Waliopanda ndege ya Mama kwenda Algeria ni mashabaiki wa Yanga SC au wavaa suti tu wanaokwenda kutalii na kupiga selfie?

Kwa sababu ni suala la Yanga umejifanya mwanaharakati sana na kubana bajeti.
 
Wawe mashabiki ama wavaa suti,ukweli ni kwmb muhimu ni bench la ufundi na utayar wa wachezaji kupambana ndo kitakacholeta matokeo chanya
 
Nendeni mkachapwe nchi itukie 😎
 
Ingepewa Simba hiyo ndege ungesemaje??
Mbona mataifa ya wenzetu wanasapotiwa na viongozi wao.

Acha kisokolokwinyo we mzee.
Haya mambo utayakuta huku kwa Waswahili tu wasiojitambua. Serikali inatoa ndege kusapoti safari ya KLABU, umeona wapi? Tena sapoti inatolewa kipindi haihitajiki, kipindi hizi klabu zinayumba kifedha umewahi kuona serikali inatoa hiyo sapoti?
 
Huwezi kwenda wakati huwezi kununua hata maji ya wachezaji, asilimia kubwa wameenda watu ambao wanaweza kuongeza motivation kwa Timu na siyo unaenda huko na hela yako ya kodi ya nyumba Kwa Mnyamani ukirudi unatimuliwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…