sana huwa hawakai wakamsikiliza mtu kama Dr. Tulia huwa hachanganyi lugha na yuko vizuri sana, kuna January makamba yupo makini sana kwenye utumizi wa lugha kama ni kiswahili ni kiswahili kingereza ni kingereza tu
 
Shule za mchepuo wa Kiingereza zimetuharibia Kiswahili chetu...hapo mtamtafuta mchawi wakati mchawi ni hizi shule..
 
Kuchanganya sio dhambi labda katika muktadha ambao ni budi kufanya hivyo kwa aina ya hadhira kusudiwa
 
Shule za mchepuo wa Kiingereza zimetuharibia Kiswahili chetu...hapo mtamtafuta mchawi wakati mchawi ni hizi shule..
Sidhani mkuu asilimia kubwa ya wanafunzi ipo shule za kawaida /kata still walimu wanatumia kiswahili kuelekezea wanafunzi kwenye hayo masomo ya kingereza
 
Unaweza kukuta chanzo cha tatizo ni hao hao walimu ambao wewe ndio unawataka waangalie hilo tatizo!
 
Lakini mkuu nina imani watu kama hao umekutana nao
Ndio nimekutana nao lkn asilimia kubwa hata darasa la saba hawakumaliza tena vijijini huko na wala siwalaumu ni baadhi ya mazingira kutokuwa rafiki katka elimu hasa vijijini watoto wengi wanamaliza primary hata kusoma tabu

Sioni haja ya kulichukulia kama udhaifu kwa walimu tena siku hizi walimu wanajitahidi sana watoto wanaanza darasa la kwanza wanajua kusoma lkn zamani kusoma mtu unaanza la tatu tena kwa shida
 
Nilipokuwa nasoma bandiko lako, nilikuwa makini kutafuta makosa ya kiuandishi kutoka kwako ambayo si ya bahati mbaya bali ni matokeo ya walimu wako.

1. ebu=hebu
2. kiswahili=Kiswahili
 
Nilipokuwa nasoma bandiko lako, nilikuwa makini kutafuta makosa ya kiuandishi kutoka kwako ambayo si ya bahati mbaya bali ni matokeo ya walimu wako.

1. ebu=hebu
2. kiswahili=Kiswahili
Upo makini sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…