Wamachinga Simu 2000 wamshukia Albert Chalamila, wasema kauli kuwa machinga wanatakiwa kustaafu miaka mitatu ilhali wanasiasa hawastaafu inashangaza

Hivi huyu Chalamila na Nape si huenda biological father wao akawa ni mtu mmoja!
 
Wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao kwenye soko lililopo stendi ya mabasi Simu 2000 wamelaani vikali baadhi ya kauli zilizotolewa na Mkuu wa mkoa Dar es salaam, Bw Albert Chalamila baada ya mgomo uliofanywa na wafanyabiashara hao hivi karibuni.

Akizungumza na wanahabari, Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao bw Mussa Ndile amelaani kauli hizo na kumtaka mkuu wa mkoa kushughukia swala lao badala ya kuwabeza na kuona madai yao si ya msingi.

"Kweli mtu analia kwa uchungu, unasema anajiliza vimachozi kwasababu amefinywa na mumewe nyumbani! Na kwamba anajiliza kwa unafiki! Hizi kauli si nzuri na tunaomba zisijirudie tena. Sisi hatuna ubaya na Mkuu wa mkoa na ndio maana alipokuja mara ya kwanza tuliosha gari lake na tulimtunza mia mbili mbili zetu lakini alipokuja mara ya pili kwa kweli kauli zake zilituvunja moyo na tunaomba kauli kama hizi asizitumie tena" Alisisitiza bw. Ndile.

Mnamo Julai 8, wafanyabiashara wa soko lililopo ndani ya stendi ya mabasi ya simu 2000 waligoma na kufunga barabara wakipinga mpango wa kugawa sehemu ya eneo la soko hilo kwa ajili ya ujenzi wa karakana ya mabasi ya Mwendokasi (Dart)
 
Hapo ndio mlianza kukosea
 
dah hii nchi mbna usegeju umezidi sana watu wanaona kama ni ya kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…