Hapa ndo huwa najiuliza kazi ya CWT ni nini
kazi yao kuchukua hela tu majukumu hawayajui
CWT haipo kwa maslahi ya walim. Someni katiba yake, kujiunga si lazma msiliwe pesa zenu
Kujiunga si lazima ndio, ila ujiunge usijiunge 2% yao wanachukua tu sasa huu si ni u.....!!!
sasa kijana hapo kwenye kusema eti degree wamepata wote unajichanganya na hujui unachoandika, inaonekana una lako jambo,wewe sema mshahara walimu wapya hawajapata acha kuleta longolongo za wenye degree eti wamepata.nakuonaga sana mara nyingi unakashifu wenye degree NAKUAHIDI USIPOACHA HIZI BANGI ZAKO NTAKUSHUGHULIKIA.
hapa halmashauri ya manyoni waliopata mshahara kwa walimu wa ajira mpya ni 2 kwa idara ya msingi na 35 kwa idara ya sekondari. Degree si kgezo cha kupata mshahara, tumeenda hadi kwa mkurugenzi hakwepo tukaonana na afisa utumishi wilaya majibu aliyotupa tusubir wa mwezi huu wa tano then tuandke barua ya madai ya mshahara wa mwezi wa nne. Yan tayari tushaingizwa kwenye madeni ya walimu!!
Mi hawajala hata mia siku wakinikata nitaandamana make mi sio mwanachama, na sitaki kusikia habari za CWTTatizo la walim ndo liko hapo,yaani hatuwezi kujisimamia! Kipindi mimi nafanya kazi ya ualimu tulifanyiwa kama hivyo tukaenda Kwa mwajiri wetu mkurugenzi tukiwa na katiba ya cwt mkononi, na tukamwandikia mkurugenzi kuwa tutamshitaki kwa sababu ameidhinisha makato ya mshahara bila ridhaa yetu.katiba ya cwt inaonesha ili uwe mwanachama ni lazima ufanye application na ujaze fomu,ndani ya zile formu una sign mwenyewe kuwa ukatwe hizo asilimia.pia katiba inaeleza kuwa kama hulipi michango ya uanachama basi unakuwa umepoteza sifa.kwa hyo mkurugenzi alituelewa na akasitisha makato na akataka tumalizane na cwt kwa wale wanaotaka. Nimefanya kazi ya ualim miaka 3 na pesa yangu cwt hawakuila hata senti moja.HEBU JISIMAMIENI!watu wananenepa kwa pesa zenu
Mi hawajala hata mia siku wakinikata nitaandamana make mi sio mwanachama, na sitaki kusikia habari za CWT
Hakatwi mtu hapa....
Tatizo letu walimu wengi hatuwezi kujisimamia! Nilipokuwa Mwalimu CWT walikata mshahara wetu tukaenda kwa Muajiri wetu (Mkurugenzi) tukiwa na Katiba ya CWT mkononi, na tukamwandikia kuwa tutamshitaki kwa sababu ameidhinisha makato ya mshahara wetu bila ridhaa yetu. Katiba ya CWT inaonesha ili uwe mwanachama ni lazima ufanye uombe (ufanye application) kwa kujaza fomu, ndani ya hizo fomu unasaini mwenyewe kuwa ukatwe hizo asilimia 2, pia Katiba hiyo inaeleza kuwa kama hulipi michango ya uanachama basi unakuwa umepoteza sifa ya uanachama. Kwa hayo Mkurugenzi alituelewa na akasitisha makato na akataka tumalizane na CWT kwa wale wanaotaka. Nimefanya kazi ya Ualimu miaka 3 na pesa yangu CWT hawakuila hata senti moja. HEBU JISIMAMIENI! Watu wananenepa kwa pesa zenu!!!
Wakati jana raisi akitangaza nyongeza ya mshahara kuna idadi kubwa ya walimu wapya walioajiriwa aprili ambao hawajapata mshahara mfano h/mashauri ya kilindi ni walimu wapya 15 tu walioingiziwa mshahara...halmashauri zingine ni watu 10~30 waliopata mshahara..Sasa CWT inafanya nini? na inavyoonyesha ni jambo la makusudi limefanyika maana wale wa degree wengi wamepata mshahara..jamani serikali iache utani hivi umpange mtu porini halafu usimpe mshahara unategemea aishije??
Wilaya ya Kyerwa na Karagwe ndio bado haijajulikana, hata hela ya kujikimu hawajapewa yote hapo unategemea nn....
Mi hawajala hata mia siku wakinikata nitaandamana make mi sio mwanachama, na sitaki kusikia habari za CWT
Edited but point noted.