Wakuu habari zenu kutokana na mabadiliko kuendelea na kutolewa list ya majina ya walimu wa sanaa,biashara na walimu wa sayansi na hisabati kuna haja walimu hao kwenda kuripoti kwenye vituo walivyopangiwa maana kama kujua sehemu wanazokwenda wameshajua toka siku walipotoa mjina hayo au wasubiri list itakayo tolewa upya maana huenda kukatokea mabadiliko, pili katika mkoa wa morogoro hasa wilaya ya Ulanga hakuna hata mwalimu mmoja wa cheti aliyeapangiwa wilaya hiyo. Swali langu ni kwamba walaya hiyo ya Ulanga walimu wa shule za msingi wametosha au laa maana kuna maeneo wanajenga shule mfano maeneo ya nalukoo katika wilaya hiyo, je walimu wa shule za msingi wametosha. Ni hayo tu wadau kama kuna mtu anajua zaidi ya hapo anakaribishwa kutujuza . Nawasilisha