Walitufanyia utumwa baadaye wakatufanyia ukoloni na sasa wanatuwekeza! Malengo yao ni yale yale, tuwe makini

Walitufanyia utumwa baadaye wakatufanyia ukoloni na sasa wanatuwekeza! Malengo yao ni yale yale, tuwe makini

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Bara la Afrika ndiyo bara tajiri sana kuliko mabara yote duniani, kuanzia kwenye rasilimali watu (human resources) hadi kwenye rasilimali asili (natural resources).

Ni bara kubwa lenye majitu yenye nguvu yanayo stahimili dhoruba mbali mbali kuliko watu wengine duniani. Ndiyo maana utaona mabingwa wa dondi duniani ni watu toka bara hili, wachezaji wazuri wa soka na ridhaa wengi wanatoka bara hili. Ni mijitu highly naturally selected yanayo stahimili magonjwa na taabu za duniani kuliko watu wengine duniani.

Ni bara lenye rasimali nyingi na za aina zote za hapa duniani. Ardhi yenye rutuba ya asili, misitu minene, viumbe vya aina zote - both micro and macro organisms, madini ya aina zote, maji mengi ya mabahari, maziwa mengi makubwa makubwa, mito mingi mikubwa mikubwa na kadhalika. Bara hili ni kama ile bustani ya Adeni kule paradiso inayosimuliwa na vitabu vitakatifu.

Ndiyo maana jamaa walipoliona bara hili, walilivamia. Walianza na kutuchukua utumwa na kutupeleka huko kwao kuwajengea nchi zao. Ndiyo maana utatukuta tuko huko, America tunaitwa maniga na kadhalika. Wakaona hiyo haitoshi wakatufanya makoloni yao ili waweze kuzichota vizuri maliasili zetu. Walipoona tunataka kuwa wajanja, wakaamua kutuwekeza (neocolonize). Lengo lao ni hilo hilo la kuendelea kuchota na kumiliki maliasili zetu hususani madini yetu, bandari zetu, rasilimali watu yetu na kadhalika.

Hiyo janja janja ya mikataba yao ya uwekezaji ndiyo mikakati yao ya neocolonization. Tunahitaji kuwa makini sana na hawa jamaa. Uwekezaji salama tunapaswa kuufanya wenyewe. Makampuni yetu ya wazalendo yanaweza. Hata hayo makampuni ya nje mitaji yao wanaipata kwa kukopa mabenki. Mikopo hiyo ndiyo inawawezesha kununua vifaa vya miradi na kuajili watalaam wa kutekeleza hiyo miradi. Hata kampuni zetu za ndani za wazalendo zinaweza sana kufanya mambo hayo. Hao siyo wajomba zetu. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe. Tuzinduke.
 
Kuna watu huwa nashindwa sana kuwaelewa akili zao zikoje.
Mtu huyo huyo kila siku hapa anaimba nyimbo za CCM kutwa humu JF, halafu sijui ni kitu gani kikamtokea mara moja moja kuja na mada ya aina hii hapa!

Huu ndio mfano mahsusi kabisa ya hayo anayoyaandika kwenye mada yake. Kwamba bara letu hili pamoja na kuwa na hizo raslimali zote tunazojigamba nazo, kitu tunachopungukiwa kitakuwa kwenye uwezo wa baadhi ya watu miongoni mwetu, wanaokwamisha bara hili lisinufaike na utajiri wake

Katika yooote aliyoandika kwenye mada hiyo, kasahau kabisa kulizungumzia hilo la kupungukiwa uongozi, ndiyo maana kila mara tunayumbayumba tu na kuchezewa hata na hivi vinchi kama UAE, Uingereza na vingi vinginevyo.

Namshauri, aanzie mageuzi huko ndani ya CCM.
Ni jana tu hapa, kaleta mada inayotisha watu wasipige kelele, wafungwe midoma, eti masharti ya taaluma zao hayaruhusu!
Leo hii kasahau hao hao wanaokerwa na hawa vikaragosi vya wakoloni wapya wanakataa ukoloni huo kwa njia zozote zitakazowezesha kuwazuia hawa mawakala, hata kama ni kutumia lugha wasiyoipenda wao!
Kasahau kuwa, hizo mbinu za kuweka vizuizi, ni moja ya njia hizo hizo za kukoleza ukoloni mambo leo.
 
Bara la Afrika ndiyo bara tajiri sana kuliko mabara yote duniani, kuanzia kwenye rasilimali watu (human resources) hadi kwenye rasilimali asili (natural resources).

Ni bara kubwa lenye majitu yenye nguvu yanayo stahimili dhoruba mbali mbali kuliko watu wengine duniani. Ndiyo maana utaona mabingwa wa dondi duniani ni watu toka bara hili, wachezaji wazuri wa soka na ridhaa wengi wanatoka bara hili. Ni mijitu highly naturally selected yanayo stahimili magonjwa na taabu za duniani kuliko watu wengine duniani.

Ni bara lenye rasimali nyingi na za aina zote za hapa duniani. Ardhi yenye rutuba ya asili, misitu minene, viumbe vya aina zote - both micro and macro organisms, madini ya aina zote, maji mengi ya mabahari, maziwa mengi makubwa makubwa, mito mingi mikubwa mikubwa na kadhalika. Bara hili ni kama ile bustani ya Adeni kule paradiso inayosimuliwa na vitabu vitakatifu.

Ndiyo maana jamaa walipoliona bara hili, walilivamia. Walianza na kutuchukua utumwa na kutupeleka huko kwao kuwajengea nchi zao. Ndiyo maana utatukuta tuko huko, America tunaitwa maniga na kadhalika. Wakaona hiyo haitoshi wakatufanya makoloni yao ili waweze kuzichota vizuri maliasili zetu. Walipoona tunataka kuwa wajanja, wakaamua kutuwekeza (neocolonize). Lengo lao ni hilo hilo la kuendelea kuchota na kumiliki maliasili zetu hususani madini yetu, bandari zetu, rasilimali watu yetu na kadhalika.

Hiyo janja janja ya mikataba yao ya uwekezaji ndiyo mikakati yao ya neocolonization. Tunahitaji kuwa makini sana na hawa jamaa. Uwekezaji salama tunapaswa kuufanya wenyewe. Makampuni yetu ya wazalendo yanaweza. Hata hayo makampuni ya nje mitaji yao wanaipata kwa kukopa mabenki. Mikopo hiyo ndiyo inawawezesha kununua vifaa vya miradi na kuajili watalaam wa kutekeleza hiyo miradi. Hata kampuni zetu za ndani za wazalendo zinaweza sana kufanya mambo hayo. Hao siyo wajomba zetu. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe. Tuzinduke.
Naunga mkono hoja
P
 
Sio kweli kwamba bara la Africa ni tajiri kuliko mabara yote kwa rasilimali watu au rasilimali asili.
Bara la Afrika ndiyo bara tajiri sana kuliko mabara yote duniani, kuanzia kwenye rasilimali watu (human resources) hadi kwenye rasilimali asili (natural resources).

Ni bara kubwa lenye majitu yenye nguvu yanayo stahimili dhoruba mbali mbali kuliko watu wengine duniani. Ndiyo maana utaona mabingwa wa dondi duniani ni watu toka bara hili, wachezaji wazuri wa soka na ridhaa wengi wanatoka bara hili. Ni mijitu highly naturally selected yanayo stahimili magonjwa na taabu za duniani kuliko watu wengine duniani.

Ni bara lenye rasimali nyingi na za aina zote za hapa duniani. Ardhi yenye rutuba ya asili, misitu minene, viumbe vya aina zote - both micro and macro organisms, madini ya aina zote, maji mengi ya mabahari, maziwa mengi makubwa makubwa, mito mingi mikubwa mikubwa na kadhalika. Bara hili ni kama ile bustani ya Adeni kule paradiso inayosimuliwa na vitabu vitakatifu.

Ndiyo maana jamaa walipoliona bara hili, walilivamia. Walianza na kutuchukua utumwa na kutupeleka huko kwao kuwajengea nchi zao. Ndiyo maana utatukuta tuko huko, America tunaitwa maniga na kadhalika. Wakaona hiyo haitoshi wakatufanya makoloni yao ili waweze kuzichota vizuri maliasili zetu. Walipoona tunataka kuwa wajanja, wakaamua kutuwekeza (neocolonize). Lengo lao ni hilo hilo la kuendelea kuchota na kumiliki maliasili zetu hususani madini yetu, bandari zetu, rasilimali watu yetu na kadhalika.

Hiyo janja janja ya mikataba yao ya uwekezaji ndiyo mikakati yao ya neocolonization. Tunahitaji kuwa makini sana na hawa jamaa. Uwekezaji salama tunapaswa kuufanya wenyewe. Makampuni yetu ya wazalendo yanaweza. Hata hayo makampuni ya nje mitaji yao wanaipata kwa kukopa mabenki. Mikopo hiyo ndiyo inawawezesha kununua vifaa vya miradi na kuajili watalaam wa kutekeleza hiyo miradi. Hata kampuni zetu za ndani za wazalendo zinaweza sana kufanya mambo hayo. Hao siyo wajomba zetu. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe. Tuzinduke.
 
Kuna watu huwa nashindwa sana kuwaelewa akili zao zikoje.
Mtu huyo huyo kila siku hapa anaimba nyimbo za CCM kutwa humu JF, halafu sijui ni kitu gani kikamtokea mara moja moja kuja na mada ya aina hii hapa!

Huu ndio mfano mahsusi kabisa ya hayo anayoyaandika kwenye mada yake. Kwamba bara letu hili pamoja na kuwa na hizo raslimali zote tunazojigamba nazo, kitu tunachopungukiwa kitakuwa kwenye uwezo wa baadhi ya watu miongoni mwetu, wanaokwamisha bara hili lisinufaike na utajiri wake

Katika yooote aliyoandika kwenye mada hiyo, kasahau kabisa kulizungumzia hilo la kupungukiwa uongozi, ndiyo maana kila mara tunayumbayumba tu na kuchezewa hata na hivi vinchi kama UAE, Uingereza na vingi vinginevyo.

Namshauri, aanzie mageuzi huko ndani ya CCM.
Ni jana tu hapa, kaleta mada inayotisha watu wasipige kelele, wafungwe midoma, eti masharti ya taaluma zao hayaruhusu!
Leo hii kasahau hao hao wanaokerwa na hawa vikaragosi vya wakoloni wapya wanakataa ukoloni huo kwa njia zozote zitakazowezesha kuwazuia hawa mawakala, hata kama ni kutumia lugha wasiyoipenda wao!
Kasahau kuwa, hizo mbinu za kuweka vizuizi, ni moja ya njia hizo hizo za kukoleza ukoloni mambo leo.
Mapinduzi ya fikra yanatakiwa kujengwa kuanzia katika ngazi ya chini kabisa ya mtu mmoja mmoja, vyama vije baadaye.
Tukiwa na wananchi wazuri kifikra, vyama na taasisi mbalimbali na hatimaye viongozi wa kitaifa, vyote vitakuwa vinaendelea kwa uelekeo mzuri kwa mustakabali mwema wa taifa.
Ni lazima tuwe na wananchi wanaojua na kusema baya ni baya na zuri ni zuri ili pia kuweza kuwashghulikia viongozi wapuuzi.
Hata kama haupo kwenye active politics, uwe mwalimu, nesi, daktari, mhandisi, mtaalamu wa fani yoyote, kasisi, mkulima, mfanyabiashara na maaskari wote, tukiungana bila kujali vyama, kudhibiti mwanasiasa yeyote asiyelinda maendeleo na uhuru wetu, Afrika itapanda juu kiuchumi kuliko tunavyodhani.
 
Kuna watu huwa nashindwa sana kuwaelewa akili zao zikoje.
Mtu huyo huyo kila siku hapa anaimba nyimbo za CCM kutwa humu JF, halafu sijui ni kitu gani kikamtokea mara moja moja kuja na mada ya aina hii hapa!

Huu ndio mfano mahsusi kabisa ya hayo anayoyaandika kwenye mada yake. Kwamba bara letu hili pamoja na kuwa na hizo raslimali zote tunazojigamba nazo, kitu tunachopungukiwa kitakuwa kwenye uwezo wa baadhi ya watu miongoni mwetu, wanaokwamisha bara hili lisinufaike na utajiri wake

Katika yooote aliyoandika kwenye mada hiyo, kasahau kabisa kulizungumzia hilo la kupungukiwa uongozi, ndiyo maana kila mara tunayumbayumba tu na kuchezewa hata na hivi vinchi kama UAE, Uingereza na vingi vinginevyo.

Namshauri, aanzie mageuzi huko ndani ya CCM.
Ni jana tu hapa, kaleta mada inayotisha watu wasipige kelele, wafungwe midoma, eti masharti ya taaluma zao hayaruhusu!
Leo hii kasahau hao hao wanaokerwa na hawa vikaragosi vya wakoloni wapya wanakataa ukoloni huo kwa njia zozote zitakazowezesha kuwazuia hawa mawakala, hata kama ni kutumia lugha wasiyoipenda wao!
Kasahau kuwa, hizo mbinu za kuweka vizuizi, ni moja ya njia hizo hizo za kukoleza ukoloni mambo leo.
Umetoa mchango mzuri ila nikurekebishe... Uingereza sio kinchi kidogo! Wacha kabisa!


CCM na vijana wao wanaowandaa kuwa Mashetani (UVCCM) unaona wanakuwaga na akili basi?! 🤣👍🏾🙌🏾
 
Mapinduzi ya fikra yanatakiwa kujengwa kuanzia katika ngazi ya chini kabisa ya mtu mmoja mmoja, vyama vije baadaye.
Tukiwa na wananchi wazuri kifikra, vyama na taasisi mbalimbali na hatimaye viongozi wa kitaifa, vyote vitakuwa vinaendelea kwa uelekeo mzuri kwa mustakabali mwema wa taifa.
Ni lazima tuwe na wananchi wanaojua na kusema baya ni baya na zuri ni zuri ili pia kuweza kuwashghulikia viongozi wapuuzi.
Hata kama haupo kwenye active politics, uwe mwalimu, nesi, daktari, mhandisi, mtaalamu wa fani yoyote, kasisi, mkulima, mfanyabiashara na maaskari wote, tukiungana bila kujali vyama, kudhibiti mwanasiasa yeyote asiyelinda maendeleo na uhuru wetu, Afrika itapanda juu kiuchumi kuliko tunavyodhani.
ujinga ni mzigo sana, mabepari yametengeneza ma puppet ndio wanaotumaliza. Adui wa mwafrika ni mwafrika mwenzie! Mtanzania anamalizwa na mtz mwenzie. usaliti ni mwingi sana!


JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Dunia ya sasa nyie mko bize na siasa za ukoloni sijui rasilimali wenzetu wako kwenye lab za tech wanatutengenezea whtasapp,tiktok ,facebook instagram na sie tunakuwa watumiaji na wao wanatengeneza billions za usd hakuna ncchi ambayo haijakuwa koloni la nchi nyingine ukizitafuta ni chache sana hata hao uae washakuwa koloni la uingereeza wamejikwamua kwa kutengamana na walioendelea wewe unataka ubinafsi na kujitenga hufiki kokote hata msanii prof j aliimba ukitakakuwin mjini shirikiana na wale magwiji utatoboa.
 
Bara la Afrika ndiyo bara tajiri sana kuliko mabara yote duniani, kuanzia kwenye rasilimali watu (human resources) hadi kwenye rasilimali asili (natural resources).

Ni bara kubwa lenye majitu yenye nguvu yanayo stahimili dhoruba mbali mbali kuliko watu wengine duniani. Ndiyo maana utaona mabingwa wa dondi duniani ni watu toka bara hili, wachezaji wazuri wa soka na ridhaa wengi wanatoka bara hili. Ni mijitu highly naturally selected yanayo stahimili magonjwa na taabu za duniani kuliko watu wengine duniani.

Ni bara lenye rasimali nyingi na za aina zote za hapa duniani. Ardhi yenye rutuba ya asili, misitu minene, viumbe vya aina zote - both micro and macro organisms, madini ya aina zote, maji mengi ya mabahari, maziwa mengi makubwa makubwa, mito mingi mikubwa mikubwa na kadhalika. Bara hili ni kama ile bustani ya Adeni kule paradiso inayosimuliwa na vitabu vitakatifu.

Ndiyo maana jamaa walipoliona bara hili, walilivamia. Walianza na kutuchukua utumwa na kutupeleka huko kwao kuwajengea nchi zao. Ndiyo maana utatukuta tuko huko, America tunaitwa maniga na kadhalika. Wakaona hiyo haitoshi wakatufanya makoloni yao ili waweze kuzichota vizuri maliasili zetu. Walipoona tunataka kuwa wajanja, wakaamua kutuwekeza (neocolonize). Lengo lao ni hilo hilo la kuendelea kuchota na kumiliki maliasili zetu hususani madini yetu, bandari zetu, rasilimali watu yetu na kadhalika.

Hiyo janja janja ya mikataba yao ya uwekezaji ndiyo mikakati yao ya neocolonization. Tunahitaji kuwa makini sana na hawa jamaa. Uwekezaji salama tunapaswa kuufanya wenyewe. Makampuni yetu ya wazalendo yanaweza. Hata hayo makampuni ya nje mitaji yao wanaipata kwa kukopa mabenki. Mikopo hiyo ndiyo inawawezesha kununua vifaa vya miradi na kuajili watalaam wa kutekeleza hiyo miradi. Hata kampuni zetu za ndani za wazalendo zinaweza sana kufanya mambo hayo. Hao siyo wajomba zetu. Tanzania itajengwa na watanzania wenyewe. Tuzinduke.
Kutwa kucha mtu mweusi ni kulalamika 😁😁😁

Wazungu na weupe wengine ongezeni kasi Hawa watu Bado hawajielewi
 
Umetoa mchango mzuri ila nikurekebishe... Uingereza sio kinchi kidogo! Wacha kabisa!


CCM na vijana wao wanaowandaa kuwa Mashetani (UVCCM) unaona wanakuwaga na akili basi?! 🤣👍🏾🙌🏾
EEEeeehEEEE Heeeeee!.
Sikubaliani na "urekebishaji" wako mkuu wangu 'Hohehahe', ninaelewa vizuri sana ninachokizungumzia hapa.
Wewe unatazama tulikotoka, mimi natazama tunakokwenda na 'potentia' tuliyonayo sisi. Ingekuwa ni kuchora 'chart/graph', ya kwetu inakwenda juu, ya kwao inashuka.
Miaka michache iliyopita unglinganisha India na Uingereza, ungesema kama ulivyosema hapa sasa hivi; lakini angalia sasa anakokwenda India 'relative to' Uingereza.

Niliiweka hapo maksudi tu kama mfano kujieleza, na nilitegemea pawepo na watu kama wewe kuona ulivyoona na kuamua kunijibu.

Ninajua sana alipo Mwingereza, kwa sanbabu nyingi tu hata za kibinafsi ambazo sitapenda kuzitaja hapa. Namshukuru sana kwa kuniwezesha nilivyoweza kupata uwezo kwa msaada wake. Simdharau hata kidogo, lakini inapokuja kwenye mambo ya u'snobbish' walio nao baadhi yao, na matatizo mengi wanayoyasababisha duniani kote hadi leo, sina sababu ya kutetea hayo.
 
EEEeeehEEEE Heeeeee!.
Sikubaliani na "urekebishaji" wako mkuu wangu 'Hohehahe', ninaelewa vizuri sana ninachokizungumzia hapa.
Wewe unatazama tulikotoka, mimi natazama tunakokwenda na 'potentia' tuliyonayo sisi. Ingekuwa ni kuchora 'chart/graph', ya kwetu inakwenda juu, ya kwao inashuka.
Miaka michache iliyopita unglinganisha India na Uingereza, ungesema kama ulivyosema hapa sasa hivi; lakini angalia sasa anakokwenda India 'relative to' Uingereza.

Niliiweka hapo maksudi tu kama mfano kujieleza, na nilitegemea pawepo na watu kama wewe kuona ulivyoona na kuamua kunijibu.

Ninajua sana alipo Mwingereza, kwa sanbabu nyingi tu hata za kibinafsi ambazo sitapenda kuzitaja hapa. Namshukuru sana kwa kuniwezesha nilivyoweza kupata uwezo kwa msaada wake. Simdharau hata kidogo, lakini inapokuja kwenye mambo ya u'snobbish' walio nao baadhi yao, na matatizo mengi wanayoyasababisha duniani kote hadi leo, sina sababu ya kutetea hayo.
GNP na GDP ya Uingereza inafanana na ya India? 😃
 
Mapinduzi ya fikra yanatakiwa kujengwa kuanzia katika ngazi ya chini kabisa ya mtu mmoja mmoja, vyama vije baadaye.
Tukiwa na wananchi wazuri kifikra, vyama na taasisi mbalimbali na hatimaye viongozi wa kitaifa, vyote vitakuwa vinaendelea kwa uelekeo mzuri kwa mustakabali mwema wa taifa.
Ni lazima tuwe na wananchi wanaojua na kusema baya ni baya na zuri ni zuri ili pia kuweza kuwashghulikia viongozi wapuuzi.
Hata kama haupo kwenye active politics, uwe mwalimu, nesi, daktari, mhandisi, mtaalamu wa fani yoyote, kasisi, mkulima, mfanyabiashara na maaskari wote, tukiungana bila kujali vyama, kudhibiti mwanasiasa yeyote asiyelinda maendeleo na uhuru wetu, Afrika itapanda juu kiuchumi kuliko tunavyodhani.
Unajua mkuu 'lebabu11', kuna kibindi tulisha anza kuelekea huko unakokueleza, lakini tukavurugika hapo katikati baada ya mageuzi yaliyotokea duniani kote na tukaanza kupoteza njia.
Hali tuliyo nayo sasa hivi ni ya kila mtu na lwake. Kila mtu anapambana kwa sababu yake siyo kwa sababu ya taifa.

Jambo la kushangaza ni kwamba, sisi tulioiga mtindo wa ubepari, hatukufahamu kwamba huko huko kulikozaliwa ubepari,maslahi ya nchi ndiyo namba moja, sisi waigaji tu, maslahi ya chama na viongozi ndiyo kila kitu.
Matokeo yake ndiyo haya, na tunavurugwa kila siku.
 
GNP na GDP ya Uingereza inafanana na ya India? 😃
Dah!

Sasa tena unataka twende huko kwenye 'nitty grtty' hizo? Fimbo tunazopigwa nazo kila siku kwa vipimo wanavyoweka wao?
Ngoja nikwambie, GDP ya India sasa ipo juu ya Uingereza, bado hujui?
Utanipeleka kwenye hiyo 'GNP', hata huko pengine hutopenda kuangalia wingi wa watu katika nchi hizo kama kigezo.

Lakini la muhimu zaidi ni kwamba nadhani hujanielewa ninakoelekea kimawazo. Nisome vizuri katika mchango wangu hapo juu. Sijasema popote kwamba hali ya maisha ya Uingereza ni duni kuliko India. Tafadhali, usikimbilie kwenda kwenye hitimisho bila kuelewa kilichoelezwa.
 
Dah!

Sasa tena unataka twende huko kwenye 'nitty grtty' hizo? Fimbo tunazopigwa nazo kila siku kwa vipimo wanavyoweka wao?
Ngoja nikwambie, GDP ya India sasa ipo juu ya Uingereza, bado hujui?
Utanipeleka kwenye hiyo 'GNP', hata huko pengine hutopenda kuangalia wingi wa watu katika nchi hizo kama kigezo.

Lakini la muhimu zaidi ni kwamba nadhani hujanielewa ninakoelekea kimawazo. Nisome vizuri katika mchango wangu hapo juu. Sijasema popote kwamba hali ya maisha ya Uingereza ni duni kuliko India. Tafadhali, usikimbilie kwenda kwenye hitimisho bila kuelewa kilichoelezwa.
Tunaongelea mambo kwenye maono na uwezo tofauti wa kufikiri komredi
 
Bara la afrika halina raslimali watu, nakataa! Halina kabisa! Ndio maana nchi nyingi za bara hili ni maskini. Nenda Maleysia, Russia, China huko ndo Kuna raslimali watu!
 
Tunaongelea mambo kwenye maono na uwezo tofauti wa kufikiri komredi
Haya sasa.
Una maana gani hapa, kwamba Uingereza wanao uwezo tofauti wa maono na kufikiri dhidi ya wahindi, au bado sijakuelewa maana yako?

Kama hivyo ndivyo unavyo dhani, hata huko huna kitu cha kutetea.
 
Back
Top Bottom