Mwishokambi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2020
- 390
- 1,425
Kuanza kuisema sema timu yetu vibaya na kuanza kushambulia kocha kuwa alichelewa kufanya sub, kwamba Zimbwe ameshazeeka hana uwezo wa kumweka benchi Nouma, mara Ngoma alichoka na ilibidi Mavambo aingie, sijui Ahoua hana uwezo wa kuwa MVP anacheza slow sana, maneno kibao baada ya sare ya leo.
Mimi nadhani kwa sasa tukianza kukosoa kwa kuponda timu yetu tutatoka kwenye mstari mapema sana, zipo changamoto nyingi ndani ya timu yetu kuanzia benchi la ufundi hadi baadhi ya wachezaji lakini kwa sasa muda tuliokuwa nao wa kuanza kutukana na kuzomea uongozi sio wakati wake kabisa.
Soma Pia: FT | Simba SC 2-2 Azam FC | NBC Premier League | Benjamin Mkapa | 24 Februari, 2025
Tuache uongozi uendelea kupambana hadi mwisho tuone, kama kuna ukosoaji basi tukaambiane kwenye matawi yetu na sio humu kwenye mitandao ya kijamii, adui yetu anafuatilia nyendo zetu mwanzo mwisho, adui yetu hajalala, ananunua mechi huku akihakikisha anaharibu mechi zetu, kwa hiyo sisi tuna wakati mgumu sana msimu huu wa ubaya ubwela.
Adui yetu yuko huko anashangaa mbuga sio kwa bahati mbaya, yuko kwenye heka heka ya kutuangamiza tarehe 08 machi, hivyo sisi tuuungane mwenye shoka, kisu, jembe, jiwe ashike kwa ajili ya tarehe 8 machi, vinginevyo tutawakatisha tamaa wapiganaji wetu walio vitani.
Asanteni
Mimi nadhani kwa sasa tukianza kukosoa kwa kuponda timu yetu tutatoka kwenye mstari mapema sana, zipo changamoto nyingi ndani ya timu yetu kuanzia benchi la ufundi hadi baadhi ya wachezaji lakini kwa sasa muda tuliokuwa nao wa kuanza kutukana na kuzomea uongozi sio wakati wake kabisa.
Soma Pia: FT | Simba SC 2-2 Azam FC | NBC Premier League | Benjamin Mkapa | 24 Februari, 2025
Tuache uongozi uendelea kupambana hadi mwisho tuone, kama kuna ukosoaji basi tukaambiane kwenye matawi yetu na sio humu kwenye mitandao ya kijamii, adui yetu anafuatilia nyendo zetu mwanzo mwisho, adui yetu hajalala, ananunua mechi huku akihakikisha anaharibu mechi zetu, kwa hiyo sisi tuna wakati mgumu sana msimu huu wa ubaya ubwela.
Adui yetu yuko huko anashangaa mbuga sio kwa bahati mbaya, yuko kwenye heka heka ya kutuangamiza tarehe 08 machi, hivyo sisi tuuungane mwenye shoka, kisu, jembe, jiwe ashike kwa ajili ya tarehe 8 machi, vinginevyo tutawakatisha tamaa wapiganaji wetu walio vitani.
Asanteni