Wanafunzi kufukuzwa kusoma somo la chemistry ilhali wamepata grade "C na D"

Wanafunzi kufukuzwa kusoma somo la chemistry ilhali wamepata grade "C na D"

Ungeandika kwa utaratibu. Labda anaoufanya ni mchujo wa kuwapata wanafunzi wanaozingatia anachofundisha na kufaulu. Hapo ni kumsaidia mwanafunzi kumtua mzigo ambao hakuwa anauweza.
Sahivi hakuna opt ya masomo, wanasoma yote hadi 4m 4.
Sasa yeye anawatoaje?
 
Ni Kawaida kwa shule nyingi kuweka wastani kwenye masomo complicated kupunguza miswaki hapo baadaye mtihani wa taifa.
Wanaojitoa kusoma basi wasome bila kubabaisha..wavivu wavivu wapambane na masomo Saba yaliyobakia.
Lakini si walifuta mfumo wa opt kwa wanafunzi? Au opt imerudishwa tena?
 
Kwa elimu ya sasa wacha watu wasome tu jamani.

Hizo D za chemistry na Bios. Zitamsaidia kusoma course ya afya ambayo itampa Maisha baadae.

So kuwa na wanafunzi wachache sio kigezo cha kufundisha na wakaelewa
Dah ila hii elimu aisee yani unakuja kutibiwa na dokta ambae ata wewe biology unaijua kushinda yy.. mtu ana D ya biology af anakua daktari aisee
 
katika shule ya secondary Kanoge iliyopo wilayani Nsimbo mkoani KATAVI Kuna tatizo la mwalimu wa somo la chemistry kuwatoa wanafuzi kwenye somo analofundisha akidai yeye anahitaji wanafunz atakao wafu Disha table teach mfano wanafunz WALIOPO kidato Cha nne mwaka 2024 hawafiki hata15 wengi wao aliwaondoa kwenye somo Hilo Bada ya kuwapa mtihani walipo kua kidato Cha tatu wote waliopata grade C na D aliwafukuza pia Kwa waliomaliza kidato Cha nne mwaka 2023 wapi aliowatoa hali kama hii inakatisha ndoto za wanafunz wengi wenye malengo ya kusoma masomo ya sayansi
Huyo mwalimu apewe zawadi kama mwanafunzi anapata D form two itakuaje form four?
 
Lakini si walifuta mfumo wa opt kwa wanafunzi? Au opt imerudishwa tena?
Kama walifuta ni kisiasa
Lakini ukienda shule ukaendekeza ukilaza unafutwa kwenye hayo masomo.

Unataka kusoma sayansi pambana ufaulu.
Sisi mtihani wa form 2 ndio ulikuwa wa mchujo, matokeo yako yataamua wewe uende arts , sayansi au biashara.

Hakuna cha kuchagua wakati umefeli..wenye uhuru wa kuchagua ni wale waliofaulu hayo masomo yote, ndio waliopewa option ya kuchagua waende Biashara au Sayansi.
Nje na hapo ni arts .. walimu wanapunguza idadi ya miswaki hapo baadaye.
 
Hahaha! Mwanafunzi aliyepata C na D 'standadised' anaomba huruma ya Waziri wa Elimu ili asome chumba kimoja na waliopata A.
 
Kwanza Ni aibu mzazi kuhoji sh Elfu 5 kwa mwezi ajili ya masomo ya ziada kwa ajili ya mwanao, Tena anaesoma masomo ya sayansi, Tena shule hizi za elimu bure, ticha mmoja wanafunzi mamia darasani.

Enzi zetu tulikua tunalipia kwa topic, Tena mitaani na ukimwambia mzazi hata hakuulizi Mara mbili mbili ili usilete visingizio vyako Siku ukifeli, maana kifuatacho Ni stick Kwenda mbele.

Sasa mwanao unataka afaulu afu ata kutoa motisha ya elfu 5 kwa mwalimu wake akufundishie mwanao vzur unahisi Kama unatapeliwa.

Hivi wazazi Kama nyie Ni mnajielewa kweli?
Wazazi wanaonaga fahari mtoto anaposoma sayansi, kuna dingi mmoja aliwaghasi walimu, na anajitapa kijiweni kuwa mtoto wake ameruhusiwa kusoma sayansi, kumbe dogo alipata B moja tu ya Kiswahili, huko kwingine ni bendera
 
Kumtoa mwanafunzi kusoma somo flani haliyakuwa yeye anapenda kusoma sio sawa hasa kwa hao ambao wanapata grade C na sijajua anatumia muda gani kusema huyu hafai kusoma somo hili (Idadi ya mitihani). Kwenye mitihani kuna mambo mengi huwenda huo ulikuwa mgumu kwake ndio akapata hivyo

Na muda mwingine unakuta ni kutokujielewa kwa mwanafunzi (Utoto mwingi) ila huko mbeleni anakuja kuwa serious na masomo na atafaulu vizuri tu

Mimi ni mfano halisi kabisa. Nilipokuwa vidato vya chini form 1&2 ufaulu wangu ulikuwa wa kawaida tu though sikuwahi kutoka top 10, form 3&4 nilijitambua nikawa serious na masomo nikawa sitoki top 3 na advance nikasoma science. Sasa kama mwalimu angenitoa kutokana na ufaulu wangu wa 1&2 option ambayo nilikuwa nayo ingekuwa ni masomo ya Arts pekee
 
Mtoto Kutaka kusoma asicho na uwezo nacho kisa tu anakipenda nao Ni ujinga mwngine, Mtoto asome anachokimudu.

Kama angekua anakipenda Basi angejibidiisha kukisoma na angefaulu Kama wengine ili kusiwe na longolongo.

Ningekua wewe,
Ningemuuliza mtt sababu za kufeli na anajua mwalimu keshaweka standard zake anazopaswa kuzipass ili kusoma sayansi. Na sio kumlaumu ticha.
Kwanza mtoto akipata D au C huyo hajafeli, hata kwenye cheti ukipata D huandikiwi FAIL unaandikiwa PASS!

Pili kufail kuna mengi sio lazima kwamba mtu alikua hasomi!

Mtoto aachiwe asome kama anapenda.
 
Mwalimu hayupo sahihi maana ufaulu Wa C ni ufaulu Wa wastani unaofaa MTU kuendelea na hatua nyingine ya Elimu
 
Those are burden

Hutuwezi kuwa na wahudumu wa afya vilaza
 
Sasa Chemistry ya Form 2 mwanafunzi anapata D, mimi naona ni sawa tu kwa mwalimu kumkataza mwanafunzi wa hivyo kuendelea na hilo somo, maana utakua ni mzigo tu kwa mwanafunzi, bora akomae na masomo mengine anayoyaweza zaidi.

Chemistry ya Form 2 ukipata D, most likely hapo form 3 itamtesa sana sana, na form 4 ataishia tu kupata F au akikomaa sana hiyo hiyo D. Mwalimu anafanya hivyo kwa faida ya wanafunzi, wazazi acheni kulazimishia watoto wasome masomo ambayo yanawakimbiza, na muwe waelewa msipende kulazimisha mambo.
Unafahamu kwamba mwanafunzi form four akipata
Physics D
Chemistry D
Biology D
Math D

Anadahiliwa kozi ya afya,

Huyo mwalimu aiachie NECTA mamlaka ya ku grade wanafunzi
 
Mwanafunzi pekee ndio mwenye maamuzi ya kusoma au kutosoma
Si kazi yake mwalimu kuamua Nani asome!
Hata Kama Mwanafunzi amepata F form two, ni haki yake kuamua asome chemistry au aache,
Hizo geography, Biology na maths wanafunzi wanapata F na wanaendelea kusoma

Unamwamuliaje Mwanafunzi, mustakabali wake?
Unaijua hatima ya maisha yake mbeleni?

Waalimu wajue kuwa shule sio zao, maabara sio zao, maburette, mahydrochloric sio zao, Ni za serikali kwa Kodi za wazazi wa hao anaowakataa,

Mtoto amepata C, D form two, anataka kuendelea kupambania kombe yeye anamzuia kwa mamlaka gani? Kwa muongozo gani?

Mwalimu Bora Ni yule anayemwezesha kilaza kuperform kwa kutumia mbinu mbalimbali za ufundishaji

Mwalimu huyohuyo, ameshasahau alipata chemistry C form four, chemistry D form six, na alipata sup ya kozi ya chemistry kule DUCE

Hizo D, vijana wetu zinawasaidia kwenda kusomea ufugaji wa kuku na wakaanzisha ufugaji kujikimu na maisha

Waalimu wanajifanyaga ndio wafalme wa shule, ndio watunga sera za Elimu wakati wao ni watekelezaji wa sera tu

Watunga sera wametoa option kwa Mwanafunzi, na si kwa mwalimu,
Kazi ya mwalimu Ni kufundisha tu!

Waalimu hawapendi kufuata miongozo ktk uendeshaji wa shule, ndio maana serikali itasema wanafunzi warudi likizo, wao wanasema hapana wasirudi likizo

Serikali itasema bakora ni fimbo tatu, wao ni bakora za mvua tena za changizo waalimu wote staff
 
Mwanafunzi pekee ndio mwenye maamuzi ya kusoma au kutosoma
Si kazi yake mwalimu kuamua Nani asome!
Hata Kama Mwanafunzi amepata F form two, ni haki yake kuamua asome chemistry au aache,
Hizo geography, Biology na maths wanafunzi wanapata F na wanaendelea kusoma

Unamwamuliaje Mwanafunzi, mustakabali wake?
Unaijua hatima ya maisha yake mbeleni?

Waalimu wajue kuwa shule sio zao, maabara sio zao, maburette, mahydrochloric sio zao, Ni za serikali kwa Kodi za wazazi wa hao anaowakataa,

Mtoto amepata C, D form two, anataka kuendelea kupambania kombe yeye anamzuia kwa mamlaka gani? Kwa muongozo gani?

Mwalimu Bora Ni yule anayemwezesha kilaza kuperform kwa kutumia mbinu mbalimbali za ufundishaji

Mwalimu huyohuyo, ameshasahau alipata chemistry C form four, chemistry D form six, na alipata sup ya kozi ya chemistry kule DUCE

Hizo D, vijana wetu zinawasaidia kwenda kusomea ufugaji wa kuku na wakaanzisha ufugaji kujikimu na maisha

Waalimu wanajifanyaga ndio wafalme wa shule, ndio watunga sera za Elimu wakati wao ni watekelezaji wa sera tu

Watunga sera wametoa option kwa Mwanafunzi, na si kwa mwalimu,
Kazi ya mwalimu Ni kufundisha tu!

Waalimu hawapendi kufuata miongozo ktk uendeshaji wa shule, ndio maana serikali itasema wanafunzi warudi likizo, wao wanasema hapana wasirudi likizo

Serikali itasema bakora ni fimbo tatu, wao ni bakora za mvua tena za changizo waalimu wote staff
[emoji706][emoji706][emoji706][emoji706]
 
Mshahara mkia wa mbuzi Sina posho,, nafundisha kadri ninavyo lipwa
 
Yupo sahihi sasa C and D za nini? Nenda kasome history huko.
Tumieni busara.
Kuna watu walipata D form two wakaja kupata C Hadi A firm four kwenye SoMo hilo hilo.
Kuna mabadiliko, pia D inaweza kumsaidia kigezo cha chini cha kusoma kozi flani elimu ya juu.
 
Nchi hii ina wazazi/walezi wapumbavu sana, mtu anashindwa kumpambania mtoto wake halafu ankuja kulialia mitandaoni kwa kubebesha watu lawama.

Hivi unadhani PHY/CHEM ni fuvu kila mmoja analo?.

Kusoma masomo hayo kunahitaji mtoto mwenye IQ kubwa ambaye yuko tayari kujibidisha.

Mimi sio mwalimu lakini nimebobea kiasi kwenye moja ya masomo ya sayansi, hivyo ninaelewa uzito wa hayo masomo kuanzia O-level hadi University.

Mwalimu hawezi kuwa na uchungu wa kuhangaika na mwanao uliyemtelekeza mithili ya kuku wa kienyeji, unaona shida kutoa elfu 5 mwanao asome tuition ili kumuongezea uelewa halafu unakuja kumlaumu tu mwalimu.

Umeona elimu ni gharama bakini na ujinga wenu, pia mchuma janga hula na wakwao

Wengine familia ziliuza vingi ili kututengenezea mazingira ya kumudu hayo masomo ila nyie mmekaza fuvu kutafuta lawama kwa serikali na waalimu kwenye vitu mnavyopaswa kuwajibika wenyewe moja kwa moja.

Cc DeepPond
 
Sasa Chemistry ya Form 2 mwanafunzi anapata D, mimi naona ni sawa tu kwa mwalimu kumkataza mwanafunzi wa hivyo kuendelea na hilo somo, maana utakua ni mzigo tu kwa mwanafunzi, bora akomae na masomo mengine anayoyaweza zaidi.

Chemistry ya Form 2 ukipata D, most likely hapo form 3 itamtesa sana sana, na form 4 ataishia tu kupata F au akikomaa sana hiyo hiyo D. Mwalimu anafanya hivyo kwa faida ya wanafunzi, wazazi acheni kulazimishia watoto wasome masomo ambayo yanawakimbiza, na muwe waelewa msipende kulazimisha mambo.
Acha ujinga ww nina mfano halisi kwamba watu wanabadilika, kuna dem nimesoma nae tulipokuwa form one na form two hakuwa vizur ktk masomo ya sayansi. Alikua anapata D ni rafiki yang kabisa ila tulipoingia form 3 alikuja tofauti kabisa alibadilika akawa Ana faulu kushinda mpaka kina john kisomo na necta alipata physics C,bio A , chemistry B,Math D.
 
Back
Top Bottom