Waliomuua Dkt. Isack wa Nyamongo HC wakamatwe haraka

Waliomuua Dkt. Isack wa Nyamongo HC wakamatwe haraka

HustlerD

Senior Member
Joined
May 15, 2021
Posts
131
Reaction score
428
Nawasalimu wote wakubwa kwa wadogo,

Ni usiku wa kuamkia leo nimepokea taarifa kutoka kwa watu wangu wa karibu kua kuna daktari ameuawa kwa kukatwa katwa mapanga katika mji wa Nyamongo wilaya ya Tarime.

Daktari huyo kijana mdogo kabisa aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Afya Nyamongo(Nyamongo HC) amekutwa na umauti huo wakati akiwa anaendesha pikipiki yake kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine katika mji huo.

Bado chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana, na wala sina taarifa yoyote kuhusiana na kukamatwa kwa wahusika wa tukio hilo.

Ni aibu kubwa Kwa mji huo kumuua mtumishi tena kwa kumkata kata kwa mapanga wakati huu ambao kumekua na uhaba wa watumishi hasa kada ya afya katika maeneo ya pembezoni ya nchi. Je, ni nani atakubali kwenda kufanya kazi katika eneo kama hilo ambalo linaonekana si salama tena kwa watumishi na ukizingatia ajira za TAMISEMI zimetangazwa juzi.

Haijalishi sababu ya kifo itakuwa nini lakini huu ni ukatili wa hali ya juu.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Dr Isack Sima Mahala pema peponi, Amina.
 
Kwa nyamongo lazima itakuwa anatuhumiwa kutembea na mchepuko wa mtu, nielewe sio mke wa mtu, mchepuko wa mtu!

Yule majamaa ni bora yakukute na mkewe yanaweza kabisa kukusamehe ila sio akukute na mchepuko wake
 
Kanda ya ziwa hasa Mara,musoma.,kagera ni watu wa ajabu Sana,Hawa jamaa kukata mtu mapanga imekuwa Kama jadi Sasa,ni maeneo hatari Sana haya,Kuna classmate wangu tulipotezana miaka kadhaa baada ya kumaliza chuo ,majuz hivi tukakutana kwenye event moja hivi ya mh.rais jijini Dodoma ,kumchek jamaa usoni ana lialama la mkato wa panga Ila limepona so kabaki na lialama la kukatwa,sikutaka kumuuliza kulikoni mkuu li ngeu panga usoni ,maana tulikuwa serious kidogo na event ,yeye alikuwa huko Mara kikazi bt baadae alifanya transfer kutoka kule.
 
Nawasalimu wote wakubwa kwa wadogo,

Ni usiku wa kuamkia leo nimepokea taarifa kutoka kwa watu wangu wa karibu kua kuna dakitari ameuawa kwa kukatwa katwa mapanga katika mji wa Nyamongo wilaya ya Tarime.

Dakitari huyo kijana mdogo kabisa aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Afya Nyamongo(Nyamongo HC) amekutwa na umauti huo wakati akiwa anaendesha pikipiki yake kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine katika mji huo.

Bado chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana, na wala sina taarifa yoyote kuhusiana na kukamatwa kwa wahusika wa tukio hilo.

Ni aibu kubwa Kwa mji huo kumuua mtumishi tena kwa kumkata kata kwa mapanga wakati huu ambao kumekua na uhaba wa watumishi hasa kada ya afya katika maeneo ya pembezoni ya nchi, je ni nani atakubali kwenda kufanya kazi katika eneo kama hilo ambalo linaonekana si salama tena kwa watumishi na ukizingatia ajira za TAMISEMI zimetangazwa juzi,

Haijalishi sababu ya kifo itakuwa nini lakini huu ni ukatili wa hali ya juu

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Dr Isack Sima Mahala pema peponi, Amina
Cc Ushimen
 
Back
Top Bottom