Wanachofanya AZAM TV kwenye mpira ni uhuni na utapeli, wadau amkeni

Wanachofanya AZAM TV kwenye mpira ni uhuni na utapeli, wadau amkeni

Azam Media kuna shida kubwa ya viongozi wengi kukosa weledi na dira ya wapi wanataka taasisi hiyo kuelekea.

Na shida kubwa ni aina ya ajira zao kuwa za kijamaa na urafiki, na sio uzoefu na taaluma. Ndiyo maana haya yanatokea.

Viongozi wengi pale hawafukuziki hata wafanye makosa ya namna gani, kwa sababu labda wameletwa na Yusuf.

Niliwahi kuzungumza na Tido wakati akiwa pale, nikimuuliza kukosa kwao kukua, kwa maana ya kuongeza channels za michezo.

Alisema kuwa, amekosa timu sahihi ya kukuza taasisi, kwani wakati wote akitoa maelekezo/ mwongozo huwa kuna utekelezaji hafifu.

Fikiria, baada ya kustaafu Tido kwa sasa Kahemele ndiyo kiongozi Mkuu pale, ila yeye yuko kwenye nafasi hiyo kwa kuwa walikuwa naye kwenye timu ya Azam kabla kuanza TV.

Hadi sasa wana miaka kumi tangu walipoanza, ila bado wana channels saba au nane tu, nyingine zote siyo zao. Kuna shida pale.

Ova
hata upande wa klabu ni hivyo hivyo,.....

jamaa hawapo serious
 
kuna zile azam one na two sielewagi ni moja au zina utofauti,maudhui yanajirudia ya one unayakuta two na two unayakuta one,kuna ile cinema zetu movie za ajabu ajabu tamthilia mbovu

sport hd hazieleweki zinaingiliana maudhui pia,azam nimeambulia channel ya kix tu naangalia zangu waki yuen biao na kina samu hongi enzi zao lakini ukijichanganya e movie,movie moja unaangalia masaa ma5 kuna matangazo ya waarabu muda wote[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Na hakuna offer ya aina yoyote kama wenzao startimes, DStv,mzee bakhresa aache tamaa hela anazopata ni nyingi sana kupitia ving'amuzi vyake
 
Hivi kwanini TBC wasiwe na channel ya michezo tu, japo hata waoneshe ndondo cup, chandimu na umiseta?
Kuwategemea Azam pekee ndio tunaishia kupata tabu hizi.

Ngoja nimwambie Nape na Ayubu walichukue hili kama majaribio ya kuwa bora zaidi kurusha matangazo.

Hatuwezi kuwa na TBC chovu.
 
Wakuu Azam tv hivi karibuni imeanza uhuni ambao lazima ukemewe!

Azam walijinasibu kuonyesha ligi ya ufaransa (Ligue 1) ligi ya ujerumani (bundesliga) ligi kuu ya Tanzania (NBC) na hivi karibuni wakasema na Ligue ya waarabu kwa kina Ronaldo...
Nakuuliz hivi mwezi wa June fifa world cup je, zitaonyesha mpira ya world cup ipo kweny Azam tv?
 
Hivi kwanini TBC wasiwe na channel ya michezo tu, japo hata waoneshe ndondo cup, chandimu na umiseta?
Kuwategemea Azam pekee ndio tunaishia kupata tabu hizi.
TBC pale wamejaa wazee tupu mbaya zaidi wanawalisha ujinga na uzembe baadhi ya vijana wa hapo ndio mana TBC hakuna content inayofatiliwa.

atleast sasa hv wameshtukia fursa ya kuonyesha mechi za CAF na Fifa kitu ambacho walitakiwa kukifanya tangu kitambo.
 
Siku azam wakilogwa copyright ya kuonyesha NBC premiere L. Ikaingia dstv au kwingine kokote,basi hapo ndiyo nafunga nao mkataba rasmi kulipia kifurushi.
Unaweza kudhani hii itasaidia ila nakuambia ligi itaporomoka vibaya mno.

Kabla ya hii copyright ya Sasa ya Azam kuonyesha ligi, pia DStv walitaka kuonyesha ligi ila wao walitaka kuonyesha mechi za simba na Yanga tuu wakati Azam yeye anaonyesha mechi zote za ligi.
 
Hahahahah!!!!. ni movie za uturuki, ufilipino, documentary za mpira kila siku msuva, na dogo fulani hivi wa kike anachezea twiga stars. kuna baadhi ya channel kamera low quality utazani tupo miaka ya 1900's.
 
Ila tuache masihara Zanzibar ingekuwa inajitegemea kama nchi pengine ingekuwa mbali sana imagine kwa sh 12000 tu kwa mwezi naangalia ligi zote kubwa Ulaya mfano Leo Kuna FA cup final, DFB Pokal, Coupe de France, Caf champions ligi final, zote nimeziangalia kasoro huu utumbo wa NBC tu ndio huwezi kuona.
 
Unawaza azam anaweza akawafurahisheni na kuwaridhisha wateja wake wote mamilioni nchini. Lazima mtakuwepo pimbi kama nyinyi msioona jema popote. Hamna shukrani kwa hata hicho anachofanya mtamsaidia nini kumboresha?
Mkuu ukimjibu mdau yeyote kwa kumwelewesha itapendeza sana mkuu wangu.
 
Kwenye EURO 2024 ni bora kutumia DSTV tu huko Azam level zao ni ligi za kwetu tu.
 
Back
Top Bottom