Wana Yanga wenzangu kinachoenda kufanyika Sudan na Al Hilal siyo mpira ni vita!

Wana Yanga wenzangu kinachoenda kufanyika Sudan na Al Hilal siyo mpira ni vita!

Uongozi wa Klabu ya Al Hilal umezuia mchezo wao wa Klabu Bingwa dhidi ya Yanga kuonyesha kwenye Tv wala kutangazwa kwenye Redio...

Porojo tu za karumekenge hizo! Usitudanganye hapa tutauona tu mnavyonyukwa magoli! Mnataka mkifungwa msingizie kuwa mlifanyiwa fujo kwa vile mpira haukuonyeshwa! Marefa, makamisaa na viongozi wengine wa kimataifa watakuwa pale kwa hiyo kipigo mtakachokula wala hakitakuwa na hujuma!
 
Unahamisha magoli siyo! Wewe sema tu hao waarabu wenu koko wameingiwa na mchecheto.

Na kwa bahati nzuri wanatambua fika Yanga imesheheni wachezaji wenye uzoefu na mashindano ya kimataifa. Hivyo hawawezi kutoka kirahisi tu mchezoni kupitia hizo mind game zao.
Hizo ngonjera zako zihifadhi tu,kama mlishindwa kuonyesha huo ukubwa wenu hapa basi imeshakula kwenu. Mnaenda kudhalilishwa na kuliabisha Taifa.
 
Imagine mchezaji kama Bernard Morrison, eti unamtishia nyau! Aisee anakumaliza. Yaani hao Wasudan waombee Nabi aanzishe tu kikosi dhaifu!

Ila akipanga kikosi chake kwa usahihi, kiukweli uwezekano wa kufuzu ni mkubwa sana.
Yaani timu kubwa mnaweka matumaini yenu kwa kichaa Morrison? Ama kweli mumevurugwa nyie si bure.
 
Sasa wale mashabiki wa Yanga ambao walikuwa wanasema Al Hilal ameridhika na matokeo ya kwa Mkapa na kuwa kule kwao wata defense ili wapate sare ya 0-0 wao wavuke naona wameanza kugundua hawakuwa sahihi

Mimi naamini hii mechi itaoneshwa live, kinachofanywa saizi hapa ni figisu za kuwatoa mchezoni ili focus yao katika kipindi hiki ipotee kwenye kuhangaikia kwenye maswala ya broadcasting

Na sio hivyo tu, wataweza kutengeneza propaganda nyingine ambazo zitaingia kwenye rotation katikati ya hili sakata ambalo wana dili nalo saizi.

Hayo yote yatafanyika wakati Yanga bado yupo hapa hapa Tanzania, unaweza ku imagine watakutana na figisu za kiasi gani wakifika huko.

Yanga na mashabiki wake wanapaswa waelewe kuwa timu pinzani haiwezi ikafanya hayo yote kwa lengo la kutafuta sare tena ikiwa nyumbani.
Anaehangaika na broadcast ni Azam. Kwa ajili ya biashara zake. Mechi kuonyeshwa au kutokuonyeshwa hakuna athari yoyote uwanjani
 
Hawa waarabu siyo kama ni wagumu kiviile, ndiyo maana wanaanza mikwala mapema,ila mlikosea sana kuwaacha salama hapa, mngewapiga kama migoli mitatu bila wangelegea hata hizo amsha amsha zao zisingekuwa na nguvu. Hawa wanajua wakiwadindia mkatoka sare tasa tu wamepita.

Na hili ndio kosa lenu Yanga mmewadharau Sana Al Hilal na ndicho wanachotaka.
 
رفتن نوعش نکسوس تلسننتط نکوواففبرشگ موودسسونانطسگ ننکاهستوگطپت[emoji378][emoji378][emoji378][emoji378] MOCHWARI کتثحگکوسوث[emoji196][emoji196][emoji196]UTOPOLOکوسکککطنKIBWANA SHOMARI ننیمنگAL HILAL
😂😂😂Aunt
 
Yanga itafanya vizuri confederation cup.
Sioni timu ya cecafa itakayofika semi finals za Championships mwaka huu.
Ila kombe la washindi, Yanga itAFANYA VIZURI, NAAMINI HILO.
Mungu awasaidie lakini Al hilal nao si Haba wanajitahidi
 
Ila Al Hilal ndio ana nafasi kubwa ya kushinda maana atmosphere ya uwanja wao usipime.
Hakuna cha atmoshere wala nini, ukiwa na uwezo mkubwa unashinda. Kama atmoahere inawabeba, mbona hawajawahi kuwa mabingwa wa Africa??
 
Sasa unaposema Yanga ni nzuri away kuliko ikiwa Lupaso unakuwa umetumia vigezo vipi? Hiyo ni ishara ya kupagawa mkuu.[emoji23]
Lini wametoka nje kucheza hao Yanga[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]!!!muulize
 
رفتن نوعش نکسوس تلسننتط نکوواففبرشگ موودسسونانطسگ ننکاهستوگطپت[emoji378][emoji378][emoji378][emoji378] MOCHWARI کتثحگکوسوث[emoji196][emoji196][emoji196]UTOPOLOکوسکککطنKIBWANA SHOMARI ننیمنگAL HILAL
Wamekanusha muda mfupi uliopita. Wamesema itakuwa kama walivyotangaza mwanzo!
 
Back
Top Bottom