Walisema DP World itashusha gharama na siku za mizigo kukaa Bandarini. Leo gharama za kuingiza mzigo zitapanda kwa 360%

Walisema DP World itashusha gharama na siku za mizigo kukaa Bandarini. Leo gharama za kuingiza mzigo zitapanda kwa 360%

the power

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
407
Reaction score
799
Hakika sikio la kufa halisikii dawa. Wabunge wakishirikiana na mawaziri, machawa na wapambe e.g. baadhi ya waandishi walituaminisha pitisha hiyo sheria ya kubinafsisha bandari zetu kwa DP world.

Tuliaminishwa, ulimwengu unaenda kasi lazima tuende na wakati, tuende na utandawazi, pitisha hiyo sheria ya kubinafsisha bandari zote baharini na nchi kavu na misitu yetu mikubwa kwa DP world, mwanzo ilikuwa kwa miaka 100, baada ya kilio ikashushwa kwa miaka kama 30, miaka ambayo karibu viongozi na wabunge wote waliopitisha hii sheria watakuwa wamekwisha kufia mbali na kuwaachia vizazi vyetu umasikini wa kutupwa chini ya utumwa mamboleo kwenye rasilimali zao.

"Sikieni nyie watanzania msiotaka maendeleo, hawa DP world wanauzoefu wa kuendesha mabandari makubwa kimataifa; India na Marekani (just to mention a few). Hawa jamaa sio tu tukiwapatia bandari watapunguza siku za mzigo kukaa bandarini mwezi mzima bali itakuwa wiki moja au mbili na ghalama za kuingiza mzigo zitashushwa zaidi ya nusu ya gharama za sasa"

"Watakuja na vifaa state of arts, watacomputerize process nzima za kutoa mzigo kuongeza quality na tija. Nchi itapata mapato matrililioni (ile figure siwezi kuiweka hapa kwani ni kituko) , mapato ya mwaka yatakuwa zaidi ya jumla ya mapato ya miaka kumi iliyopita" NDIVYO WATANZANIA TULIVYOHAMINISHWA NA WAWAKILISHI WETU BUNGENI, wakipewa support na machawa na wapambe waandishi waliolipwa rushwa ya kupelekwa DubaI few days kwenye five stars Hotel na kulipwa mamilioni na magari ya kifahari juu. Hivi wanajisikiaje sasa wakiona wotetunasuffer; Ila wabongo bwana hatuna aibu, tunajua kumute, macho makavuuuu, ndindindi! as if nothing happened.

Sasa tunaambiwa tukae mkao wa kula, kwa kupanda kwa gharama ya kwa asilimia 360% kuingiza na kutoa mzigo bandarini; haijawahi kutokea tangia bandari zetu zianze kufanya kazi, tutegemee mfumuko wa bei ya vifaa vyote tunavyotumia (vipuli na vifaa vya magari, magari yenyewe, ujenzi, kilimo, umwagiliaji, mafuta n.k) kwani hata hivyo vinavyotengenezwa nchini mali ghafi inatoka nje, tutegemee mfumuko wa bei ya vyakula na mafuta, tutegemee ghalama zote za maisha kupanda. Kibaya zaidi serikali itakosa mapato makubwa, sitakiwi kuweka takwimu hapa na contribution ya bandari zetu kwenye budget nzima ya nchi; Kwishnei! Nakwambia kama wangekuwa na tija tayari leo tungeambiwa mapato yalivyoongezeka, huduma ilivyoboreshwa, Jiulize kwa nini kimya kikali sana.?

Tunaambiwa copper ya Congo iliyokuwa ikipitishwa hapa kwetu, sasa inapitia bandari ya Mombasa, Wafanyabiashara wa nchi zote jirani na wa ndani wamehama/watahamia bandari ya Mombasa. Hivi jiulize yale malori lukuki ya Mizigo kutoka na kwenda Uganda, Burundi, Kongo, Malawi, Rwanda , Zambia, Malori uliyokuwa ukipishana nayo wakati wote yameunga tela kutokea Dodoma mpaka Dar es salaam to and fro yamepotelea wapi?. what is the implication of that? Ni kiasi gani cha mabillioni walikuwa wakilipa kwa mwezi na sasa yanapotea. Hakika huhitaji akili ya PhD ya uchumi kujua kitakachotokea kesho kwenye maisha ya watu wa kawaida.

Rushwa ni mbaya sana, kwani mpokea rushwa hajali madhara yatakayotokea kwa wenzake na kizazi kijacho, yeye anaangalia masilahi yake na familia yake kwa wakati huo, ndio umesikia. Ni kweli hakuna ubishi kuna watu wamekuwa mabilionea kupitia ishu hii ya DP world. Ila wapambe koko, wengine utawasikia hata humu jamii forum kupitia comments zao huku hata wao ni njaa kali na shida kwelikweli ila bado wanatetea dhuluma hii ya rasilimali yetu, wanatetea ubakaji na utekaji wa mali ya umma tuliyokuwa tunamiliki tangia uhuru na kujipangia kulingana na kipato chetu

Na hii unaambiwa ni bado, hizi ni mvua za rasharasha, cha mtoto (this is just a pre-amble) labda tuvunje mkataba, mkataba ambao hatuwezi hata thubutu.

Nafikiri bado hatujasahahu vifungu toa damu, vifungu kata roho walivyotuwekea ili tusithubutu hata kufikiria kuvunja huu mkataba, achana na independent tribunal ya nje itakayotakiwa kibaya eti lazima wao kwanza wakubali na kulidhia ndipo waturuhusu kuvunja mkataba. Ebu msomaji fikiria eti ili uvunje mkataba unaambiwa itabidi huyo anayefaidi akubali kwanza. Hivi wasomi wetu, wanasheria, viongozi wetu kuna wakati mnakuwa na mapepo wakati mnasign mikataba hii, au akili zenu zinakuwa zimehamishwa seheme nyingine na kubaki vichwa tupu, eti inabidi adui, dhulumati , anayefaidi alidhie kwanza ndipo kukuruhusu uanze mchakato wa kuchukua kile anachofaidi,ili umnyang'anye tonge nono mdomoni. Hivi kwa akili ya kawaida inawezekana kweli. Hata Malaika hawezi kufanya upuuzi huo.

Ngoja sasa msumari wa moto uingie vizuri, sisi wabongo tunajifanyaga wajuaji sana, hatujifunzi hata kwa wenzetu Malysia waliovunja mkataba na hawa DP-world, kizuri wao hawakuwa na masharti magumu sisi vipofu tukajifanya wajanja kama kawaida yetuna kukubali masharti kata roho, masharti vujisha damu. Sasa tusubili kuendelea kubleed till we are dried -up. Na hili liwe somo kwa watunga sheria wetu, sio kila ukipewa kadola, ukipelekwa Dubai for 5 days night in 5 starts hotel unasahau ndugu zako, wazazi wako, wajukuu zako, kizazi chako, mbaya zaidi hata wale waliokuweka hapo.
 
Tutatumia tu bandari ya mombasa kama majirani zetu.
 
Nipo siti ya mbele wangine wanasema sababu ya gharama ya kuingiza mzigo kupanda ni kutokana na maharamia waliopo baharini huko
 
Safi sana , ni hbri njema hii.Gharama zipande za kutoa mizigo zipande , bidhaa madukani zipande, wananchi washike adabu ili ikifika 2025 wawe na akili za kulitoa madarakani hili dubwana liitwalo CCM
Ccm ni wahuni kabisa!
 
Hakika sikio la kufa halisikii dawa. Wabunge wakishirikiana na mawaziri, machawa na wapambe e.g baadhi ya waandishi walituaminisha pitisha hiyo sheria ya kubinafsisha badandri zetu kwa DP world.

Tuliaminishwa, ulimwengu unaenda kasi lazima tuende na wakati, tuende na utandawazi, pitisha hiyo sheria ya kubinafsisha bandari zote baharini na nchi kavu na misitu yetu mikubwa kwa DP world, mwanzo ilikuwa kwa miaka 100, baada ya kilio ikashushwa kwa miaka kama 30, miaka ambayo karibu viongozi na wabunge wote waliopitisha hii sheria watakuwa wamekwisha kufia mbali na kuwaachia vizazi vyetu umasikini wa kutupwa chini ya utumwa mamboleo kwenye rasilimali zao.

"Sikieni nyie watanzania msiotaka maendeleo, hawa DP world wanauzoefu wa kuendesha mabandari makubwa kimataifa; India na Marekani (just to mention a few). Hawa jamaa sio tu tukiwapatia bandari watapunguza siku za mzigo kukaa bandarini mwezi mzima bali itakuwa wiki moja au mbili na ghalama za kuingiza mzigo zitashushwa zaidi ya nusu ya gharama za sasa"

"Watakuja na vifaa state of arts, watacomputerize process nzima za kutoa mzigo kuongeza quality na tija. Nchi itapata mapato matrililioni (ile figure siwezi kuiweka hapa kwani ni kituko) , mapato ya mwaka yatakuwa zaidi ya jumla ya mapato ya miaka kumi iliyopita" NDIVYO WATANZANIA TULIVYOHAMINISHWA NA WAWAKILISHI WETU BUNGENI, wakipewa support na machawa na wapambe waandishi waliolipwa rushwa ya kupelekwa DubaI few days kwenye five stars Hotel na kulipwa mamilioni na magari ya kifahari juu. Hivi wanajisikiaje sasa wakiona wotetunasuffer; Ila wabongo bwana hatuna aibu, tunajua kumute, macho makavuuuu, ndindindi! as if nothing happened.

Sasa tunambiwa tukae mkao wa kula, kwa kupanda kwa gharama ya 360% kuingiza na kutoa mzigo bandarini; haijawahi kutokea tangia bandari zetu zianze kufanya kazi, tutegemee mfumuko wa bei ya vifaa vyote tunavyotumia (vipuli na vifaa vya magari, magari yenyewe, ujenzi, kilimo, umwagiliaji, mafuta n.k) kwani hata hivyo vinavyotengenezwa nchini mali ghafi inatoka nje, tutegemee mfumuko wa bei ya vyakula na mafuta, tutegemee ghalama zote za maisha kupanda. Kibaya zaidi serikali itakosa mapato makubwa, sitakiwi kuweka takwimu hapa na contribution ya bandari zetu kwenye budget nzima ya nchi; Kwishnei! Nakwambia kama wangekuwa na tija tayari leo tungeambiwa mapato yalivyoongezeka, huduma ilivyoboreshwa, Jiulize kwa nini kimya kikali sana.?

Tunaambiwa copper ya Congo iliyokuwa ikipitishwa hapa kwetu, sasa inapitia bandari ya Mombasa, Wafanyabiashara wa nchi zote jirani na wa ndani wamehama/watahamia bandari ya Mombasa. Hivi jiulize yale malori lukuki ya Mizigo kutokana kwenda Uganda, Burundi, Kongo, Malawi, Rwanda , Zambia, Malori uliyokuwa ukipishana nayo wakati wote yameunga tela kutokea Dodoma mpaka Dar es salaam to and fro yamepotelea wapi?. what is the implication of that? Ni kiasi gani cha mabillioni walikuwa wakilipa kwa mwezi na sasa yanapotea. huhitaji akili ya PhD ya uchumi kujua kitakachotokea kesho kwenye maisha ya watu wa kawaida.

Rushwa ni mbaya sana, kwani mpokea rushwa hajali madhara yatakayotokea kwa wenzake na kizazi kijacho, yeye anaangalia masilahi yake na familia yake kwa wakati huo, ndio umesikia. Ni kweli hakuna ubishi kuna watu wamekuwa mabilionea kupitia ishu hii ya DP world. Ila wapambe koko, wengine utawasikia hata humu jamii forum kupitia comments zao huku hata wao ni njaa kali na shida kwelikweli ila bado wanatetea dhuluma hii ya rasilimali yetu, wanatetea ubakaji na utekaji wa mali ya umma tuliyokuwa tunamiliki tangia uhuru na kujipangia kulingana na kipato chetu

Na hii unaambiwa ni bado, hizi ni mvua za rasharasha, cha mtoto (this is just a pre-amble) labda tuvunje mkataba, mkataba ambao hatuwezi hata thubutu.

Nafikiri bado hatujasahahu vifungu toa damu, vifungu kata roho walivyotuwekea ili tusithubutu hata kufikilia kuvunja huu mkataba, achana na independent tribunal ya nje pamoja na wao kulidhia na kuturuhusu kuvunja. Ebu msomaji fikilia eti ili uvunje mkataba unaambiwa itabidi huyo anayefaidi alidhie kwanza. Hivi wasomi wetu, wanasheria, viongozi wetu kuna wakati mnakuwa na mapepo wakati mnasign mikataba hii, au akili zenu zinakuwa zimehamishwa sehemeu nyingine na kubaki vichwa tupu, eti inabidi adui, mdhulumati , anayefaidi alidhie kwanza ndipo kukuruhusu uanze mchakato wa kuchukua kile anachofadi. Hata Malaika hawezi kufanya hivyo

Ngoja sasa msumari uingie vizuri, sisi wabongo hatujifunzi hata kwa wenzetu Malysia waliovunja mkataba na hawa DP-world, kizuri wao hawakuwa na masharti magumu sisi vipofu tukajifanya wajanja kama kawaida yetuna kukubali masharti kata roho, masharti vujisha damu. Sasa tusubili kuendelea kubleed till we are dried -up. Na hili liwe somo kwa watunga sheria wetu, sio kila ukipewa kadola unasahau ndugu zako, wazazi wako, wajukuu zako, kizazi chako, hata wale waliokuweka hapo.

Toka lini wapiga deals wakasema ukweli? Kwasababu ni wakubwa wanataka tukubali tu. Ila tunalipia gharama za matendo yao.
Faraja yetu haiko kwao, sababu ni waongo na wabinafsi. Mwenyezi Mungui mwema anatuonea huruma na ndiye atakayetunusuru
 
Kwa kweli huyu bibi yenu ametuharibia kabisa Nchi yetu.97%ya mzigo wote wa congo drc unapitia bandari ya mombasa.na hii imeanza baada ya bandari ya Dar es salaam kuuziwa dp world na kupelekea kukosa mapato.kingine Kwa Sasa meli zinakaa muda mrefu sana tofauti na tulivyokuwa tunaaminishwa na Hawa wahuni waliojipachika cheo Cha ubunge kuwa mapato yataongezeka wakati ukweli yameshuka sana.Kuchelewa Kwa upakuaji mizigo imepelekea wakongo kuihama bandari yetu na kuhamia mombasa.huyu mama ni hatari Kwa ustawi wa jamii.
 
Ushahidi upo wapi?
Soma vizuri andiko kuna baadhi ya viashiria vimetajwa na mwandishi, huhitaji ushahidi wa kimaandishi. Ila umeambiwa subiri mpaka mwezi wa 12 ndipo urudi na kuuliza ushahidi. Wabongo wengine bwana. Soma mchania mada Sapire juu hapo na yeye ametoa ushahidi. Hivi watanzania mpaka mtu akukate shingo ndio ujue upanga ni mkali
 
Haoa tutegemee nguvu za wanajeshi tu JWT kutunusuru kama walivyofanya huko Afrika ya kati,Mana hawa viongozi wetu hawana Aibu kabsa.
 
Tutatumia tu bandari ya mombasa kama majirani zetu.
Huu mjadala ningeweza kuandika kwa kirefu tatizo liko wapi, Hii sio DP wala bandari ya Mombasa shida ni ya kidunia na wakubwa ndio wameamua hivyo. Niandike kwa kifupi sana nini kimetokea. Red sea jamaa wanashambulia meli sasa gharama zimekuwa kubwa sana kwa insurance na wakichukua njia mbadala lakini hii inaleta shida zaidi kwa nchi za ulaya na US kuliko China na zingine Asia na pia Africa.

Shipping agent wakaona kuongeza gharama kwa meli zinazoenda Ulaya tu na US itawapa advantage nchi zingine na hasa China wakaamua bei zote shipping ziwe sawa ila kutompa mtu mmoja advantage kibishara sasa hizi gharama dunia nzima zimepanda kwa maana hiyo nenda port yoyote story ni the same. Ni story ndefu kinachofanyika na wakubwa huko juu kuleta hili balaa.
 
Safi sana , ni hbri njema hii.Gharama zipande za kutoa mizigo zipande , bidhaa madukani zipande, wananchi washike adabu ili ikifika 2025 wawe na akili za kulitoa madarakani hili dubwana liitwalo CCM
Msoma matokeo 2025.

Idadi ya wapiga kura M35.
Waliopo mjini M15.
Waliopo vijijini, umasaini, porini kusipo na internet wala duka la kijiji wala bandari 20M.
 
Kwa kweli huyu bibi yenu ametuharibia kabisa Nchi yetu.97%ya mzigo wote wa congo drc unapitia bandari ya mombasa.na hii imeanza baada ya bandari ya Dar es salaam kuuziwa dp world na kupelekea kukosa mapato.kingine Kwa Sasa meli zinakaa muda mrefu sana tofauti na tulivyokuwa tunaaminishwa na Hawa wahuni waliojipachika cheo Cha ubunge kuwa mapato yataongezeka wakati ukweli yameshuka sana.Kuchelewa Kwa upakuaji mizigo imepelekea wakongo kuihama bandari yetu na kuhamia mombasa.huyu mama ni hatari Kwa ustawi wa jamii.
Atakuwa amewekwa kwa kazi maalum huyu sio bure...Haiwezekani raisi mambo ya msingi haangaiki nayo anaangaika na ishu za kuzindua albam ya KondeBoy.
 
Back
Top Bottom