Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
Ilikuwa ni furaha na tabasamu kwa wanakijiji 10 wa Nkomelo wilayani Muleba mkoani Kagera baada ya kukabidhiwa nyumba zao mpya zkama sehemu ya fidia kwa ajili ya kupisha ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linalotarajiwa kuanza ujenzi baadae mwaka huu.
Nyumba hizo walizokabidhiwa wanakijiji hao zina huduma zote muhimu, ikiwa ni pamoja na majiko na vyoo vya nje, mifumo ya nishati ya jua, matenki kwa ajili ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita 5,000 kwa kila nyumba na vitu vingine muhimu yakiwemo madirisha ya kisasa ya vioo.
"Kusema kweli, sikuwahi kufikiria kumiliki nyumba nzuri kama hii maishani mwangu kwa sababu nilikuwa naishi kwenye nyumba ndogo ya udongo, lakini kumiliki nyumba ya kisasa ni jambo ambalo sikuwahi kufikiria hapo awali," alisema. Jovin Bebwa Thadeo mwenye umri wa miaka 67, baba wa watoto 15.
Dustan Muganyizi, 54, wakati akipokea ufunguo wa nyumba ya familia yake, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na furaha na hakuweza kuizuia furaha yake.
"Pia tulipokea pesa za fidia ambazo zilibadilisha maisha yetu kabisa kwa kutuwezesha kufanya vitu mbalimbali vya kimaendeleo kama vile kununua pikipiki, mashamba ya ziada, na Ng'ombe," amesema.
Muganyizi, baba wa familia ya watoto watano ameongeza kuwa kupewa nyumba ni sehemu ya fidia ambayo imeboresha maisha yao.
Wawakilishi waandamizi mbalimbali kutoka Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na viongozi wa serikali ya Muleba walihudhuria pia hafla hiyo ya kukabidhi nyumba hizo.
Mkurugenzi wa Biashara ya Petroli wa TPDC Dk. Wellington Hudson amesema jumla ya nyumba 292 zitajengwa kwa ajili ya watu walioathirika na mradi ambapo kati ya hizo, 58 tayari zimejengwa katika maeneo mbalimbali litakalopita bomba hilo.
Amesema makabidhiano hayo ya nyumba kwa walioguswa na mradi ni ishara tosha kwamba mchakato wa fidia kwa walioguswa na mradi unaendelea bila vikwazo vyovyote.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa EACOP Martin Tiffen , kabla ya kusaini mikataba, wananchi walioguswa na mradi walishirikishwa katika mchakato wa malipo na tathmini kwa ajili ya fidia zao.
Amesema kuwa watu 9898 walioguswa na mradi ambao ni sawa na asilimia 97 sehemu yao ya mashamba ndio yamepitiwa na mradi .
Amesema watu 344 ambao ni sawa na asilimia 3 iliyobaki, nyumba zao ndio zimepitiwa na mradi na zitabomolewa kwa ajili ya kupisha ujenzi wa bomba hilo la mafuta ghafi.
Bosi huyo wa EACOP aliongeza kuwa 90% ya watu hao ambao nyumba zao zinapitiwa na mradi walifanya uamuzi wa busara wa kuchagua kujengewa nyumba mbadala za zege ambazo zinajengwa na wakandarasi wazawa kwa kutumia ubunifu kutoka Afrika Kusini.
Aliongeza kuwa nyumba hizo mbadala ziko chini uangalizi (warantii ) kwa mwaka mmoja ambapo wakandarasi watawajibika kurekebisha uharibifu wowote utakaotokea katika kipindi hicho
𝐍𝐚𝐲𝐞 𝐌𝐰𝐞𝐧𝐲𝐞𝐤𝐢𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐁𝐨𝐝𝐢 𝐲𝐚 𝐖𝐚𝐤𝐮𝐫𝐮𝐠𝐞𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐌𝐚𝐦𝐥𝐚𝐤𝐚 𝐲𝐚 𝐔𝐝𝐡𝐢𝐛𝐢𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐇𝐮𝐝𝐮𝐦𝐚 𝐳𝐚 𝐍𝐢𝐬𝐡𝐚𝐭𝐢 𝐧𝐚 𝐌𝐚𝐣𝐢 (𝐄𝐖𝐔𝐑𝐀) 𝐏𝐫𝐨𝐟𝐞𝐬𝐚 𝐌𝐚𝐫𝐤 𝐌𝐰𝐚𝐧𝐝𝐨𝐬𝐲𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐩𝐨𝐧𝐠𝐞𝐳𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐲𝐚 𝐄𝐀𝐂𝐎𝐏 𝐤𝐮𝐤𝐚𝐛𝐢𝐝𝐡𝐢 𝐧𝐲𝐮𝐦𝐛𝐚 𝐡𝐢𝐳𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐥𝐞𝐧𝐠𝐰𝐚 𝐚𝐤𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐡𝐢𝐲𝐨 𝐢𝐧𝐚𝐭𝐨𝐚 𝐮𝐣𝐮𝐦𝐛𝐞 𝐤𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐨𝐩𝐢𝐧𝐠𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐨 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐡𝐚𝐤𝐢 𝐳𝐚 𝐛𝐢𝐧𝐚𝐝𝐚𝐦𝐮 𝐩𝐢𝐚 𝐳𝐢𝐧𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐚𝐭𝐢𝐰𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐞.
"𝐓𝐮𝐧𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐚𝐭𝐢𝐚 𝐦𝐚𝐭𝐚𝐤𝐰𝐚 𝐲𝐨𝐭𝐞 𝐲𝐚 𝐣𝐮𝐦𝐮𝐢𝐲𝐚 𝐳𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐚𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚 𝐢𝐤𝐢𝐰𝐚 𝐧𝐢 𝐩𝐚𝐦𝐨𝐣𝐚 𝐧𝐚 𝐮𝐥𝐢𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐢𝐫𝐚 𝐧𝐚 𝐮𝐡𝐢𝐟𝐚𝐝𝐡𝐢 𝐭𝐮𝐧𝐚𝐩𝐨𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐤𝐚𝐤𝐚𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚,".
"𝐓𝐮𝐥𝐢𝐚𝐡𝐢𝐝𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐭𝐮𝐭𝐚𝐥𝐢𝐧𝐝𝐚 𝐦𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐢𝐫𝐚 𝐧𝐚 𝐤𝐮𝐛𝐨𝐫𝐞𝐬𝐡𝐚 𝐦𝐚𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐲𝐚 𝐰𝐚𝐭𝐮 𝐰𝐞𝐭𝐮 𝐤𝐢𝐣𝐚𝐦𝐢𝐢 𝐧𝐚 𝐤𝐢𝐮𝐜𝐡𝐮𝐦𝐢", 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐏𝐫𝐨𝐟𝐞𝐬𝐚 𝐌𝐰𝐚𝐧𝐝𝐨𝐬𝐲𝐚, 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐞 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐡𝐢𝐤𝐚 𝐧𝐲𝐚𝐝𝐡𝐢𝐟𝐚 𝐭𝐨𝐟𝐚𝐮𝐭𝐢 𝐳𝐚 𝐔𝐰𝐚𝐳𝐢𝐫𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐬𝐞𝐫𝐢𝐤𝐚𝐥𝐢 𝐲𝐚 𝐚𝐰𝐚𝐦𝐮 𝐲𝐚 𝐧𝐧𝐞.
𝐀𝐳𝐢𝐳 𝐌𝐥𝐢𝐦𝐚, 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐞 𝐧𝐢 𝐁𝐚𝐥𝐨𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐔𝐠𝐚𝐧𝐝𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐢𝐤𝐨 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐧𝐳𝐮𝐫𝐢 𝐲𝐚 𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐧𝐚 𝐤𝐮𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐚𝐦𝐞𝐟𝐮𝐫𝐚𝐡𝐢𝐬𝐡𝐰𝐚 𝐧𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐢𝐥𝐢𝐲𝐨𝐟𝐢𝐤𝐢𝐰𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐦𝐚𝐞𝐧𝐞𝐨 𝐭𝐨𝐟𝐚𝐮𝐭𝐢 𝐲𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐨 𝐚𝐥𝐢𝐲𝐨𝐰𝐚𝐡𝐢 𝐤𝐮𝐲𝐚𝐭𝐞𝐦𝐛𝐞𝐥𝐞𝐚.
𝐍𝐭𝐚𝐤𝐢 𝐂𝐡𝐚𝐫𝐥𝐞𝐬 𝐌𝐚𝐲𝐮𝐧𝐠𝐚, 𝐊𝐚𝐢𝐦𝐮 𝐌𝐭𝐞𝐧𝐝𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐖𝐢𝐥𝐚𝐲𝐚 𝐲𝐚 𝐌𝐮𝐥𝐞𝐛𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐲𝐞𝐦𝐰𝐚𝐤𝐢𝐥𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐌𝐤𝐮𝐮 𝐰𝐚 𝐖𝐢𝐥𝐚𝐲𝐚 𝐀𝐛𝐞𝐥 𝐍𝐲𝐚𝐦𝐚𝐡𝐚𝐧𝐠𝐚 𝐚𝐦𝐞𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐮𝐣𝐞𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐧𝐲𝐮𝐦𝐛𝐚 𝐡𝐢𝐳𝐨 𝐮𝐦𝐞𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐧𝐚 𝐭𝐢𝐣𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐤𝐮𝐳𝐚 𝐮𝐜𝐡𝐮𝐦𝐢 𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐤𝐚𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐍𝐤𝐨𝐦𝐞𝐥𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐤𝐮𝐭𝐞𝐧𝐠𝐞𝐧𝐞𝐳𝐚 𝐚𝐣𝐢𝐫𝐚.
𝐄𝐀𝐂𝐎𝐏 𝐢𝐦𝐞𝐩𝐞𝐰𝐚 𝐥𝐞𝐬𝐞𝐧𝐢 𝐲𝐚 𝐤𝐮𝐣𝐞𝐧𝐠𝐚 𝐦𝐢𝐮𝐧𝐝𝐨𝐦𝐛𝐢𝐧𝐮 𝐲𝐚 𝐮𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐚𝐟𝐮𝐭𝐚 𝐠𝐡𝐚𝐟𝐢 𝐲𝐞𝐧𝐲𝐞 𝐮𝐫𝐞𝐟𝐮 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐥𝐨𝐦𝐢𝐭𝐚 1443 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐳𝐨 𝐳𝐢𝐭𝐚𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐦𝐚𝐟𝐮𝐭𝐚 𝐠𝐡𝐚𝐟𝐢 𝐤𝐮𝐭𝐨𝐤𝐚 𝐊𝐚𝐛𝐚𝐚𝐥𝐞 - 𝐇𝐨𝐢𝐦𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐔𝐠𝐚𝐧𝐝𝐚 𝐡𝐚𝐝𝐢 𝐂𝐡𝐨𝐧𝐠𝐨𝐥𝐞𝐚𝐧𝐢 𝐦𝐤𝐨𝐚𝐧𝐢 𝐓𝐚𝐧𝐠𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐚𝐣𝐢𝐥𝐢 𝐲𝐚 𝐤𝐮𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐬𝐨𝐤𝐨 𝐥𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐚𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚.
Nyumba hizo walizokabidhiwa wanakijiji hao zina huduma zote muhimu, ikiwa ni pamoja na majiko na vyoo vya nje, mifumo ya nishati ya jua, matenki kwa ajili ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita 5,000 kwa kila nyumba na vitu vingine muhimu yakiwemo madirisha ya kisasa ya vioo.
"Kusema kweli, sikuwahi kufikiria kumiliki nyumba nzuri kama hii maishani mwangu kwa sababu nilikuwa naishi kwenye nyumba ndogo ya udongo, lakini kumiliki nyumba ya kisasa ni jambo ambalo sikuwahi kufikiria hapo awali," alisema. Jovin Bebwa Thadeo mwenye umri wa miaka 67, baba wa watoto 15.
Dustan Muganyizi, 54, wakati akipokea ufunguo wa nyumba ya familia yake, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na furaha na hakuweza kuizuia furaha yake.
"Pia tulipokea pesa za fidia ambazo zilibadilisha maisha yetu kabisa kwa kutuwezesha kufanya vitu mbalimbali vya kimaendeleo kama vile kununua pikipiki, mashamba ya ziada, na Ng'ombe," amesema.
Muganyizi, baba wa familia ya watoto watano ameongeza kuwa kupewa nyumba ni sehemu ya fidia ambayo imeboresha maisha yao.
Wawakilishi waandamizi mbalimbali kutoka Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na viongozi wa serikali ya Muleba walihudhuria pia hafla hiyo ya kukabidhi nyumba hizo.
Mkurugenzi wa Biashara ya Petroli wa TPDC Dk. Wellington Hudson amesema jumla ya nyumba 292 zitajengwa kwa ajili ya watu walioathirika na mradi ambapo kati ya hizo, 58 tayari zimejengwa katika maeneo mbalimbali litakalopita bomba hilo.
Amesema makabidhiano hayo ya nyumba kwa walioguswa na mradi ni ishara tosha kwamba mchakato wa fidia kwa walioguswa na mradi unaendelea bila vikwazo vyovyote.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa EACOP Martin Tiffen , kabla ya kusaini mikataba, wananchi walioguswa na mradi walishirikishwa katika mchakato wa malipo na tathmini kwa ajili ya fidia zao.
Amesema kuwa watu 9898 walioguswa na mradi ambao ni sawa na asilimia 97 sehemu yao ya mashamba ndio yamepitiwa na mradi .
Amesema watu 344 ambao ni sawa na asilimia 3 iliyobaki, nyumba zao ndio zimepitiwa na mradi na zitabomolewa kwa ajili ya kupisha ujenzi wa bomba hilo la mafuta ghafi.
Bosi huyo wa EACOP aliongeza kuwa 90% ya watu hao ambao nyumba zao zinapitiwa na mradi walifanya uamuzi wa busara wa kuchagua kujengewa nyumba mbadala za zege ambazo zinajengwa na wakandarasi wazawa kwa kutumia ubunifu kutoka Afrika Kusini.
Aliongeza kuwa nyumba hizo mbadala ziko chini uangalizi (warantii ) kwa mwaka mmoja ambapo wakandarasi watawajibika kurekebisha uharibifu wowote utakaotokea katika kipindi hicho
𝐍𝐚𝐲𝐞 𝐌𝐰𝐞𝐧𝐲𝐞𝐤𝐢𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐁𝐨𝐝𝐢 𝐲𝐚 𝐖𝐚𝐤𝐮𝐫𝐮𝐠𝐞𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐌𝐚𝐦𝐥𝐚𝐤𝐚 𝐲𝐚 𝐔𝐝𝐡𝐢𝐛𝐢𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐇𝐮𝐝𝐮𝐦𝐚 𝐳𝐚 𝐍𝐢𝐬𝐡𝐚𝐭𝐢 𝐧𝐚 𝐌𝐚𝐣𝐢 (𝐄𝐖𝐔𝐑𝐀) 𝐏𝐫𝐨𝐟𝐞𝐬𝐚 𝐌𝐚𝐫𝐤 𝐌𝐰𝐚𝐧𝐝𝐨𝐬𝐲𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐩𝐨𝐧𝐠𝐞𝐳𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐲𝐚 𝐄𝐀𝐂𝐎𝐏 𝐤𝐮𝐤𝐚𝐛𝐢𝐝𝐡𝐢 𝐧𝐲𝐮𝐦𝐛𝐚 𝐡𝐢𝐳𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐥𝐞𝐧𝐠𝐰𝐚 𝐚𝐤𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐡𝐢𝐲𝐨 𝐢𝐧𝐚𝐭𝐨𝐚 𝐮𝐣𝐮𝐦𝐛𝐞 𝐤𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐨𝐩𝐢𝐧𝐠𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐨 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐡𝐚𝐤𝐢 𝐳𝐚 𝐛𝐢𝐧𝐚𝐝𝐚𝐦𝐮 𝐩𝐢𝐚 𝐳𝐢𝐧𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐚𝐭𝐢𝐰𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚𝐤𝐞.
"𝐓𝐮𝐧𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐚𝐭𝐢𝐚 𝐦𝐚𝐭𝐚𝐤𝐰𝐚 𝐲𝐨𝐭𝐞 𝐲𝐚 𝐣𝐮𝐦𝐮𝐢𝐲𝐚 𝐳𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐚𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚 𝐢𝐤𝐢𝐰𝐚 𝐧𝐢 𝐩𝐚𝐦𝐨𝐣𝐚 𝐧𝐚 𝐮𝐥𝐢𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐢𝐫𝐚 𝐧𝐚 𝐮𝐡𝐢𝐟𝐚𝐝𝐡𝐢 𝐭𝐮𝐧𝐚𝐩𝐨𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐤𝐚𝐤𝐚𝐭𝐢 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚,".
"𝐓𝐮𝐥𝐢𝐚𝐡𝐢𝐝𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐭𝐮𝐭𝐚𝐥𝐢𝐧𝐝𝐚 𝐦𝐚𝐳𝐢𝐧𝐠𝐢𝐫𝐚 𝐧𝐚 𝐤𝐮𝐛𝐨𝐫𝐞𝐬𝐡𝐚 𝐦𝐚𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐲𝐚 𝐰𝐚𝐭𝐮 𝐰𝐞𝐭𝐮 𝐤𝐢𝐣𝐚𝐦𝐢𝐢 𝐧𝐚 𝐤𝐢𝐮𝐜𝐡𝐮𝐦𝐢", 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐏𝐫𝐨𝐟𝐞𝐬𝐚 𝐌𝐰𝐚𝐧𝐝𝐨𝐬𝐲𝐚, 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐞 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐡𝐢𝐤𝐚 𝐧𝐲𝐚𝐝𝐡𝐢𝐟𝐚 𝐭𝐨𝐟𝐚𝐮𝐭𝐢 𝐳𝐚 𝐔𝐰𝐚𝐳𝐢𝐫𝐢 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐬𝐞𝐫𝐢𝐤𝐚𝐥𝐢 𝐲𝐚 𝐚𝐰𝐚𝐦𝐮 𝐲𝐚 𝐧𝐧𝐞.
𝐀𝐳𝐢𝐳 𝐌𝐥𝐢𝐦𝐚, 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐲𝐞 𝐧𝐢 𝐁𝐚𝐥𝐨𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐔𝐠𝐚𝐧𝐝𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐢𝐤𝐨 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐧𝐳𝐮𝐫𝐢 𝐲𝐚 𝐮𝐭𝐞𝐤𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐮 𝐧𝐚 𝐤𝐮𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐚𝐦𝐞𝐟𝐮𝐫𝐚𝐡𝐢𝐬𝐡𝐰𝐚 𝐧𝐚 𝐡𝐚𝐭𝐮𝐚 𝐢𝐥𝐢𝐲𝐨𝐟𝐢𝐤𝐢𝐰𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐦𝐚𝐞𝐧𝐞𝐨 𝐭𝐨𝐟𝐚𝐮𝐭𝐢 𝐲𝐚 𝐦𝐫𝐚𝐝𝐢 𝐡𝐮𝐨 𝐚𝐥𝐢𝐲𝐨𝐰𝐚𝐡𝐢 𝐤𝐮𝐲𝐚𝐭𝐞𝐦𝐛𝐞𝐥𝐞𝐚.
𝐍𝐭𝐚𝐤𝐢 𝐂𝐡𝐚𝐫𝐥𝐞𝐬 𝐌𝐚𝐲𝐮𝐧𝐠𝐚, 𝐊𝐚𝐢𝐦𝐮 𝐌𝐭𝐞𝐧𝐝𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐖𝐢𝐥𝐚𝐲𝐚 𝐲𝐚 𝐌𝐮𝐥𝐞𝐛𝐚 𝐚𝐥𝐢𝐲𝐞𝐦𝐰𝐚𝐤𝐢𝐥𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐌𝐤𝐮𝐮 𝐰𝐚 𝐖𝐢𝐥𝐚𝐲𝐚 𝐀𝐛𝐞𝐥 𝐍𝐲𝐚𝐦𝐚𝐡𝐚𝐧𝐠𝐚 𝐚𝐦𝐞𝐬𝐞𝐦𝐚 𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐮𝐣𝐞𝐧𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐧𝐲𝐮𝐦𝐛𝐚 𝐡𝐢𝐳𝐨 𝐮𝐦𝐞𝐤𝐮𝐰𝐚 𝐧𝐚 𝐭𝐢𝐣𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐤𝐮𝐳𝐚 𝐮𝐜𝐡𝐮𝐦𝐢 𝐰𝐚 𝐰𝐚𝐤𝐚𝐳𝐢 𝐰𝐚 𝐍𝐤𝐨𝐦𝐞𝐥𝐨 𝐤𝐰𝐚 𝐤𝐮𝐭𝐞𝐧𝐠𝐞𝐧𝐞𝐳𝐚 𝐚𝐣𝐢𝐫𝐚.
𝐄𝐀𝐂𝐎𝐏 𝐢𝐦𝐞𝐩𝐞𝐰𝐚 𝐥𝐞𝐬𝐞𝐧𝐢 𝐲𝐚 𝐤𝐮𝐣𝐞𝐧𝐠𝐚 𝐦𝐢𝐮𝐧𝐝𝐨𝐦𝐛𝐢𝐧𝐮 𝐲𝐚 𝐮𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚𝐣𝐢 𝐰𝐚 𝐦𝐚𝐟𝐮𝐭𝐚 𝐠𝐡𝐚𝐟𝐢 𝐲𝐞𝐧𝐲𝐞 𝐮𝐫𝐞𝐟𝐮 𝐰𝐚 𝐤𝐢𝐥𝐨𝐦𝐢𝐭𝐚 1443 𝐚𝐦𝐛𝐚𝐳𝐨 𝐳𝐢𝐭𝐚𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐦𝐚𝐟𝐮𝐭𝐚 𝐠𝐡𝐚𝐟𝐢 𝐤𝐮𝐭𝐨𝐤𝐚 𝐊𝐚𝐛𝐚𝐚𝐥𝐞 - 𝐇𝐨𝐢𝐦𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐔𝐠𝐚𝐧𝐝𝐚 𝐡𝐚𝐝𝐢 𝐂𝐡𝐨𝐧𝐠𝐨𝐥𝐞𝐚𝐧𝐢 𝐦𝐤𝐨𝐚𝐧𝐢 𝐓𝐚𝐧𝐠𝐚 𝐧𝐜𝐡𝐢𝐧𝐢 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐚𝐣𝐢𝐥𝐢 𝐲𝐚 𝐤𝐮𝐬𝐚𝐟𝐢𝐫𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐤𝐚𝐭𝐢𝐤𝐚 𝐬𝐨𝐤𝐨 𝐥𝐚 𝐤𝐢𝐦𝐚𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚.