Waliondamana Dar es Salaam kupinga mkataba wa bandari wakamatwa na polisi. Mratibu wa maandamano na wenzake 10 wanahojiwa na Polisi

Mkuu vijana wa enzi ya Nyerere na Mwinyi walikuwa jasiri, waliandamana hata watoto wa shule walikuwa wanaandamana; lakini hawa wa leo wala chips, wengine waoga, wanafiki, chawa hawawezi kuandamana, wengine kazi yao ni kuwachongea wenzao tu.

Hata Bungeni; lile la zamani lilikuwa bora hasa, Mawaziri walikuwa wanajipanga na majibu ya uhakika. Nadhani mnalikumbuka lile G55 lilimwinua Mwalimu kutoka Msasani hadi IBungeni kusawazisha mambo.
 
Maanda ya watu hawazidi watano ni maandamano gani hayo?
 
Mods acheni tabia ya kufuta nyuzi na kuunganisha mada hovyo..

Gazeti Lina heading niliyonukuu nyie mnafuta Kwa maslahi gani?
 
Kibaya zaidi huyu Deus Soka ni kutoka familia maskini kabisa na anadanganywa na hawa wahuni ambao wamekula na kushiba kama mzee mbowe,lissu na Lema
 
Mungu awabariki walioandamana.

Wamedhihirisha kwa vitendo Uzalendo kwa nchi yao.
Eeh ila nyie kazi yenu ni kuandamana nyuma ya keyboard wakikamatwa watu wanatudi hapa kuwapongeza
 
Huyo askari aliyemkamata muandamanaji naomba anikamate na mimi, nipo Tegeta.
 
Hii ndio Taarifa mpya ya sasa kutokea Mnazi Mmoja , Dar es Salaam .

Miongoni mwa Maelfu ya Waandamanaji wa kupinga Mauzo ya Bandari kuna Dada mmoja ambaye ametajwa kuwa shujaa wa Taifa hasa baada ya kujitokeza mstari wa Mbele bila kujali vitisho vya Polisi .

Mpeni Maua yake .

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…