Walioguswa na Mradi wa Bomba la Mafuta Nkomelo wakabidhiwa nyumba zao mpya

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
Ilikuwa ni furaha na tabasamu kwa wanakijiji 10 wa Nkomelo wilayani Muleba mkoani Kagera baada ya kukabidhiwa nyumba zao mpya zkama sehemu ya fidia kwa ajili ya kupisha ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linalotarajiwa kuanza ujenzi baadae mwaka huu.

Nyumba hizo walizokabidhiwa wanakijiji hao zina huduma zote muhimu, ikiwa ni pamoja na majiko na vyoo vya nje, mifumo ya nishati ya jua, matenki kwa ajili ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita 5,000 kwa kila nyumba na vitu vingine muhimu yakiwemo madirisha ya kisasa ya vioo.

"Kusema kweli, sikuwahi kufikiria kumiliki nyumba nzuri kama hii maishani mwangu kwa sababu nilikuwa naishi kwenye nyumba ndogo ya udongo, lakini kumiliki nyumba ya kisasa ni jambo ambalo sikuwahi kufikiria hapo awali," alisema. Jovin Bebwa Thadeo mwenye umri wa miaka 67, baba wa watoto 15.

Dustan Muganyizi, 54, wakati akipokea ufunguo wa nyumba ya familia yake, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na furaha na hakuweza kuizuia furaha yake.

"Pia tulipokea pesa za fidia ambazo zilibadilisha maisha yetu kabisa kwa kutuwezesha kufanya vitu mbalimbali vya kimaendeleo kama vile kununua pikipiki, mashamba ya ziada, na Ng'ombe," amesema.

Muganyizi, baba wa familia ya watoto watano ameongeza kuwa kupewa nyumba ni sehemu ya fidia ambayo imeboresha maisha yao.

Wawakilishi waandamizi mbalimbali kutoka Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na viongozi wa serikali ya Muleba walihudhuria pia hafla hiyo ya kukabidhi nyumba hizo.

Mkurugenzi wa Biashara ya Petroli wa TPDC Dk. Wellington Hudson amesema jumla ya nyumba 292 zitajengwa kwa ajili ya watu walioathirika na mradi ambapo kati ya hizo, 58 tayari zimejengwa katika maeneo mbalimbali litakalopita bomba hilo.

Amesema makabidhiano hayo ya nyumba kwa walioguswa na mradi ni ishara tosha kwamba mchakato wa fidia kwa walioguswa na mradi unaendelea bila vikwazo vyovyote.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa EACOP Martin Tiffen , kabla ya kusaini mikataba, wananchi walioguswa na mradi walishirikishwa katika mchakato wa malipo na tathmini kwa ajili ya fidia zao.

Amesema kuwa watu 9898 walioguswa na mradi ambao ni sawa na asilimia 97 sehemu yao ya mashamba ndio yamepitiwa na mradi .

Amesema watu 344 ambao ni sawa na asilimia 3 iliyobaki, nyumba zao ndio zimepitiwa na mradi na zitabomolewa kwa ajili ya kupisha ujenzi wa bomba hilo la mafuta ghafi.

Bosi huyo wa EACOP aliongeza kuwa 90% ya watu hao ambao nyumba zao zinapitiwa na mradi walifanya uamuzi wa busara wa kuchagua kujengewa nyumba mbadala za zege ambazo zinajengwa na wakandarasi wazawa kwa kutumia ubunifu kutoka Afrika Kusini.

Aliongeza kuwa nyumba hizo mbadala ziko chini uangalizi (warantii ) kwa mwaka mmoja ambapo wakandarasi watawajibika kurekebisha uharibifu wowote utakaotokea katika kipindi hicho
๐๐š๐ฒ๐ž ๐Œ๐ฐ๐ž๐ง๐ฒ๐ž๐ค๐ข๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐๐จ๐๐ข ๐ฒ๐š ๐–๐š๐ค๐ฎ๐ซ๐ฎ๐ ๐ž๐ง๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐Œ๐š๐ฆ๐ฅ๐š๐ค๐š ๐ฒ๐š ๐”๐๐ก๐ข๐›๐ข๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐‡๐ฎ๐๐ฎ๐ฆ๐š ๐ณ๐š ๐๐ข๐ฌ๐ก๐š๐ญ๐ข ๐ง๐š ๐Œ๐š๐ฃ๐ข (๐„๐–๐”๐‘๐€) ๐๐ซ๐จ๐Ÿ๐ž๐ฌ๐š ๐Œ๐š๐ซ๐ค ๐Œ๐ฐ๐š๐ง๐๐จ๐ฌ๐ฒ๐š ๐š๐ฅ๐ข๐ฉ๐จ๐ง๐ ๐ž๐ณ๐š ๐ก๐š๐ญ๐ฎ๐š ๐ฒ๐š ๐„๐€๐‚๐Ž๐ ๐ค๐ฎ๐ค๐š๐›๐ข๐๐ก๐ข ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š ๐ก๐ข๐ณ๐จ ๐ค๐ฐ๐š ๐ฐ๐š๐ฅ๐ž๐ง๐ ๐ฐ๐š ๐š๐ค๐ข๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐ก๐š๐ญ๐ฎ๐š ๐ก๐ข๐ฒ๐จ ๐ข๐ง๐š๐ญ๐จ๐š ๐ฎ๐ฃ๐ฎ๐ฆ๐›๐ž ๐ค๐ฐ๐š ๐ฐ๐š๐ง๐š๐จ๐ฉ๐ข๐ง๐ ๐š ๐ฆ๐ซ๐š๐๐ข ๐ก๐ฎ๐จ ๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐ก๐š๐ค๐ข ๐ณ๐š ๐›๐ข๐ง๐š๐๐š๐ฆ๐ฎ ๐ฉ๐ข๐š ๐ณ๐ข๐ง๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐š๐ญ๐ข๐ฐ๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฎ๐ญ๐ž๐ค๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š๐ค๐ž.

"๐“๐ฎ๐ง๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐š๐ญ๐ข๐š ๐ฆ๐š๐ญ๐š๐ค๐ฐ๐š ๐ฒ๐จ๐ญ๐ž ๐ฒ๐š ๐ฃ๐ฎ๐ฆ๐ฎ๐ข๐ฒ๐š ๐ณ๐š ๐ค๐ข๐ฆ๐š๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š ๐ข๐ค๐ข๐ฐ๐š ๐ง๐ข ๐ฉ๐š๐ฆ๐จ๐ฃ๐š ๐ง๐š ๐ฎ๐ฅ๐ข๐ง๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐ฆ๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ซ๐š ๐ง๐š ๐ฎ๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ญ๐ฎ๐ง๐š๐ฉ๐จ๐ญ๐ž๐ค๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š ๐ฆ๐ซ๐š๐๐ข ๐ก๐ฎ๐ฎ ๐ฐ๐š ๐ค๐ข๐ฆ๐ค๐š๐ค๐š๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐ค๐ข๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š,".

"๐“๐ฎ๐ฅ๐ข๐š๐ก๐ข๐๐ข ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ค๐ฎ๐ญ๐ž๐ค๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š ๐ฆ๐ซ๐š๐๐ข ๐ก๐ฎ๐ฎ ๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐ญ๐ฎ๐ญ๐š๐ฅ๐ข๐ง๐๐š ๐ฆ๐š๐ณ๐ข๐ง๐ ๐ข๐ซ๐š ๐ง๐š ๐ค๐ฎ๐›๐จ๐ซ๐ž๐ฌ๐ก๐š ๐ฆ๐š๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐ฒ๐š ๐ฐ๐š๐ญ๐ฎ ๐ฐ๐ž๐ญ๐ฎ ๐ค๐ข๐ฃ๐š๐ฆ๐ข๐ข ๐ง๐š ๐ค๐ข๐ฎ๐œ๐ก๐ฎ๐ฆ๐ข", ๐š๐ฅ๐ข๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐๐ซ๐จ๐Ÿ๐ž๐ฌ๐š ๐Œ๐ฐ๐š๐ง๐๐จ๐ฌ๐ฒ๐š, ๐š๐ฆ๐›๐š๐ฒ๐ž ๐š๐ฅ๐ข๐ฌ๐ก๐ข๐ค๐š ๐ง๐ฒ๐š๐๐ก๐ข๐Ÿ๐š ๐ญ๐จ๐Ÿ๐š๐ฎ๐ญ๐ข ๐ณ๐š ๐”๐ฐ๐š๐ณ๐ข๐ซ๐ข ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฌ๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐ฒ๐š ๐š๐ฐ๐š๐ฆ๐ฎ ๐ฒ๐š ๐ง๐ง๐ž.

๐€๐ณ๐ข๐ณ ๐Œ๐ฅ๐ข๐ฆ๐š, ๐š๐ฆ๐›๐š๐ฒ๐ž ๐ง๐ข ๐๐š๐ฅ๐จ๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐“๐š๐ง๐ณ๐š๐ง๐ข๐š ๐ง๐œ๐ก๐ข๐ง๐ข ๐”๐ ๐š๐ง๐๐š ๐š๐ฅ๐ข๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐“๐š๐ง๐ณ๐š๐ง๐ข๐š ๐ข๐ค๐จ ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ก๐š๐ญ๐ฎ๐š ๐ง๐ณ๐ฎ๐ซ๐ข ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ญ๐ž๐ค๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š ๐ฆ๐ซ๐š๐๐ข ๐ก๐ฎ๐ฎ ๐ง๐š ๐ค๐ฎ๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐š๐ฆ๐ž๐Ÿ๐ฎ๐ซ๐š๐ก๐ข๐ฌ๐ก๐ฐ๐š ๐ง๐š ๐ก๐š๐ญ๐ฎ๐š ๐ข๐ฅ๐ข๐ฒ๐จ๐Ÿ๐ข๐ค๐ข๐ฐ๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฆ๐š๐ž๐ง๐ž๐จ ๐ญ๐จ๐Ÿ๐š๐ฎ๐ญ๐ข ๐ฒ๐š ๐ฆ๐ซ๐š๐๐ข ๐ก๐ฎ๐จ ๐š๐ฅ๐ข๐ฒ๐จ๐ฐ๐š๐ก๐ข ๐ค๐ฎ๐ฒ๐š๐ญ๐ž๐ฆ๐›๐ž๐ฅ๐ž๐š.

๐๐ญ๐š๐ค๐ข ๐‚๐ก๐š๐ซ๐ฅ๐ž๐ฌ ๐Œ๐š๐ฒ๐ฎ๐ง๐ ๐š, ๐Š๐š๐ข๐ฆ๐ฎ ๐Œ๐ญ๐ž๐ง๐๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š ๐–๐ข๐ฅ๐š๐ฒ๐š ๐ฒ๐š ๐Œ๐ฎ๐ฅ๐ž๐›๐š ๐š๐ฅ๐ข๐ฒ๐ž๐ฆ๐ฐ๐š๐ค๐ข๐ฅ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐Œ๐ค๐ฎ๐ฎ ๐ฐ๐š ๐–๐ข๐ฅ๐š๐ฒ๐š ๐€๐›๐ž๐ฅ ๐๐ฒ๐š๐ฆ๐š๐ก๐š๐ง๐ ๐š ๐š๐ฆ๐ž๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š ๐ก๐ข๐ณ๐จ ๐ฎ๐ฆ๐ž๐ค๐ฎ๐ฐ๐š ๐ง๐š ๐ญ๐ข๐ฃ๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ค๐ฎ๐ค๐ฎ๐ณ๐š ๐ฎ๐œ๐ก๐ฎ๐ฆ๐ข ๐ฐ๐š ๐ฐ๐š๐ค๐š๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐๐ค๐จ๐ฆ๐ž๐ฅ๐จ ๐ค๐ฐ๐š ๐ค๐ฎ๐ญ๐ž๐ง๐ ๐ž๐ง๐ž๐ณ๐š ๐š๐ฃ๐ข๐ซ๐š.

๐„๐€๐‚๐Ž๐ ๐ข๐ฆ๐ž๐ฉ๐ž๐ฐ๐š ๐ฅ๐ž๐ฌ๐ž๐ง๐ข ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ ๐š ๐ฆ๐ข๐ฎ๐ง๐๐จ๐ฆ๐›๐ข๐ง๐ฎ ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ฌ๐š๐Ÿ๐ข๐ซ๐ข๐ฌ๐ก๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š ๐ฆ๐š๐Ÿ๐ฎ๐ญ๐š ๐ ๐ก๐š๐Ÿ๐ข ๐ฒ๐ž๐ง๐ฒ๐ž ๐ฎ๐ซ๐ž๐Ÿ๐ฎ ๐ฐ๐š ๐ค๐ข๐ฅ๐จ๐ฆ๐ข๐ญ๐š 1443 ๐š๐ฆ๐›๐š๐ณ๐จ ๐ณ๐ข๐ญ๐š๐ฌ๐š๐Ÿ๐ข๐ซ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐ฆ๐š๐Ÿ๐ฎ๐ญ๐š ๐ ๐ก๐š๐Ÿ๐ข ๐ค๐ฎ๐ญ๐จ๐ค๐š ๐Š๐š๐›๐š๐š๐ฅ๐ž - ๐‡๐จ๐ข๐ฆ๐š ๐ง๐œ๐ก๐ข๐ง๐ข ๐”๐ ๐š๐ง๐๐š ๐ก๐š๐๐ข ๐‚๐ก๐จ๐ง๐ ๐จ๐ฅ๐ž๐š๐ง๐ข ๐ฆ๐ค๐จ๐š๐ง๐ข ๐“๐š๐ง๐ ๐š ๐ง๐œ๐ก๐ข๐ง๐ข ๐“๐š๐ง๐ณ๐š๐ง๐ข๐š ๐ค๐ฐ๐š ๐š๐ฃ๐ข๐ฅ๐ข ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ฌ๐š๐Ÿ๐ข๐ซ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฌ๐จ๐ค๐จ ๐ฅ๐š ๐ค๐ข๐ฆ๐š๐ญ๐š๐ข๐Ÿ๐š.

 
Una taka mtu ajengewe nyumba ya vyumba kumi wakati wa tathimini alikuwa na tembe ya chumba kimoja?

Wamewekewa na maji ambayo hawa kuwa nayo
Choo cha kisasa ambacho hawa kuwa navyo
Umeme ambao hawa kuwa nao
Tank la maji, una weza vuna ya mvua, kitu ambacho hawa kuwa navyo nk
Leo wengine wana lalamika et nyumba ndogo... udogo wake nini?

Nyumba hizo walizokabidhiwa wanakijiji hao zina huduma zote muhimu, ikiwa ni pamoja na majiko na vyoo vya nje, mifumo ya nishati ya jua, matenki kwa ajili ya kuhifadhia maji yenye ujazo wa lita 5,000 kwa kila nyumba na vitu vingine muhimu yakiwemo madirisha ya kisasa ya vioo.

"Pia tulipokea pesa za fidia ambazo zilibadilisha maisha yetu kabisa kwa kutuwezesha kufanya vitu mbalimbali vya kimaendeleo kama vile kununua pikipiki, mashamba ya ziada, na Ng'ombe," amesema.
 
Watoto 15 Kwa nyumba hiyo inakuwaje?
 
Unakuta fidia ilikuwa 60M ila kanyumba ni ka 20M kalikopigwa finishing kali kuwapumbaza wananchi hao na kudanganywa gharama ni 50M. Kisha anapewa na million 10 cash asijue kumbe kapigwa 30M juu kwa juu.
all is possible!
 
Achana nao ni uwivu unawasumbua.

Kwa hili la nyumba mm nawapongeza wahusika ni jambo nzuri.
 
Vipi waguswa wa ardhi? kuna watu ardhi zao zimetwaliwa na mradi na baada ya fidia wakahaidiwa kupewa chakula na mbolea kwa kipindi cha mwaka mzima, la ajabu mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambae ameishapewa hivyo vitu vilivyoahidiwa.

Pili, walisema wenyeji wa eneo husika watanufaika na fursa za mradi (Local content) watu wakafuata taratibu na kujisajiri makampuni yao kwenye kanzidata ya EWURA la kushangaza mpaka sasa hakuna cha local content wala nini, kinachoendelea mpaka sasa shetani ndiye anajua.

UkiwaulIza wahusika wa EACOP nini kinajili wanasema wamekuwa overpowered na TPDC, habari ndiyo hiyo tusidanganyane huu mradi umegubikwa na sintofahamu nyingi na janjajanja nyingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ