Waliogundua hesabu ngumu walikuwa wanatafuta nini na walizigunduaje?

Waliogundua hesabu ngumu walikuwa wanatafuta nini na walizigunduaje?

Hesabu ni somo linalochukiza sana.
Tangu napata ufahamu nikiwa primary nilikua nafeli tu hesabu. Darasa la 4 mpaka la 7 nilikua napata 10% mpaka 20%, yaani 5/50 mpaka 10/50. Inshort primary nilikua mbumbumbu na mwonekano wa kimbumbumbu, mpaka nikawa nafananishwa na kilaza wa darasa, nikawa naitwa kwa jina la huyo kilaza.
Nilivyoanza sekondari nikaanza kujifunza mwenyewe kwenye kitabu bila kufundishwa. Nikawa najifunza mwenyewe kwa muda mrefu, kidato cha pili NECTA nikapata C (49%). Kutoka 10% - 20% mpaka 49% nikaona kumbe inawezekana!, likizo ya form 2 kwenda form 3 nikakazana nikawa najifunza mwenyewe kitabu cha form 3. Midterm ya form 3 nikapata 78% kumzidi aliyeongoza shule nzima kidato cha pili, yeye midterm alipata 77%, nikapata moyo zaidi. Nikamaliza book 3 na book 4 harakaharaka nikiwa form 3, nikiwa form 3 nikaanza kufanya mitihani ya form 4 na wanafunzi wa form 4, nikawa nawakimbiza form 4, grade As zikawa za kumwaga. Form 4 NECTA usiulize, nimetoka na banda la
Wera weraaaa; ingawa hata mleta UZI hajasema kwamba haiwezekani, yeye anacho uliza, hao wagunduzi walikua wanatafuta nini hadi wakagundua madude magumu gumu vile? But in fact unastahiri pongezi mkuu, well done hasa
 
Haa ha haha; halafu kwenye real life wala hazina impact yoyote yaani
Hakuna hesabu isiyokuwa na umuhimu,mimi kabla sijamaliza chuo,nilikua najiuliza haya mahesabu ya linear programming yana umuhimu gani katika maisha..baada ya kuingia kazini ndio nikagundua hayo mahesabu ni muhimu sana katika maisha yetu coz wachumi na wahasibu ndio wanayatumia katika planning na kuandaa budget mbalimbali.
 
Amna kigumu sema kichwa chako kigumu tuu.
mods futeni huu uzi
 
Einstein na Tesla Hawa watu walikuwa wako dunia yao
Screenshot_20211006-134525_Twitter.jpg
 
Ni katika hali ya kutafuta "ukweli" hakuna anaejua ukweli. Ukiulizwa "what's the truth" utajibu nini? Achana na mambo ya imani.
 
Tofautisha kwanza "hesabu" na "hisabati".

Halafu wenye hasabati yao watakuja kudadavua maswali yako.
 
Mi pia nina mtazamo kama wako! Kwa sababu kuna mambo mengine unaona kabisa kuwa kwa akili ya kawsida ya binadamu ni vigumu sana.

Juzi hapa na rafiki yangu tulikuwa tunaangalia ufanyaji kazi wa kitu kidogo tu, photocopy machine. Tukaangalia wingi wa vidudedude vilivyopo mle na jinsi inavyofanya kazi na kujiuliza hivi binadamu huyu alitumia miaka mingapi hadi kukamilisha hili? Mwishowe tukasema kama ulivyosema wewe mkuu, kwamba Mungu kuna alivyoamua kuvishusha kupitia tu binadamu
Nadra sana. Elimu/sayansi/techonolioia ni incremental. Kila mtu au kizazi kinaongezea pale kilipoishia kingine. Kwa hivyo ukitizama hiyo photocopier utaona ni muungiko wa technolojia mbali mbali.....kuanzia pulleys, wino, taa/mwanga, camera etc. Na yenyewe utaona overtime imekuwa na improvement kidogo kidogo.....pengine mwazo ilikuwa black na white na sasa coloured, etc.

Elimu mpya inajengwa juu ya msingi wa elimu ya zamani na ya sasa.
 
Back
Top Bottom