KERO Wanachowafanyia HESLB wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu siyoo uungwana kabisa

KERO Wanachowafanyia HESLB wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu siyoo uungwana kabisa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kila baada ya siku 60 mnufaika wa mkopo wa bodi ya mikopo HESLB inabidi apewe pesa ya kujikimu na chakula shilingi 10,000 kwa siku lakini mpaka leo naandika uzi huu hakuna mwanafunzi hata mmoja Tanzania aliyeingiziwa pesa ya Boom ilihali malipo vyuoni yaani Disbursement imewanyika takribani wiki tatu zilizopita na hakuna taarifa yoyote kutoka bodi inayosema lini boom litaingia

Hali hii inapelekea kuleta taharuki vyuoni chuo kikuu Ardhi na chuo kikuu Dar es saalam kuna vuguvugu la mgomo wa kushinikiza malipo siku ya kesho kutokea.

Mbali na hilo wanafunzi wa kike wanakosa pesa ya kujikimu wanajiuza sana ubungo riverside.

Bodi ya mikopo itoe hata taarifa shida nini vyuo vingi vimeshapita siku 60 za masomo.

Mfano chuo kikuu ardhi leo ni siku ya 92
 
Ma loan officer wa vyuoni kwenu ndiyo wahuni si mpaka wapandishe cheque kwenye account zenu
 
Udsm siku hizi hamgomi!!!! Revolution square mmepafanya sehemu ya kumpiga selfie tu! Kweli nyakati zinabadilika.
 
Back
Top Bottom