Wamejenga ukumbi wa kufanya sherehe tunapokaa. Weekend hatulali

Wewe wasema, yeye kafuata taratibu wewe huna guts za kuchalange chochote we mpangaji tu, kibaya zaidi hudai risiti kwa mwenye nyumba subiri TRA wakudake tarehe 02
We jamaa bila shaka utakua mmiliki wa kagrosari na unasumbua sana watu hapo mtaani kwenu.
 
Wachangieni waweke sound proof
 
Omba hata kazi ya ulinzi hapo hapo mda wa shughuli unapiga kazi kuliko kukosa usingizi kwa bure bure
 
Poleni. Kisheria, kama amejenga ukumbi bila kufuata utaratibu basi amefanya makosa.

Iko hivi, bilashaka maeneo hayo yatakuwa ni maeneo ya makazi; ambapo Sheria ina-suggest yanapaswa yawe na utulivu. Mtu akitaka kubadilisha matumizi (change of use) na kufanya biashara anapaswa aombe kibali cha kubadilisha matumizi kinachotanguliwa na tangazo litakalobandikwa ili kukaribisha maoni ya wakazi kuona kama wanaafiki au la.

Iwapo amejenga ukumbi kiholela mnaweza kufungua kesi Mahakamani. Cause of action itakuwa nuisance ambayo inaweza kuwafidia wakazi mlioathirika na kadhia hiyo.

Tafuteni Wakili awaongeze katika hili kwa kumuandikia demand notice ya kumtaka aweke vizuia sauti (sound proof); akishindwa mumpeleke Mahakamani akajibu tuhuma zinazomkabili.

Sijajua uko mkoa gani, lakini kama ungekuwa Dodoma bilashaka ningekuwa msaada. Nawatakia kila la kheri.
 
Umeeleweka.
 
Huenda ni Makazi na Biashara ,kama mtu upo serious inabidi ununue eneo lililopimwa kwa matumizi ya makazi onlymhapo hautakuta Bar wala club ila ukichukua makazi na biashara inabdi ujiandae kisaikolojia maana wengi wanatumia kwa kufanya biashara.
Basi usingemjibu moja kwa moja kuwa yupo kwenye skwata. Nchi hii mipango miji haifuatwi ndio maana unaona bar,clubs na vitu kama hivyo viko residential areas au hata karibu na shule na hospitali.
 
Basi usingemjibu moja kwa moja kuwa yupo kwenye skwata. Nchi hii mipango miji haifuatwi ndio maana unaona bar,clubs na vitu kama hivyo viko residential areas au hata karibu na shule na hospitali.
Unakuta kuna bar halafu inafuatia hospital
Au shule bar na gesti zimefuatana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…