Wanachotaka wafanyabiashara kwenye mgomo ulioanza leo tarehe Juni 24, 2024 Kariakoo na nchi nzima

Wanachotaka wafanyabiashara kwenye mgomo ulioanza leo tarehe Juni 24, 2024 Kariakoo na nchi nzima

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
1. Kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao zaidi ya 10 na mamlaka ya mapato TRA ,hawakupata majibu.

2.kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao na serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Ilala wakiomba Waziri wa fedha afike kuwa sikiliza lakini Waziri wa fedha hakuwahi kwenda.

3.Mkuu wa Wilaya ya Ilala amepambana sana kuhakikisha mgomo hautokei (Wafanyabiashara wanampongeza) Mkuu wa wilaya ya ilala akaomba Wafanyabiashara wasubiri mwezi mmoja ,ili awasiliane na Viongozi wake kwanza

Mwezi ukaisha Mkuu wa Wilaya akapuuzwa na viongozi wake wa Juu.

4. Mkuu wa Mkoa mara zote hizi hakuwahi kuonekana katika vikao chochote cha Wafanyabiashara, wala hakuwahi kusaidia kupeleka malalamiko ngazi za Juu.

Ameonekana Jana tu, ktk Vitisho.

5. Viongozi wa Wafanyabiashara wakaomba waende Dodoma kuonana na Waziri wa fedha ili madai yao yaingizwe katika Bajeti hii na sheria mpya ya fedha- Wakapuuzwa

6. Viongozi wa Wafanyabiashara kupitia kamati yao Maalumu iliyoundwa wakati Waziri Mkuu alipofika Kariakoo iliwajulisha wafanya biashaara wenzao kuwa hoja zao zote 27 zimetupiliwa mbali.

7. Katika hoja zao 27 za awali,Wafanyabiashara wanahoja za haraka 7 zikifanyiwa kazi watafungua Maduka yao wakati wanasubiri serikali wafanyie kazi hizo 20.

8. Hoja hizo ni
  1. Kupunguza faini ya kuto toa risiti ambayo kwa sasa ni 15M
  2. Kuondoa service levy.
  3. Kamtakamata ya TRA mitaani
  4. Kunyan'ganywa kwa VAT baadhi ya wafanya biashara
  5. VAT kukusanywa bandarini,airport na ktk Mipaka
  6. Kuzuia wachina na Wageni ktk biashara ndogondogo Kariakoo
  7. VAT ianze Tsh millioni 500 hadi Tsh billioni 1 badala ya sasa ya Tsh million 200

9. Leo saa 7: 00 mchana, Dodoma, Waziri wa fedha na Waziri wa viwanda na biashara wamekutana na viongozi wa wafanya biashara(Mrejesho utaletwa hapa hapa).

Msimamo wa wafanyabishara ni kwamba hawataki kusikia lolote kutoka kwa Mawaziri hao baada ya kuongopewa kwa muda mrefu

10. WANATAKA RAIS AENDE KARIAKOO au KAULI YA RAIS KUHUSU HOJA ZAO

Pia soma:
News Alert: - Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024

Soma:Chalamila awasili Kariakoo awaambia Wafanyabiashara “Fungueni maduka, Biashara sio Siasa”

Soma: Chalamila: Kama Serikali inatuma vikosi kupigana Congo, inashindwa kuja kupigana Kariakoo?
Soma: Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam umenikuna sana leo sakata la wafanyabiashara Kariakoo
 
1. Kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao zaidi ya 10 na mamlaka ya mapato TRA ,hawakupata majibu.

2.kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao na serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Ilala wakiomba Waziri wa fedha afike kuwa sikiliza lakini Waziri wa fedha hakuwahi kwenda.

3.Mkuu wa Wilaya ya Ilala amepambana sana kuhakikisha mgomo hautokei (Wafanyabiashara wanampongeza) Mkuu wa wilaya ya ilala akaomba Wafanyabiashara wasubiri mwezi mmoja ,ili awasiliane na Viongozi wake kwanza

Mwezi ukaisha Mkuu wa Wilaya akapuuzwa na viongozi wake wa Juu.

4. Mkuu wa Mkoa mara zote hizi hakuwahi kuonekana katika vikao chochote cha Wafanyabiashara, wala hakuwahi kusaidia kupeleka malalamiko ngazi za Juu.

Ameonekana Jana tu, ktk Vitisho.

5. Viongozi wa Wafanyabiashara wakaomba waende Dodoma kuonana na Waziri wa fedha ili madai yao yaingizwe katika Bajeti hii na sheria mpya ya fedha- Wakapuuzwa

6. Viongozi wa Wafanyabiashara kupitia kamati yao Maalumu iliyoundwa wakati Waziri Mkuu alipofika Kariakoo iliwajulisha wafanya biashaara wenzao kuwa hoja zao zote 27 zimetupiliwa mbali.

7. Katika hoja zao 27 za awali,Wafanyabiashara wanahoja za haraka 7 zikifanyiwa kazi watafungua Maduka yao wakati wanasubiri serikali wafanyie kazi hizo 20.

8. Hoja hizo ni
  1. Kupunguza faini ya kuto toa risiti ambayo kwa sasa ni 15M
  2. Kuondoa service levy.
  3. Kamtakamata ya TRA mitaani
  4. Kunyan'ganywa kwa VAT baadhi ya wafanya biashara
  5. VAT kukusanywa bandarini,airport na ktk Mipaka
  6. Kuzuia wachina na Wageni ktk biashara ndogondogo Kariakoo
  7. VAT ianze Tsh millioni 500 hadi Tsh billioni 1 badala ya sasa ya Tsh million 200

9. Leo saa 7: 00 mchana, Dodoma, Waziri wa fedha na Waziri wa viwanda na biashara wamekutana na viongozi wa wafanya biashara(Mrejesho utaletwa hapa hapa).

Msimamo wa wafanyabishara ni kwamba hawataki kusikia lolote kutoka kwa Mawaziri hao baada ya kuongopewa kwa muda mrefu

10. WANATAKA RAIS AENDE KARIAKOO au KAULI YA RAIS KUHUSU HOJA ZAO

Pia soma:
News Alert: - Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024
Hii ya kupunguza adhabuu yakutoto rist za EFD sikubalini nayo.Nadhani kutoa risit ni wajibu wa Kila mtu amayefanya biashara
 
1. Dawa ya hii ni kutoa risiti. Ukitoa risiti hata faini ikiwa 1b haitakuhusu.
2.Naunga mkono hoja
3.Kamatakamata ya nini? Kwanini? Kukamata mizigo ya magendo au isiyolipiwa kodi ni kawaida. Labda watuambie wanakamatwa bila sababu.
4.Kunyang'anywa VAT? Sheria inasemaje? Kwani Kariakoo wengi si hawataku kulipa VAT?
5.Nani aliwaambia bandarini,airport na kwenye mipaka hawakusanyi VAT? Ukileta mzigo unatozwa vat, ukiuza mzigo unamtoza mteja vat halafu unatoa VAT uliolipa wewe inayobaki unapeleka TRA.
6.Naunga mkono hoja, mgeni hawezi kuja kuuza kandambili au karanga Kariakoo.
7.Aisee 500m mbali anyway hii wataalam wa uchumi wakaliangalie.
 
1. Kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao zaidi ya 10 na mamlaka ya mapato TRA ,hawakupata majibu.

2.kabla ya mgomo Wafanyabiashara wamekaa vikao na serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Ilala wakiomba Waziri wa fedha afike kuwa sikiliza lakini Waziri wa fedha hakuwahi kwenda.

3.Mkuu wa Wilaya ya Ilala amepambana sana kuhakikisha mgomo hautokei (Wafanyabiashara wanampongeza) Mkuu wa wilaya ya ilala akaomba Wafanyabiashara wasubiri mwezi mmoja ,ili awasiliane na Viongozi wake kwanza

Mwezi ukaisha Mkuu wa Wilaya akapuuzwa na viongozi wake wa Juu.

4. Mkuu wa Mkoa mara zote hizi hakuwahi kuonekana katika vikao chochote cha Wafanyabiashara, wala hakuwahi kusaidia kupeleka malalamiko ngazi za Juu.

Ameonekana Jana tu, ktk Vitisho.

5. Viongozi wa Wafanyabiashara wakaomba waende Dodoma kuonana na Waziri wa fedha ili madai yao yaingizwe katika Bajeti hii na sheria mpya ya fedha- Wakapuuzwa

6. Viongozi wa Wafanyabiashara kupitia kamati yao Maalumu iliyoundwa wakati Waziri Mkuu alipofika Kariakoo iliwajulisha wafanya biashaara wenzao kuwa hoja zao zote 27 zimetupiliwa mbali.

7. Katika hoja zao 27 za awali,Wafanyabiashara wanahoja za haraka 7 zikifanyiwa kazi watafungua Maduka yao wakati wanasubiri serikali wafanyie kazi hizo 20.

8. Hoja hizo ni
  1. Kupunguza faini ya kuto toa risiti ambayo kwa sasa ni 15M
  2. Kuondoa service levy.
  3. Kamtakamata ya TRA mitaani
  4. Kunyan'ganywa kwa VAT baadhi ya wafanya biashara
  5. VAT kukusanywa bandarini,airport na ktk Mipaka
  6. Kuzuia wachina na Wageni ktk biashara ndogondogo Kariakoo
  7. VAT ianze Tsh millioni 500 hadi Tsh billioni 1 badala ya sasa ya Tsh million 200

9. Leo saa 7: 00 mchana, Dodoma, Waziri wa fedha na Waziri wa viwanda na biashara wamekutana na viongozi wa wafanya biashara(Mrejesho utaletwa hapa hapa).

Msimamo wa wafanyabishara ni kwamba hawataki kusikia lolote kutoka kwa Mawaziri hao baada ya kuongopewa kwa muda mrefu

10. WANATAKA RAIS AENDE KARIAKOO au KAULI YA RAIS KUHUSU HOJA ZAO

Pia soma:
News Alert: - Mgomo wa Wafanyabiashara: Biashara zafungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024

Soma:Chalamila awasili Kariakoo awaambia Wafanyabiashara “Fungueni maduka, Biashara sio Siasa”

Soma: Chalamila: Kama Serikali inatuma vikosi kupigana Congo, inashindwa kuja kupigana Kariakoo?
Mimi siyo mfanyabiashara zote isipokuwa namba 7 hazina mashiko. Hususan hiyo hoja namba moja ingwekwa chini kabisa na hoja namba 7 ndo iwe ya kwanza hapo ingeoneonekana kweli kuna hoja za msingi.
Ila hiyo namba moja inatosha kusema kwamba tuna safari ndefu na inaharibu image ya wafanyabiashara kwamba siyo waaminifu kama kweli wao ndo wametoa hizo hoja
 
Kwa hiyo waziri alikua busy sana 🤣🤣🤣hata mda wa kuwasikiliza wafanya biashara hana ila yanga ikicheza anacheki game 🤣🤣🤣.Nchi ngumu sana hii kumbe chala boy hakuenda hata siku moja kuwasikiliza wafanya biashara leo anataka aite jeshi.Mama yetu sisi wananchi tunajua unania njema sana ila kuna watu huku chini wanakupaka mavi na ukikutana nao wanakusifu kinafiki hao malizana nao kimya kimya wanasababisha migomo uonekane hufai.
 
1. Dawa ya hii ni kutoa risiti. Ukitoa risiti hata faini ikiwa 1b haitakuhusu.
2.Naunga mkono hoja
3.Kamatakamata ya nini? Kwanini? Kukamata mizigo ya magendo au isiyolipiwa kodi ni kawaida. Labda watuambie wanakamatwa bila sababu.
4.Kunyang'anywa VAT? Sheria inasemaje? Kwani Kariakoo wengi si hawataku kulipa VAT?
5.Nani aliwaambia bandarini,airport na kwenye mipaka hawakusanyi VAT? Ukileta mzigo unatozwa vat, ukiuza mzigo unamtoza mteja vat halafu unatoa VAT uliolipa wewe inayobaki unapeleka TRA.
6.Naunga mkono hoja, mgeni hawezi kuja kuuza kandambili au karanga Kariakoo.
7.Aisee 500m mbali anyway hii wataalam wa uchumi wakaliangalie.
1. Kwa nini hawataki kutoa risiti? Hili ndilo tatizo linalotakiwa kufanyiwa kazi. Pia faini ya mil 15 ni unrealistic na inasababisha TRA kutumia kipengele hiki kupiga fedha.
Kwa kifupi Tanzania tuna matatizo haya kwenye kodi.
1. Kodi nyingi, za gharama ya juu na zisizo na formula maalumu ya utozaji. Hili linaacha mwanya wa usumbufu na rushwa
2. Pamoja na haya, kodi ingekuwa inaonekana inachofanya kwa nchi yetu watu wangeweza kuvumilia. Fikiria mtu unakamulia kodi kubwa kama hii halafu unakuja kuona malaya anajifanya ni msanii anapanda ndege na rais kwenda kula raha wakati wa ruhusa.
 
Kwa hiyo waziri alikua busy sana 🤣🤣🤣hata mda wa kuwasikiliza wafanya biashara hana ila yanga ikicheza anacheki game 🤣🤣🤣.Nchi ngumu sana hii kumbe chala boy hakuenda hata siku moja kuwasikiliza wafanya biashara leo anataka aite jeshi.Mama yetu sisi wananchi tunajua unania njema sana ila kuna watu huku chini wanakupaka mavi na ukikutana nao wanakusifu kinafiki hao malizana nao kimya kimya wanasababisha migomo uonekane hufai.
WAZIRI yupo busy na usajili wa timu yake pendwa
 
1. Kwa nini hawataki kutoa risiti? Hili ndilo tatizo linalotakiwa kufanyiwa kazi. Pia faini ya mil 15 ni unrealistic na inasababisha TRA kutumia kipengele hiki kupiga fedha.
Kwa kifupi Tanzania tuna matatizo haya kwenye kodi.
1. Kodi nyingi, za gharama ya juu na zisizo na formula maalumu ya utozaji. Hili linaacha mwanya wa usumbufu na rushwa
2. Pamoja na haya, kodi ingekuwa inaonekana inachofanya kwa nchi yetu watu wangeweza kuvumilia. Fikiria mtu unakamulia kodi kubwa kama hii halafu unakuja kuona malaya anajifanya ni msanii anapanda ndege na rais kwenda kula raha wakati wa ruhusa.
Wao ndio wajibu kwanini hawataki kutoa risiti. Kutoa risiti ipo kisheria sio mapenzi ya mtu.
 
Wao ndio wajibu kwanini hawataki kutoa risiti. Kutoa risiti ipo kisheria sio mapenzi ya mtu.
Mbona inajulikana? Hawatoi kwa sababu wanasema kodi ni kubwa. Ndiyo maana nikasema serikali inatakiwa kukaa pamoja nao iwasikilize. Hili nitatizo la siku nyingi mno ila tu serikali haijawahi kulishughulikia. Kama inaona kodi ni reasonable basi ingekaa nao na iwaambie moja kwa moja. NB: hili la risiti kwa mtu yeyote aliyewahi kufanya biashara analijua.
 
Mbona inajulikana? Hawatoi kwa sababu wanasema kodi ni kubwa. Ndiyo maana nikasema serikali inatakiwa kukaa pamoja nao iwasikilize. Hili nitatizo la siku nyingi mno ila tu serikali haijawahi kulishughulikia. Kama inaona kodi ni reasonable basi ingekaa nao na iwaambie moja kwa moja. NB: hili la risiti kwa mtu yeyote aliyewahi kufanya biashara analijua.
Vat ni 18% kubwa ilitakiwa iwe ngapi? Na kwanini ni Kariakoo tu? Wao ndio wafanyabiashara pekee nchi hii? Nasikitika kusema hoja zao karibu zote hazina mashiko. Wajipange na hoja za maana. Ni aibu eti mfanyabiashara ana negotiate fine ya kutotoa risiti. Seriously? Unatakiwa kutoa risiti sio uombe faini ndogo ya kutotoa risiti, it's a joke.
 
Sababu tra wanaangalia mauzo hawaangalii faida uliyoingiza kadri unavoandika risit nyingi ndivo mapato yako yanapanda, mfano mimi biashara yangu nikiuza 100,000 faida ni 4,000 tra wao wanahesabu umeuza 100,000 kumbe pale umepata 4000 tu
Reasoning ya wafanyabiashara wetu inachekesha.
 
Back
Top Bottom