Wanafunzi kufukuzwa kusoma somo la chemistry ilhali wamepata grade "C na D"

Wanafunzi kufukuzwa kusoma somo la chemistry ilhali wamepata grade "C na D"

Nchi hii ina wazazi/walezi wapumbavu sana, mtu anashindwa kumpambania mtoto wake halafu ankuja kulialia mitandaoni kwa kubebesha watu lawama.

Hivi unadhani PHY/CHEM ni fuvu kila mmoja analo?.

Kusoma masomo hayo kunahitaji mtoto mwenye IQ kubwa ambaye yuko tayari kujibidisha.

Mimi sio mwalimu lakini nimebobea kiasi kwenye moja ya masomo ya sayansi, hivyo ninaelewa uzito wa hayo masomo kuanzia O-level hadi University.

Mwalimu hawezi kuwa na uchungu wa kuhangaika na mwanao uliyemtelekeza mithili ya kuku wa kienyeji, unaona shida kutoa elfu 5 mwanao asome tuition ili kumuongezea uelewa halafu unakuja kumlaumu tu mwalimu.

Umeona elimu ni gharama bakini na ujinga wenu, pia mchuma janga hula na wakwao

Wengine familia ziliuza vingi ili kututengenezea mazingira ya kumudu hayo masomo ila nyie mmekaza fuvu kutafuta lawama kwa serikali na waalimu kwenye vitu mnavyopaswa kuwajibika wenyewe moja kwa moja.

Cc DeepPond
Hivi wale wanaoingia form iii wana c moja ya kiswahili masomo mengine F nao wafukuzwe kwenye hayo masomo au!

Sera inasema mwanafunzi atachagua, wala haijasema awe amepata grade ipi

Kazi ya mwalimu ni kufundisha sio kuchagulia watoto kitu cha kusoma, hiyo ni kazi ya watu wengine

Huyo mtoto akipata F, cheti chenye F kitakua ni cha huyo mtoto sio mwalimu
 
Ni Kawaida kwa shule nyingi kuweka wastani kwenye masomo complicated kupunguza miswaki hapo baadaye mtihani wa taifa.
Wanaojitoa kusoma basi wasome bila kubabaisha..wavivu wavivu wapambane na masomo Saba yaliyobakia.
Mwalimu Yuko sahihi
Masomo ya sayansi hayataki kilaza

Ndio maana Shule za katoliki hawataki huo ujinga

Wastani huo haukubaliki akasome kokote combination za HGL au HGK na course zozote zenye History mbele sayansi akae nazo mbali kilaza huyo

Shule za kanisa katoliki kufaulisha sana masomo ya sayansi Huwa wako so strict no nonsense mtu kuingia kusoma masomo ya sayansi wanachuja hasa hawataki mtu mwenye akili za kuunga unga tu utaondoka na C Yako sio Chemistry tu hata iwe fizikia ,au biology au Hisabati
 
Option zipo, kuna biashara, kompyuta (kwa baadhi ya shule), science (hawa wanapiga Physics na Chemistry) na wengine wengi hujichagulia sub-science (kwa kuacha Physics)
Oooh kumbe, hapo kat ilikua no option. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kama walifuta ni kisiasa
Lakini ukienda shule ukaendekeza ukilaza unafutwa kwenye hayo masomo.

Unataka kusoma sayansi pambana ufaulu.
Sisi mtihani wa form 2 ndio ulikuwa wa mchujo, matokeo yako yataamua wewe uende arts , sayansi au biashara.

Hakuna cha kuchagua wakati umefeli..wenye uhuru wa kuchagua ni wale waliofaulu hayo masomo yote, ndio waliopewa option ya kuchagua waende Biashara au Sayansi.
Nje na hapo ni arts .. walimu wanapunguza idadi ya miswaki hapo baadaye.
Hapo kati walifuta, labda wamerejesha upyaa.
 
Naomba wadau wa Jamiiforums waweze kufatilia uovu unaofanywa na mwalimu mmoja katika shule ya secondary Kanoge ambayo ipo wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kwani katika shule hiyo kuna mwalimu wa somo la Chemistry pia ni mwalimu wa nidhamu.

Ana tabia ya kukataza wanafunzi wasisome somo la Chemistry akidai anahitaji wanafunzi wachache anaweza kuwafundisha table teach maana ukianglia Kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2024 hata 15 hawafiki wengi aliwatoa kwenye somo hilo kisa wamepata wastani wa "C na D".

Kwenye somo hilo pia hata wanafunzi waliomaliza kidato cha nne 2023 aliwafukuza kwenye somo lake, kuwarudisha aliwambia hao aliwafukuza kila mmoja alipe elfu5 ndo arudi.

Sasa naomba waziri wa elimu , afisa elimu mkoa na wilaya, mkuu wa mkoa , na wilaya waweze kulishughlikia swala hilo mana kuna wanafunzi wana ndoto ya kusoma masomo ya sayansi lakini mwalimu huyo anakatisha ndoto zako kwa interest zake binafsi.
Wewe ulipaswa ufukuzwe na shule kabisa. Mnapoteza tu ada za wazazi wenu akili hamna na hamwelewi. Hujui hata kupangilia hoja na umemaliza darasa la 4.
 
Back
Top Bottom