KWELI Wanachama wa NSSF na PSSSF wanaweza kutumia Michango yao kama dhamana ya kuchukulia Mikopo Kujenga, Kuboresha au Kununua nyumba

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Mimi hela zangu nimpe NSSF, NSSF anaenda kufungua fixed account benki ya biashara. Kisha mimi tena naenda huko CRDB kukopa nusu ya pesa zangu mwenyewe zilizowekwa kwao na NSSF kwa riba kubwa na dhamana ya pesa hizo hizo zilizo mara mbili yake. Na kwakuwa ni mkopo wa makazi utakuwa wa muda mrefu.

Biashara kichaa hii, kwanini NSSF wasinikopeshe wenyewe kwa kuchangia gharama kiduchu za uendeshaji wa huu mchakato.
 
Makato yakizidi si unaiba iba umalize Mwezi.. kama wao wanakuibia kwa riba why you usiibe.. malipo hapa hapa duniani ule msemo nimeukumbuka.
 
Msiifurahie hio mikopo...akuna mkopo wenye manufaa...lengo la mikopo kwa nchi yetu hii ni kukudidimiza uzidi kuwa masikini...

Mkopo ni utumwa ndugu zangu​
Labda ni utumwa kwako, dunia hii inaendeshwa kwa mikopo, iwe ughaibuni au popote pale. Tatizo litakuja iwapo mkopo hautoutumia vyema.
 
Wakikujibu naomba uniambie. Kama wanakata hukohuko nina hela nyingi nikazipunguze nijenge lodge ndogo.
Unakopeshwa kulingana na salary slip Yako inavyo soma...ila wenyewe wanakopeshana mamilioni...pesa zetu🙈🙈🙈​
 
Unakopeshwa kulingana na salary slip Yako inavyo soma...ila wenyewe wanakopeshana mamilioni...pesa zetu🙈🙈🙈​
Sasa kama ni mambo yaleyale ya kuangalia 1/3 ibaki kwenye salary slip yako, kuna haja gani ya kutuambia hao PSSSF na NSSF wanafadhili watumishi au wanachama wao kukopa ili wajenge au kukarabati nyumba?.
Kama ni hivyo, siendi kukopa.
 
Msiifurahie hio mikopo...akuna mkopo wenye manufaa...lengo la mikopo kwa nchi yetu hii ni kukudidimiza uzidi kuwa masikini...

Mkopo ni utumwa ndugu zangu​
Duniani kote mikopo ndiyo inayoleta maendeleo. Miradi na uwekezaji wote mkubwa asilimia kubwa hufadhiliwa na mikopo. Umuhimu ni kukopa kwa malengo siyo kama Tanzania inavyokopa halafu inaenda kutumia kufanya sherehe za Uhuru. Huo unakuwa upumbavu
 
Ni jambo zuri iwapo itabainika kuwa kweli.

Kwa kuwa umesema ni taarifa inayofanyiwa kazi nadhani tutapata taarifa kamili soon

Ila nina wasiwasi kwamba iwapo jambo hilo likafanyika, basi mifuko mingi itakuwa kwenye Ukata.

Kama mnakumbuka, Serikali imekuwa ilikopa fedha nyingi kwenye hii mifuko, hivyo Sina uhakika kama baada ya kukopa iliweza Kurejesha.

Kuna wakati niliwahi kwenda ofisini kwao, kuomba huu Mkopo lakini sikufanikiwa. Kipindi hicho ndiyo kulikuwa na vuguvugu la Serikali kutaka kuunganisha mifuko hii.
 
Kwamba kila mfuko iwe umechangia miaka 9 ama kwa pamoja baina ya hiyo mifuko iwe imetimia miaka 9?
 
Lucas mwashamba yupo?
Analizungumziajee hili
 
Hivi nini kazi / maana ya Pension ?

Wakikopa wakashindwa kulipa inakuwaje Pension yao Inakufa ?, Na wakizeeka wanakuwa mzigo wa nani ?

Hivyo nauliza tena.... Nini maana / kazi ya Pension ?
 
Wakikujibu naomba uniambie. Kama wanakata hukohuko nina hela nyingi nikazipunguze nijenge lodge ndogo.
Mie nilishazilambaga huwa siwaachii hawa jamaa, Kila contract na mafao yake yaani nikiutumikia mkataba Kwa kampuni A Kwa miaka 4 nikimaliza nalamba changu labda itokee nimeunganisha kazi kampuni B lakini kama nita-delay Kwa miezi kadhaa uraiani kijiwe changu huwa ni NSSF na bahasha yangu kufuatilia mafao

Hii nzuri Kwa watu wa sekta binafsi maana unakuta unaingiza Kwa mwezi ela nzuri kiasi ila ukienda bank hukopesheki simply because taasisi binafsi huwa zinatoa mkataba wa mwaka mmoja mmoja hata kama utadumu nao miaka kadhaa na bank wanataka umri wa mkopo uendane na umri wa mkataba yaani kama umeomba loan miaka 2 basi uwe na contract ya miaka 2 and above, vinginevyo mwajiri akuwekee kifua na wengi miyeyusho wanajua wakikudhamini wanahofu ukifanya chini ya kiwango watapata kazi ya kuku-retain mpaka mkopo wako uishe
 
Reactions: K11
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…