KERO Walisema watatupa ufadhili kusoma Chuo Kikuu cha SUMAIT (Zanzibar) hadi tuhitimu, ufadhili umesitishwa kinyume na makubaliano

KERO Walisema watatupa ufadhili kusoma Chuo Kikuu cha SUMAIT (Zanzibar) hadi tuhitimu, ufadhili umesitishwa kinyume na makubaliano

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Torra Siabba

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
243
Reaction score
287
Mimi ni Mwanafunzi wa degree, nipo Mwaka wa Pili katika chuo Cha Abdurahman Al-Sumait kilichoko Zanzibar.

Mimi na wenzangu tulipata ufadhili wa masomo (Scholarship) kutoka Taasisi ya Direct Aid Society ambayo zamani ilijulikana kama African Muslim Agency (AMA) ambayo ndio wamiliki wa Chuo cha Sumait pamoja na MUM cha Morogoro.

Tuliahidiwa kufadhiliwa ndani ya kipindi chote cha masomo yetu yaani miaka mitatu ya degree, huku tukilipiwa kila kitu ikiwemo full tuition fee, accommodations, stationary na transport hadi mwisho wa mwaka.
Screenshot 2024-11-21 152935.png

Screenshot 2024-11-21 153011.jpg
Ajabu baadhi ya watu tumepigwa simu kutoka chuoni kwamba hatuna ufadhili tena kwa hiyo tuanze kujilipia la sivo tuache chuo bila ya kuzingatia kwamba hatuna makubaliano ya kimkataba ya kumuondoa mtu yeyote kwenye ufadhili huo.

Serikali yetu zitusaidie maana sasa hivi hatujui hatma yetu ya kimasomo ikoje na chuo kimefunguliwa tangu 28/10/2024.

Wengi wetu ni maskini na yatima ndio kilikuwa kigezo cha kupata ufadhili. Maana tungepewa maelekezo ya kimkataba awali tungeamua tukubali au tukatae ufadhili wao. Sasa wanatuacha sasa hivi hatuna pa kukimbilia na huu ndo mwaka wetu wa mwisho masomo.

Rais wa Wanafunzi wa SUMAIT, Salim Abass amesema:
JamiiForums
imewasiliana na Kiongozi huyo wa Wanafunzi, anaelezea: Mimi pia ni mmoja wa wanufaika wa ufadhili huo, kilichotokea ni kuwa kila baada ya semester kulikuwa kuna vikao vinafanyika vya maboresho na mazungumzo ya mikataba ya ufadhili.

Baadhi ya Wanafunzi walikuwa hawashiriki, hivyo inawezekana kuna baadhi ya mambo yamewapita, kwa kuwa baada ya mazungumzo kila mtu alikuwa anasaini mkataba wake pekee, huwezi jua mwenzako amesaini mkataba wa aina gani.

Moja ya maelekezo ya mkataba ni kuwa Mwanafunzi alitakiwa kuwa na wastani wa ufaulu wa GPA ya 3.0, ambaye hafikishi inamaanisha anatolewa katika ufadhili.

Fedha wanazotupa ni nyingi na inawezekana zinaweza kuwachanganya wanufaika wakajisahau kufuatilia mambo kama hayo ya maboresho ya mikataba.
 
Duh Kama ni baadhi tu labda wamefabya uchunguzi wakagundua kuna waliofanya udanganyifu,au mfadhili ameyumba kiuchumi
 
accommodations, stationary na transport hadi mwisho wa mwaka.

Ajabu baadhi ya watu tumepigwa simu kutoka chuoni kwamba hatuna ufadhili tena kwa hiyo tuanze kujilipia la sivo tuache chuo bila ya kuzingatia kwamba hatuna makubaliano ya kimkataba ya kumuondoa mtu yeyote kwenye ufadhili huo.

Serikali yetu zitusaidie maana sasa hivi hatujui hatma yetu ya kimasomo ikoje na chuo kimefunguliwa tangu 28/10/2024.

Wengi wetu ni maskini na yatima ndio kilikuwa kigezo cha kupata ufadhili. Maana tungepewa maelekezo ya kimkataba awali tungeamua tukubali au tukatae ufadhili wao. Sasa wanatuacha sasa hivi hatuna pa kukimbilia na huu ndo mwaka wetu wa mwisho masomo.
Stationery
 
Ufaulu wenu ukoje mpaka sasa?
Hakuna aliyesapu?
Kuna fadhili zingine zinaweka viwango, usipofikia, ufadhili unafutwa!
 
Mimi ni Mwanafunzi wa degree, nipo Mwaka wa Pili katika chuo Cha Abdurahman Al-Sumait kilichoko Zanzibar nasoma course ya IT.

Mimi na wenzangu tulipata ufadhili wa masomo (Scholarship) kutoka Taasisi ya Direct Aid Society ambayo zamani ilijulikana kama African Muslim Agency (AMA) ambayo ndio wamiliki wa Chuo cha Summait pamoja na MUM cha Morogoro.

Tuliahidiwa kufadhiliwa ndani ya kipindi chote cha masomo yetu yaani miaka mitatu ya degree, huku tukilipiwa kila kitu ikiwemo full tuition fee, accommodations, stationary na transport hadi mwisho wa mwaka.

Ajabu baadhi ya watu tumepigwa simu kutoka chuoni kwamba hatuna ufadhili tena kwa hiyo tuanze kujilipia la sivo tuache chuo bila ya kuzingatia kwamba hatuna makubaliano ya kimkataba ya kumuondoa mtu yeyote kwenye ufadhili huo.

Serikali yetu zitusaidie maana sasa hivi hatujui hatma yetu ya kimasomo ikoje na chuo kimefunguliwa tangu 28/10/2024.

Wengi wetu ni maskini na yatima ndio kilikuwa kigezo cha kupata ufadhili. Maana tungepewa maelekezo ya kimkataba awali tungeamua tukubali au tukatae ufadhili wao. Sasa wanatuacha sasa hivi hatuna pa kukimbilia na huu ndo mwaka wetu wa mwisho masomo.
Huo ufadhili ulipewa kimaandishi au waliongea tu kwa mdomo? Kama hakuna maandishi, unataka kulazimisha nn sasa?
 
Mimi ni Mwanafunzi wa degree, nipo Mwaka wa Pili katika chuo Cha Abdurahman Al-Sumait kilichoko Zanzibar nasoma course ya IT.

Mimi na wenzangu tulipata ufadhili wa masomo (Scholarship) kutoka Taasisi ya Direct Aid Society ambayo zamani ilijulikana kama African Muslim Agency (AMA) ambayo ndio wamiliki wa Chuo cha Summait pamoja na MUM cha Morogoro.

Tuliahidiwa kufadhiliwa ndani ya kipindi chote cha masomo yetu yaani miaka mitatu ya degree, huku tukilipiwa kila kitu ikiwemo full tuition fee, accommodations, stationary na transport hadi mwisho wa mwaka.

Ajabu baadhi ya watu tumepigwa simu kutoka chuoni kwamba hatuna ufadhili tena kwa hiyo tuanze kujilipia la sivo tuache chuo bila ya kuzingatia kwamba hatuna makubaliano ya kimkataba ya kumuondoa mtu yeyote kwenye ufadhili huo.

Serikali yetu zitusaidie maana sasa hivi hatujui hatma yetu ya kimasomo ikoje na chuo kimefunguliwa tangu 28/10/2024.

Wengi wetu ni maskini na yatima ndio kilikuwa kigezo cha kupata ufadhili. Maana tungepewa maelekezo ya kimkataba awali tungeamua tukubali au tukatae ufadhili wao. Sasa wanatuacha sasa hivi hatuna pa kukimbilia na huu ndo mwaka wetu wa mwisho masomo.

Poleni sana.

Mara nyingi ufadhili (scholarship) inakuwa na masharti ambayo yapo kimaandishi. Mojawapo ya masharti hayo ni namna gani ufadhili utasitishwa kwa sababu zipi pamoja na kuonesha nini kinacholipiwa kupitia ufadhili wenyewe. Kwa hiyo tangu mwanzo ulitakiwa kujua masharti yote, haki na wajibu wako kama mfadhiliwa (sponsee) kwenye huo ufadhili (scholarship). Na mwisho kusaini huo mkataba.

Licha ya kutosaini mkataba wowote nafikiri bado mna haki ya kuelezwa kwa nini ufadhili umesitishwa kwenu.

Pia huwa kuna uongozi wa wanafunzi chuoni au hata viongozi wa wale mliokuwa mnapokea huo ufadhili sijui kama mmeanza nao ili kuona wao kama viongozi wenu watawasaidiaje kwa hiyo changamoto. Pia nafikiri kuna vyama vya wanfunzi vyuoni/Tanzania vinavyojihusisha na kutetea haki za wanafunzi. Lazima viongozi wenu wawasaidie na kuwashauri nini cha kufanya kama wao wakishindwa.

Mengine nafikiri wataalamu wetu wa sheria ndiyo watatusaidia hasa namna ya kupata haki zenu.
Kila la kheri.
 
Poleni sana.

Mara nyingi ufadhili (scholarship) inakuwa na masharti ambayo yapo kimaandishi. Mojawapo ya masharti hayo ni namna gani ufadhili utasitishwa kwa sababu zipi pamoja na kuonesha nini kinacholipiwa kupitia ufadhili wenyewe. Kwa hiyo tangu mwanzo ulitakiwa kujua masharti yote, haki na wajibu wako kama mfadhiliwa (sponsee) kwenye huo ufadhili (scholarship). Na mwisho kusaini huo mkataba.

Licha ya kutosaini mkataba wowote nafikiri bado mna haki ya kuelezwa kwa nini ufadhili umesitishwa kwenu.

Pia huwa kuna uongozi wa wanafunzi chuoni au hata viongozi wa wale mliokuwa mnapokea huo ufadhili sijui kama mmeanza nao ili kuona wao kama viongozi wenu watawasaidiaje kwa hiyo changamoto. Pia nafikiri kuna vyama vya wanfunzi vyuoni/Tanzania vinavyojihusisha na kutetea haki za wanafunzi. Lazima viongozi wenu wawasaidie na kuwashauri nini cha kufanya kama wao wakishindwa.

Mengine nafikiri wataalamu wetu wa sheria ndiyo watatusaidia hasa namna ya kupata haki zenu.
Kila la kheri.
Sure
 
Back
Top Bottom