Wamiliki wa lodge kuweni serious

Wamiliki wa lodge kuweni serious

Kaka naona unaijua sana na hii sekta. Mungu akijalia mwisho wa mwaka huu nitaingia huko naomba nikutafute nipate madini.
Tiles za bafuni kuteleza na kuweka tiles za room unapachika washroom ni kosa kiufundi, halafu mopa ni 2500 hadi 3000 walau ukikaweka bafuni mteja akioga atajiongeza asukume hata maji lakini mtihani sana
 
Wamiliki wawe wanawapa short training wafanyakazi wao wajue hawapo hapo ku-facilitate fumanizi na umbeya.

Kuna jamaa amepata usumbufu toka kwa mtu asomjua akimtuhumu kutembea na mumewe baada ya kupewa namba toka Kwa wafanyakazi wa hiyo hotel .
Eti alienda na picha kwenye Simu akiuliza Huyu anakujaga hotel hii na Mwanamke, wafanyakazi wakajichanganya wakasema ndiyo,
Akawaambia nipeni namba ya huyo mwanamke wakatoa, Dada wa watu hana analojua anashangaa anatumiwa sms kwa mtu ambae hamjui kabisa.

Wapeni elimu ya usiri na privacy ya wateja.

Na itawasaidia kuepukana na unnecessary cases za kuitwa polisi na mahakamani Kama mashahidi.

Avoid giving information voluntarily because it can cost you much.
 
Pesa zangu nyingi zinaishia kwenye kulala, kama nalipa mwenyewe something decent…. From 50k na kuendelea. Kama wanalipa kazini wana rate zao i’ll get something better.

Japo ni kweli vikero kero vipo here and there. Kama kuna kitu siwezi kumsikiliza mtu hata awe nani ni anipe ushauri wa kucut cost kwenye malazi. Mi nateseka kutafuta pesa nilale kama mkimbizi! Na kwasisi wanawake usalama ni kipaumbele, bora miamba wanaweza pambana.

Unless kusiwe na a decent place, kuna wilaya nilienda…. Hizo lodge 🙆🏼‍♀️ nzuri kuliko zote ni elfu 20, ikabidi niende kugonga hodi kanisani, wana hostel walinihifadhi nikamaliza mambo yangu nikaondoka.
 
Sometimes mtu anasafiri analazimika kuchukua chumba lodge Kwa sababu mbalimbali ikiwemo ukaribu wa anapokwenda mfano kikazi mtu atachukua lodge karibu na ofisi, au ukumbi wa mikutano na kadhalika. Sometimes kwa sababu ya lodge zingine kuwa zimejaa n.k..

Lakini sasa unaona lodge nzuri Kwa nje na hata ndani Kwa macho unaona iko Sawa, unalipia ulale unashangaa na unayo kutana nayo.

1. Feni inapiga kelele.
2. Bomba bovu maji yanatiririka bafuni.
3. Vitasa vibovu.
4. Mlango wa bafuni haufungi.
5. Taa bafuni haiwaki
6. Kitanda kinatoa milio
7. Mto ngumu Sana au mlaini Sana..
8. Feni haipungui wala kuongezeka Ama uwashe au uzime.
9. AC inapiga kelele
10. Tiles bafuni zina kutu.
11. Wahudumu Wana makelele.

Mradi matatizo ni mengi ambayo mtu anaejali biashara yake ni rahisi kabisa kutatua.

Nashauri kama mtu unamiliki lodge au kuendesha uweke utaratibu wa kulala wewe mwenyewe kila chumba Kwa mda Fulani ukague ujirishishe na huduma unazotoa.

Kuna lodge chumba kimoja kina joto kuliko chumba kingine Nakadhalika.

Kuweni serious, lodge ni sehemu ya mteja kulala comfortable sio kuwaza wateja wote wanaenda kwa ngono tu na kuondoka.
Taulo je???
 
Kigoma nililala ka lodge kapya, kagorofa hivi… kako barabara kama unaenda lake Tangayika hotel, Kasafiiii, very decent kwa 40 au 45k sikumbuki vizuri.

Mmiliki apewe maua yake, sijui sa hivi ina hali gani maana imepita karibu miaka 2.
 
Sijui wana matatizo gani...

Kwa nje unaona lodge kali ina hadi bustani, ingia ndani sasa ukutane na mishuka au miforonya michafu...

Na kuna lodge nyingine zina vyumba ndani kwa ndani hakuna hata hewa safi, yaani ni kama uchukue kiberiti ukiweke ndani ya bakuli...
😂😂😂😂 haaaaa!
 
Kuna kipindi nilikua mwanza ikabidi nichukue chumba maeneo ya nyegezi kwa ajili ya kuwahi usafiri
Nikaenda hotel moja inaitwa "Passion hotel" ile hotel chumba nilichukua 35k ila cha ajabu maji yakawa hayatoki bafuni ikabidi nimfate mhudumu akaishia kunijibu kwamba kama hayatoki unachukua ndoo unaenda kuchota chini kwenye kisima unapump ukizingatia nilikua vyumba vya ghorofani
Mda huo huo nikamwambia rudisha pesa haraka kabla haijawa vurugu, ikabidi nichukue pesa niende lodge nyingine za karibu nilipata huduma nzuri sana zaidi ya hotel ile ya kijinga tena kwa bei ya kawaida ya 20k.
Ahahaha Kidume unabebeshwa ndoo unaenda kuchota maji kisimani daah!! hao jamaa hawako serious
 
Nimechek mpaka watoto wakaniuliz unachek nn baba, imebidi nizuge nisema picha zinu hizi kwenye simu zinanichekesha.!!!!!
Dah.! 3 hrs ndani ya chooo.! Umenifurahisha as if comedy clip kumbe ndo maisha yanaendelea.
Tena choo chenyewe kidunchuuu 😂😂😂😂 nimecheka hadi nimelia, ila nimemuonea huruma sana.
 
😀😀Hoteli gani Dodoma hizo mbaya ebu tutajie kama ni St Gaspar Hotel,Morena Hotel,NAM Hotel,Bestern Western City Hotel,Dodoma Hotel,African Dreams,Dear Mama Hotel,Golden Crown Hotel,Nashera Hotel au zipi😀😀😀

Rudi shule kama huwezi kujua tofauti ya guest house,lodge,motel,rest house,inn na hotel
Unambishia tu bure, nyingi hapo ulizotaja ni
🗑️🚮

Sasa kama NAM jamani? Dodoma hotel? Dear mama???? Golden crown??????? Hata nashera na morena ni nzuri ila sio kwa thamani ya pesa wanayochaji, tena kama Morena kuna baadhi ya vyumba ukioga maji hayasogei/hayaendi yanajaa!!!!! Nashera vyumba ni vingi sana na havijai…. So unaweza pewa chumba hakijatumika wiki, na hawapiti kuangalia usafi, ukikipewa jiandae na chafya.

Maramia ungemtajia Rafiki na yule jirani yake… Opposite na shoppers. Nisiyoijua ni hiyo Bestern ninini sijui, ndio hiyo mpya ya area D???

Hatukosoi biashara za watu kwa ubaya wamiliki wafuatilie, wateja hatulimi pesa!
 
Unambishia tu bure, nyingi hapo ulizotaja ni
🗑️🚮

Sasa kama NAM jamani? Dodoma hotel? Dear mama???? Golden crown??????? Hata nashera na morena ni nzuri ila sio kwa thamani ya pesa wanayochaji, tena kama Morena kuna baadhi ya vyumba ukioga maji hayasogei/hayaendi yanajaa!!!!! Nashera vyumba ni vingi sana na havijai…. So unaweza pewa chumba hakijatumika wiki, na hawapiti kuangalia usafi, ukikipewa jiandae na chafya.

Maramia ungemtajia Rafiki na yule jirani yake… Opposite na shoppers. Nisiyoijua ni hiyo Bestern ninini sijui, ndio hiyo mpya ya area D???

Hatukosoi biashara za watu kwa ubaya wamiliki wafuatilie, wateja hatulimi pesa!
Wadanganye washamba wenzio labda.....Hoteli zenye hadhi ya nyota nne kama St Gaspar(yenye presidential suite ndani),Morena,Dodoma Hotel,Royal Village,Best Western City Hotel unasema takataka 😀😀😀
Huyo alienda kwenye guest houses ndio akakutana na hizo changamoto sio Hoteli. Tofautisha hadhi ya guest house,lodge na Hotel
 
Unambishia tu bure, nyingi hapo ulizotaja ni
🗑️🚮

Sasa kama NAM jamani? Dodoma hotel? Dear mama???? Golden crown??????? Hata nashera na morena ni nzuri ila sio kwa thamani ya pesa wanayochaji, tena kama Morena kuna baadhi ya vyumba ukioga maji hayasogei/hayaendi yanajaa!!!!! Nashera vyumba ni vingi sana na havijai…. So unaweza pewa chumba hakijatumika wiki, na hawapiti kuangalia usafi, ukikipewa jiandae na chafya.

Maramia ungemtajia Rafiki na yule jirani yake… Opposite na shoppers. Nisiyoijua ni hiyo Bestern ninini sijui, ndio hiyo mpya ya area D???

Hatukosoi biashara za watu kwa ubaya wamiliki wafuatilie, wateja hatulimi pesa!
Best Western City Hotel ipo katikati ya mji pembeni ya TRA.

 
Sometimes mtu anasafiri analazimika kuchukua chumba lodge Kwa sababu mbalimbali ikiwemo ukaribu wa anapokwenda mfano kikazi mtu atachukua lodge karibu na ofisi, au ukumbi wa mikutano na kadhalika. Sometimes kwa sababu ya lodge zingine kuwa zimejaa n.k..

Lakini sasa unaona lodge nzuri Kwa nje na hata ndani Kwa macho unaona iko Sawa, unalipia ulale unashangaa na unayo kutana nayo.

1. Feni inapiga kelele.
2. Bomba bovu maji yanatiririka bafuni.
3. Vitasa vibovu.
4. Mlango wa bafuni haufungi.
5. Taa bafuni haiwaki
6. Kitanda kinatoa milio
7. Mto ngumu Sana au mlaini Sana..
8. Feni haipungui wala kuongezeka Ama uwashe au uzime.
9. AC inapiga kelele
10. Tiles bafuni zina kutu.
11. Wahudumu Wana makelele.

Mradi matatizo ni mengi ambayo mtu anaejali biashara yake ni rahisi kabisa kutatua.

Nashauri kama mtu unamiliki lodge au kuendesha uweke utaratibu wa kulala wewe mwenyewe kila chumba Kwa mda Fulani ukague ujirishishe na huduma unazotoa.

Kuna lodge chumba kimoja kina joto kuliko chumba kingine Nakadhalika.

Kuweni serious, lodge ni sehemu ya mteja kulala comfortable sio kuwaza wateja wote wanaenda kwa ngono tu na kuondoka.
Hapo kwenye kitanda kupiga kelele kwangu ndo kero namba moja
 
Back
Top Bottom