Elections 2010 Waliopiga kura Oktoba 31, milioni 12 walienda wapi Jumapili ile?

Elections 2010 Waliopiga kura Oktoba 31, milioni 12 walienda wapi Jumapili ile?

nimejumlisha kwa kichwa tu hapa inanipa milioni 4.85.. tukiwafuta hao wote tunabakia bado na kama milioni 14.25 .. inabidi uongeze idadi wengine wa kuwafuta ni kiasi gani na kina nani?

MM hapa kwa kifupi ni kuwa hii orodha ya watu millioni 20 ya NEC ilikuwa feki.
Akiohojiwa na waandishi wa habari siku ya uchaguzi Kikwete alisema 37% ya Watanzania ni under 18% ambayo ni almost 14.8 out of 40mil. approx.
sasa leo hii Tume kusema imeandikisha watu 20 mil out of 25 mill illegible voters, am ril dout of the figures.
 
Kulikuwa na jmla ya viyuo vya kupigia kura 50,000. Kisia wastani wa watu waliopiga kura katika kito kimoja halafu mara idadi ya vituo; utapata picha ya zoezi zima. Kama waliopigia kura wagombea wa urais ni 8,600,000- tafuta wastani waliopiga kura kwenye kituo kimoja. Sasa linganisha. This is simple arithmetic!!!! OK?????????????????????
 
nimejumlisha kwa kichwa tu hapa inanipa milioni 4.85.. tukiwafuta hao wote tunabakia bado na kama milioni 14.25 .. inabidi uongeze idadi wengine wa kuwafuta ni kiasi gani na kina nani?

Naongeza kwenye vijana nadhani vijana kama 3M majina yao kwenye mtandao wa NEC yalikuwepo ila kwenye makaratasi yaliobandikwa kwenye vituo majina yao yalikuwa hayapo. Cha ajabu wengi wa vijana hao ni wa majina ya Fred, Bernard , john na Paul na yanayofanana na hayo.
 
Mwanakijiji unakuja na mpya? Mimi nadhani idadi ya waliojiandikisha sio 20mil! Hii ni namba iliyotungwa! NEC haiaminiki kabisa! Hawa jamaa ni punda kabisa, wananiboa kweli! Dawa ni vyama vya upinzani vianze kuhakiki wapiga kura, waje na data zao. CHADEMA wamejiweka katika position nzuri ya kupambana! Nafurahi kuwa Dr Slaa anaweza kuendelea na Ukatibu Mkuu fulltime kwa sasa. I hope atakipanga chama vizuri. Pesa kutoka bungeni zitakipa Chama mfuko mkubwa zaidi kwa ajili ya kuleta maendeleo.
 
mwanakijiji hao millioni 8.6 ni wale tuliotangaziwa na tume. Na ukweili hautajulikana kwa maana tume inalindwa na katiba feki ya Tanzania kuwa hakuna atakayehoji kazi ya tume mahali popote.

Kituo changu walipjitokeza kuanzia saa 12 asubuhi ilikuwa ni idadi ya kutisha na haiwezi kuwa chini ya 80% ya matarajio. Kinachotokea hapa ile idadi ya 20 million iko juu zaidi ya watu waliojiandikisha, hii ina maana idadi ya wapiga kura halisi mwaka 2005 ni chini ya matokeo yaliyotangazwa. Hivyo sababu kubwa ya wapiga kura kupungua ni kushindikana kuingiza kura bandia vituoni na ndio sababu ya wabunge wa upinzani kushinda kwenye majimbo ya watu wenye pesa kama Ilemela, Nyamagana, Arusha Mjini, Iringa Mjini n.k
 
Kwanza kabisa kulingana wa Tanzania National Bureau of Statistics wame project kufikia mwaka 2010 kutakuwa na Watanzania 43,187,823.

National Bureau of Statistics

Kulingana na data hizo, ambao watakuwa hawajafikikisha miaka 18 siku ya kupiga kura 2010 wamekadiriwa kuwa ni 22,807,252. Watu wenye umri 80+ wako 287,758. Hivyo eligible and able voters ni 20,092,813. Haiwezekani kwamba NEC wameandikisha 100% ya watu wanaoweza kupiga kura. Ukichukulia 90% unapata 18,083,532. Ukiondoa wazee wengine wasiojiweza above 75 na vichaa au wenye mtindio wa ubongo tuweza ku conclude tuna maximum ya wapiga kura waliojiandikisha 18M Tanzania 2010, sio 19M na definately sio 20M.

Pili, Kwa mtazamo wangu kuna mambo mengi yaliyofanyika kuzuia wapiga kura "kujitokeza" uchaguzi huu:

1) Kwanza kuna uchakachuaji uliofanywa kwenye daftari la wapiga kura na NEC ama kwa NEC yenyewe kujua ama kutokujua (infiltration by Usalama). Watu zaidi ya 1.1M walihamishwa vituo vyao na hivyo kutoweza kupiga kura. Kwa mfano mtu umejiandikisha kituo Songea lakini huonekani huko bali unaonekana kituo Mafia. (Data hizi nimepewa na mtu anayelifanyia analysis daftari).

2) Kuna propaganda iliyofanywa kwa ufanisi sana na CCM nationwide ya kuwaogopesha watu kwamba kutakuwa na umwagaji damu siku ya kupiga kura. Aidha walitawanya habari tofauti na nyingi sana kwamba ukipiga kura upinzani "itayeyuka" one way or another na kuishia CCM au mawakala watanunuliwa kwa sh milioni moja etc. Stori za namna hii zilikuwa zimezagaa kila kona ya Tanzania (hata hapa JF) na hivyo kufanya watu kuogopa kwenda kupiga kura au kukata tamaa. Hapa wanawake walikuwa wengi nahisi idadi yao inaweza kuwa 2.5M.

3) Kuna uchakachuaji uliofanywa kitaalam wakati majumuisho au wakati wa kutangaza matokeo na Wasamamizi wa vituo (NEC/CID?). Waliweza kupunguza kura za wapinzani angalau 3,000 kila jimbo, hii inafanya idadi kuwa 600,000.

4) Kuna ambao walikuwa hawana kadi. Wale waliouza kadi zao, au kadi kukusanywa na mabalozi wa nyumba kumikumi au kubadilishana kadi na mtendaji kwa ajili ya vocha ya mbolea au simply kadi kupotea. Hawa ni kama 1M (BTW kuna watu walikamatwa wakinunua kadi au walikamatwa wamekusanywa kadi lakini pindi wanapofikishwa polisi wanatolewa mlango wa nyuma kabla hata maelezo hayajakamilishwa kutolewa. cases ziko nyingi tu). Kazi hii ya kukusanya kadi imefanyika kwa muda mrefu sasa zaidi ya miaka mitatu.

5) Kuna wale wanooishi mbali na vituo. Huko vijijini katika kila kituo kuna watu angalau 20 ambao wanaishi mbali sana na kituo, wengine hata umbali wa zaidi ya kilomita 15. Hivyo ukikadiria vituo 40,000 Tanzania bara, vijijini, unaongelea watu wapatao 800,000 walishindwa kupiga kura kutokana na umbali.

6) Kuna wale waliotaka kupiga kura lakini walirubuniwa. Wako waliohongwa wakati wa kampeni wasiende kupiga kura na kwa ujinga wao wakakubali. Wako walionyeshwa pombe wakashindwa kuamka siku ya uchaguzi. Wako waliorubuniwa barabarani wakienda kituoni. Au waliokuta vituo vimehamishwa bila wao kujua. Hawa nakadiria kuwa 500,000.

7) Wako walioshindwa kwenda kwa kuwa walikuwa safari au dharura ilitokea au ugonjwa. Hawa ni pamoja na wale wanafunzi waliojiandikisha shule nakujikuta shule bado zimefungwa wakati wa uchaguzi. Hawa wanaweza kuwa 500,000.

8) Wako wasio na elimu ya uraia. Kuna Watanzania wengi bado hawaoni umuhimu wa kupiga kura. Aidha hawaelewi, hawajali, ama ni wavivu kwenda kupanga mstari au mabishoo, au wanaona tu wanajidhalilisha au kujishusha hadhi kupanga mstari na watu wa kawaida. Hawa ni kama 2M.

Ukijumlisha jumla ya hivyo vipengele hapo juu 9M na kura zilizopigwa 8.6M unapata 17.6M. Tofauti ya Hii 17.6 na 18 (maximum) ni idadi ya majina yaliyojirudia kwenye daftari la wapiga kura pamoja na wale waliofariki lakini hawajaondolewa.

Sasa Tufanye nini?

Tujipange kuanzia sasa kwa chaguzi zijazo. Kuna mambo manne ya muhimu:

1) Daftari la wapiga kura lisiwe siri ya NEC. Wadau wote wa uchaguzi tudai daftari kabla ya chaguzi tuweze kulihakiki sisi wenyewe.

2) Tuhakikishe tuna mawakala waelewa kwenye vituo. Kutokuwa na uchaguzi uliokuwa wa haki kunamathiri kila Mtazania na sio to vyama vya siasa tu. Hakuna maana ya kuwa na uchaguzi wakati hatupati viongozi tunaowataka. Mwaka huu kulikuwa na vituo 55,000 (probably 65,000 by 2015), hili ni jukumu zito kwa chama chochote cha siasa hata CCM kupata mawakala waelewa. Tusiachie vyama vya siasa jukumu la kuhakikisha kwamba chaguzi zetu ni huru na haki. Serikali na NEC vimeshindwa kwa makusudi au kwa uzembe. Watanzania tuanzishe mikakati ya kuhakikisha kura unayoipiga inaenda kwa mgombea uliyemchagua. Tu campaign kuanzia sasa mpaka 2015 hili tatizo liundiwe mkakati liweze kutatuliwa localy.

3) TUsaidiane na vyama vya siasa, pamoja na NGOs husika kutoa elimu ya uraia. Tu mobilize wapiga kura waende kupiga kura siku ya uchaguzi kama wanavyofanya wenzetu majuu.

4) Tudai Tume huru na tuwe na sheria za uchaguzi zisizopendelea chama tawala. Bungeni lifanyike lakini sio hivyo tu bali tuwabane mabalozi/wahisani/wafadhili wailazimishe serikali yetu ibadili mfumo kama walivyoweza kutulazimisha kuingia kwenye siasa ya vyama vingi.
 
Mzee Mwanakijiji,

Hiyo namba ya 19M kwa vyovyote ina makosa. Siamini nusu ya Watanzania wana umri wa zaidi ya miaka 18.

Vilivyochangia:

1. Daftari halikufanyiwa uhakiki kuondoa wale waliofariki, waliohama, waliojiandikisha mara mbili nk.
2. Vijana wengi walijiandikisha ili wapate vitambulisho wakati hawakuwa na nia ya kupiga kura.
3. Vijana wenye umri chini ya miaka 18 walijiandikisha ili tu wapate vitambulisho kwa ajili ya kusajili simu zao.
4. Kwasababu ya kampeni ya nguvu wazee wengi waliogopa kwenda kupiga kura kwa kuhofia vurugu.
5. Wengi hawakuona umuhimu wa kupiga kura.
6. Migogoro ndani ya CCM wakati wa kura za maoni, ilifanya wananchama wao wengi kususia uchaguzi hasa maeneo ambayo hayakuwa na upinzani wa nguvu toka vyama vya upinzani.

Hata uchaguzi uliofanyika tarehe 14/11/2010 una turnout karibu na ile ya 31/10/2010 kwahiyo sidhani kama kuna kura zilifichwa.

Reports mbalimbali za maeneo hasa ya vijijini ambako watu wanajuana zinaonyesha wengi na hasa wazee na wanawake hawakujali kwenda kupiga kura.
 
Siamini kwamba watanzania wengi hivyo hawakupiga kura. Ila Nadhani kilichotokea ni kura za Slaa zilitolewa kwenye majumuisho. Yaani kampeni ilifanyika ya kupunguza kura za urais huku ukizingatia kuwa wabunge wetu wengi hawakuwa na uwezo wa kulipa wasimamizi nchi nzima na kadhalika hata wabunge wa chadema nao walikuwa busy na kura zao, hivyo kutoa mwanya wa CCM kuiba za uraisi.

Kama katiba yetu ingeruhusu mahakama kuchunguza kura za slaa nauhakiki NEC wangekuwa na hali tata ya kuhakikisha wanachokisema na kilichopo viko sawa na hapo ndipo CCM ingekufa.

PIa suala la kupigia kura sehemu uliojiandikishia nadhani kadhalika limechangia kuwa na idadi ndogo ya wagombea.

Sasa basi inabidi vijana tujipange na kuhakikisha kuwa 2015 CCM inaporomoka. Vijana tuliosoma kwenye kwenye vijiji vyetu tukapige kura na kugombea nafasi mbalimbali.
 
Daftari la wapiga kura haliwezi kuwa na makosa!

Idadi ya wapiga kura haihesabiwi kwa kukisiwa bali kwa kuhesabiwa. Ni sawasawa na mtu anayetaka kujua kwenye uwanja fulani wa mpira wameingia watu wangapi. Katika nchi zenye mfumo mzuri wa kuuza tiketi idadi ya watu haiwezi kukisikiwa; unaangalia tu mauzo ya tiketi, msafara wa timu, na watendaji mbalimbali wa uwanja na kupata almost an exact number ya watu waliomo uwanjani.

Kwenye daftari la kura, kuna watu walijiandikisha na hivyo kuweza kuwahesabu empirically na siyo kwa kukisikia. Na ukija kuondoa watu waliokufa au kujisajili mara mbili (NEC ilifanya hivyo na kufuta watu karibu milioni moja kutoka ile milioni 20) na kubakiwa na watu milioni 19. Hii siyo makisio ya Sensa bali idadi inayoweza kuonekana vitabuni kabisa. Kwa hiyo hoja kuwa idadi ya milioni 19 si ya kweli haina msingi kwani siyo hesabu ya kukisikiwa kama nilivyosema bali ilihesabiwa.

Inawezekana makisikio ya idadi yetu ya watu ya milioni 43 ni ya chini sana..
 
Walioandikishwa kupiga kura ni milioni 19

Waliopiga kura (turn out) ni milioni 8.6


Kikwete kapata kura milioni 5.2

Slaa kapata kura milioni 2.2


Katika chaguzi kuu kumi zilizopita hatujawahi kuwa na waliojitokeza kupiga kura chini ya asilimia 70, HAIJAWAHI KUTOKEA. Asilimia 70 ya milioni 19 ni watu milioni 13.3

Mwaka huu waliojitokeza (kuanzia saa kumi alfajiri sehemu nyingine) ni asilimia 42.84.


Ina maana karibu watu milioni 12, hawakupiga kura Jumapili ile kwa sababu mbalimbali. Naomba tutoe sababu ambazo zingeweza kuwafanya watu wasipige kura na makisio ya idadi ya watu waliokumbwa na sababu hizo kitaifa tuone kama tunaweza kufikia watu milioni 12.


Unafikiri wale wote waliopiga kura uchaguzi huu uliopita wakiitwa wajitokeze au kuhesabiwa idadi yao itakuwa karibu na 13.3 au na 8.6?

NB: Kuna idadi ya watu milioni 4 wamepungua kutoka kura za Kikwete 2005 na 2010; na kuna watu milioni 4.7 wanapungua kutoka makisio ya asilimia 70 ya waliojiandikisha kulinganisha na wale tulioripotiwa wamepiga kura. WHAT HAPPENED?
Tafadhali usithubutu kuniita Racist katika form yoyote ile. Uchaguzi wa mwaka huu umegubikwa na maswala mawili makuu, mosi ni udini pili ni Chama tawala kushika hatamu kama kawaida yake. Ukiangalia kwa undani utaona CUF na CCM ni wamoja kufuatana na kile kinachoaminika kuwa Kafiri sharti awe mkiani kumbuka CUF ilianzishwa na nani? na yuko wapi sasa na kwa sababu zipi?. Hii inaashiria kuwa Watanzania wazalendo wenye uchungu na nchi yao hawapewi fursa hiyo ya kuwatoa Watanzania kwenye dimbwi la umaskini kwa kuwa wao ni watu ambao wamekata tamaa na Akhera kama Waislaam wasemavyo. Iam sorry if Iam hurting someone for this. Ni muhimu Tanzania isiingize maendeleo ya nchi kwa kuangalia itikadi za dini. I believe kwamba kam CCM angekuwa ni Mkapa ndiyo anarun presidency mwaka huu, basi Lipumba asingeweza hata kumsupport na hata kumkabidhi ..... kama alivyompa Kikwete.. simply Mkapa ni mtu ambaye amekata tamaa na akhera kama mimi na any other christians... The same implies to any Muslim who ... had the same brain washed.... Chunguza sana upate suluhu ya hii kitu. Iam not accusing muslims or christians neither any other religion denomination but the truth is with the Almighty God kwamba Waislam wana jambo ....... If not today tomorrow will be. God bless Tanzania and her people.
 
Akili yangu inanielekeza kuwa kuna tatizo katika orodha daftalini na si vinginevyo. Hivyo ukweli ni kuwa hao waliopiga kura kipindi hiki pengine kwa uhalisia wake ni karibu 90% ya wanaostahili kupiga kura.
Tukiita watu (wenye sifa ambao wako Tz ) kupiga kura yeyote leo, namba itakaribia hiyo hiyo kama si kugota hapo hapo.

Yapigieni mstali haya mawazo yangu na mtakuja nambia siku moja.
 
Kibunago.. kutakuwa na tatizo gani kwenye daftari ambalo kina Makame hawakuliona hadi leo hii?
 
Na kubaliana na sababu zilizotolewa na wenzangu, pia naongezea sababu mbili zilizopunguza wapiga kura
1. Watu wengi waliofia fujo zitatokea, hivyo hawakwenda kupiga kura. Ikumbukwe kwa mara ya kwanza kwenye chaguzi zilizopita hakuna kiongozi wa JWTZ aliye wahi kujitokeza kutisha wananchi kuwa wanahisi kuna watu siku ya uchaguzi wange fanya fujo na kumwaga damu, kutokana hofu hiyo iliyotolewa na mwanajeshi huyo iliogopesha watu wengi hivyo kutojitokeza kupiga kura. Pia maroli mengi ya jeshi yalioneka yakipita mitaani hasa Dar. Harafu FFU walikuwa wametanda kila sehemu. Pia hiyo ilijenga hofu.
2. Factor nyingine, ni uchaguzi kufanyika Jumapili, kuna badhi ya raia hawapendi kuchanganya kuabudu Mungu na mambo ya kisiasa kwao priority ni kwenda kanisani, akisha enda kanisani harafu aje ajipage kupiga kura inakuwa si rahisi. Labda siku za usoni siku ya jumapili isiwe siku ya kupiga kura.
 
Daftari la wapiga kura haliwezi kuwa na makosa!

Idadi ya wapiga kura haihesabiwi kwa kukisiwa bali kwa kuhesabiwa. Ni sawasawa na mtu anayetaka kujua kwenye uwanja fulani wa mpira wameingia watu wangapi. Katika nchi zenye mfumo mzuri wa kuuza tiketi idadi ya watu haiwezi kukisikiwa; unaangalia tu mauzo ya tiketi, msafara wa timu, na watendaji mbalimbali wa uwanja na kupata almost an exact number ya watu waliomo uwanjani.

Kwenye daftari la kura, kuna watu walijiandikisha na hivyo kuweza kuwahesabu empirically na siyo kwa kukisikia. Na ukija kuondoa watu waliokufa au kujisajili mara mbili (NEC ilifanya hivyo na kufuta watu karibu milioni moja kutoka ile milioni 20) na kubakiwa na watu milioni 19. Hii siyo makisio ya Sensa bali idadi inayoweza kuonekana vitabuni kabisa. Kwa hiyo hoja kuwa idadi ya milioni 19 si ya kweli haina msingi kwani siyo hesabu ya kukisikiwa kama nilivyosema bali ilihesabiwa.

Inawezekana makisikio ya idadi yetu ya watu ya milioni 43 ni ya chini sana..


Daftari la wapiga kura lina makosa lukuki. Mimi nimeliona na kulipitia hilo daftari. Ukichukua kituo chochote randomly kwenye daftari (na sio orodha iliyobandikwa kwenye vituo) utakuta kuna watu kama watano mpaka kumi wanaojirudia mara mbili mbili. Halafu kumbuka kuna vituo 55,000. Mkuu wa idara ya IT ya Tume ya Uchaguzi Dr Sisti pamoja na Kiravu wamekiri wenyewe kwamba makosa yapo na bado hawajajua ni mengi kiasi gani. Na hiyo ndiyo sababu waliotoa kwa kuchelewesha kulitoa dafatari mpaka siku tatu kabla ya uchaguzi. Kwani Tume mpaka tarehe 28 Oktoba walikuwa bado wanalifanyia marekebisho daftari kuondoa watu waliojirudia mara mbili mbili na makosa mengine kibao. Walibainisha kwamba ugumu ulikuwepo kwa kuwa walikuwa wanatumia software ya face recognition kuweza kujua kama watu wamejirudia ili waweze kuwaondoa. Walisema wamelazimika kutumia hiyo software kwa kuwa watu waliojiandikisha mara ya mbili mara nyingi wanatumia majina tofauti au wanachanganya majina hivyo kuwa vigumu kuwajua na kuwaondoa. Lakini walikiri kwamba software waliyokuwa wanatumia was a bad choice ilikuwa weak isiyoweza kumudu hiyo kazi na kwamba watatafuta njia mbadala huko mbeleni.

Ukiwwauliza Tume leo wakupe idadi kamili ya wapiga kura hawataweza kukupa, watakupa makisio tu. Ndio maana pale mwanzo walisema kuna wapiga kura milioni 19 na baadae wakati wanatangaza matokeo wakabadilisha wakasema 20. NEC hawana uelewa wala capacity ya kuweza kuwa na daftari lenye hadhi ya kuitwa daftari la wapiga kura. Hili daftari lao ni uchafu mtupu.
 
nimejumlisha kwa kichwa tu hapa inanipa milioni 4.85.. Tukiwafuta hao wote tunabakia bado na kama milioni 14.25 .. Inabidi uongeze idadi wengine wa kuwafuta ni kiasi gani na kina nani?


mm, watu wanaijadili hii hoja juujuu tu, lakini ukweli ni kwamba, idadi kamili ya waliojiandikisha anaijuwa jaji makame na kiravu tu, hiyo idadi walioitangaza hata profesa baregu aliipinga kabla ya uchaguzi, ilikuwa ni idadi hewa, ccm walitegemea wangechakachuwa vya kutoka, lakini hesabu zao zimekataa. Target ya ccm ilikuwa ni kuchakachuwa kura ili ccm ijipe ushindi wa 80% lakini imeshindikana. Ndio maana jk hana furaha kabisa kupewa 61% ya ushindi, ni fedhea kwake na chama chake.
Hitimisho: Idadi kamili ya waliyojiandikisha haijurikani. Hizo ndio faida za udanganyifu.
 
mnaweka assumption kuwa idadi waliyotoa NEC ni sahihi! hiyo ni assumption kubwa sana! NEC hawana credibility hata kidogo!!
 
mkubali msikubali. sababu kubwa ni kitendo kilichofanywa na yule mnadhimu mkuu wa jeshi kuongelea habari ya usalama kwenye vyombo vya habari akisisstiza kwamba jeshi halitakubali uvunjifu wa amani. tafasiri ilikuwa ni kuwatisha wananchi. na wananchi waliielewa hiyo message yenyewe. nakumbuka nilituma message yangu kwenye kipindi cha habari TBC hawakuisoma. lakini huo ndo ukweli. sijawahi kuona kwenye historia ya nchi hii wakuu au maofisa waandamizi wa jeshi wakiongelea hali ya usalama ya nchi wakati waziri yupo na police wapo
 
hao waliingia mtini pengine kwa sababu zifuatazo;

  • vitisho vya vyombo vya dola na hasa mnadhimu mkuu wa jwtz
  • watu kukosa hamasa (indifference) kwa sababu ya uwezekano wa uchakachuaji kutokea ingawa mkuu ulitetea lisingetokea.
 
Pamoja na kwamba hili haliangaliwi sana na wengi, lakini kupiga kura Jumapili kunawanyima wakristo wengi kupiga kura. Ibada nyingi huendelea hadi saa 8 na watu wengi makanisa yao yako mbali na maeneo yao ya kupigia kura.
 
Ni vigumu kidogo kujua ukweli halisi wa nini Kimetokea kiasi hicho. Kwa kifupi Mheshimiwa Benson Bana alipendekeza utafiti ufanyike kujua ni kwa nini idadi ilikuwa ya kiasi hicho.
Kwa mtazamo wanyo mimi kama idadi ya nec ni sahihi basi naweza sema hao wote milioni kumi na ushee hawakwenda kabisa kupiga kura kwa sababu tofauti tofauti. Kwa mfano, mimi mwenyewe nilitoka Kimara Mwisho saa mbili asubuhi kwenda kupiga Kura maeneo ya Ilala Kasulu B. Nilifika kituoni pale saa tatu hivi kwani kulikuwa hakuna foreni kwa siku ile. Cha kushangaza nipanga foreni nikiwa kam mtu wa 8 nyuma ya wa mtu wa kwanza aliyetutangulia sote. Inamaanisha kwamba rate ya watu pale ilikuwa kidogo sana.
Pia nilitapa muda na kuongea na jamaa mmoja ambaye alisimamia kituo furani na kuniambia kuwa, kituoni kwake idadi ya watu waliojiandikisha walikuwa 476 lakini mpaka 11 jioni ni watu 152 tu waliojitokeza na wengi wao walikuwa ni Vijana, hiyo ni hapa Dar.
Nafikiri Kina Rajab na Bosi wake Makame wapitie upya takwimu zao na ukweli ujulikane.
 
Back
Top Bottom