Wanafunzi wa Kimarekani Wakiendesha Mdahalo wa Urais wa Tanzania kwa Kiswahili

Wanafunzi wa Kimarekani Wakiendesha Mdahalo wa Urais wa Tanzania kwa Kiswahili

Kashishi

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2010
Posts
1,142
Reaction score
635
Wana JF, tazameni hiyo video muone jinsi wanafunzi wa Kimarekani wanaosomea lugha ya kiswahili huko Chuo Kikuu Cha Indiana (Bloomington Campus) wakiendesha mdahalo wa Wagombea Urais wa Tanzania kwa kuchambua hoja mbalimbali ambazo ni kipaumbele na changamoto zinazozikabili taifa. Wako mstari wa mbele katika kukuza na kuenzi lugha ya Kiswahili.

Published on Jun 30, 2013

 
Last edited by a moderator:
Nimecheka sana, ila kura yangu nitampa huyu mwanadada-bei ya mafuta haiwezi kushuka lililo muhimu ni kuboresha usafiri wa umma ili kupunguza matumizi ya magari binafsi (ambapo ni wazi mahitaji ya mafuta yatapungua). Hahahaha
 
Hawa ndio watakaokuja kuwa agents wa akina symbion power, wanazidi kuandlaiwa
 
+wanaionyesha dunia jinsi tanzania ilivyo na viongozi ambao akili hawatumii mpaka wakisha staafu wanazitumia kuwashauri walio madarakani.
 
Hawa ndio watakaokuja kuwa agents wa akina symbion power, wanazidi kuandlaiwa

Ni kweli kabisa. Hao wakisha hitimu Chuo tu wanakuwa recruited na CIA pamoja na vyombo vingine vya usalama wa nchi yao kama Majasusi. Halafu baadae wanaletwa Bongo au Kenya au DRC Mashariki huko ku volunteer mwaka mmoja chini ya mwamvuli wa ile programu yao inayojulikana kama 'Peace Corp". Unakuta mtu ametupwa Kigoma huko ati Bwana Shamba au Muheza huko eti Mwalimu.

Na wawapo Bongo kwenye hizo mishineni zao ndio wanapata fursa ya kunoa vema (polish) 'Kiswahili' chao kuwa barabara. Baadae kulitumikia taifa lao kwa muda wanakuja kuzuka kivingine (Staili ya kutengeneza kampuni hivi yenye mkono wa serikali yao) kama akina Symbion au Winds Energy dezaini hivi. Na si kiswahili peke yake bali ni lugha zote duniani.
 
natamani wapate nyuzi hizi wazisome wajue tunawafikiriaje. wajue kuwa na sisi tunajua wakija tutapambana nao vipi,

Ingawa wanafursa nzur zaidi, akitaka kuja kufnya mazoezi kwa vitendo huku gharama ni ndogo kwa kuwa maisha ni mepesi bongo ktk maana ya dola yao.

Serikali yao inashawishi weusi maana watakuwa kama sisi hata wakija kwenye mission zao
 
Hii inadhihirisha wazi kabisa kuwa palipo au panapotumika lugha ya kiswahili katika Afrika, kwa mfano Tanzania,Kenya, Uganda,Rwanda,Burundi na Kongo kuna hazina kubwa ya mali ambayo mataifa makubwa yanataka kuichukua kwa maslahi yao! Hivyo basi ili mali itoke kirahisi mataifa hayo hayana budi kuwa kama wenye mali! Mfano mzuri tumeuona kwa wachina wamevamia kila sehemu! Waswahili wanasema,"Ukienda kwa wenye chongo,nawe yakupasa kuwa chongo."
 
Hawa ni wanafunzi wa Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Indiana kilichopo Bloomington, Indiana nchini Marekani. Hapa, wanaigiza (kwa Kiswahili), mdahalo wa urais Tanzania.

Nisiseme mengi, wenyewe mjionee

 
Last edited by a moderator:
 
Last edited by a moderator:
Je, unajua wanafunzi hao wanafundishwa katika chuo au shule gani? Na wapi? Mimi ni mwanafunzi Mmarekani wa Kiswahili pia, na naweza kukuambia ndiyo ngumu sana kuona mwalimu wa Kiswahili hapa. Ningependa kujua zaidi kuhusu hilo darasa la Kiswahili.
 
  • Thanks
Reactions: Paw
Je, unajua wanafunzi hao wanafundishwa katika chuo au shule gani? Na wapi? Mimi ni mwanafunzi Mmarekani wa Kiswahili pia, na naweza kukuambia ndiyo ngumu sana kuona mwalimu wa Kiswahili hapa. Ningependa kujua zaidi kuhusu hilo darasa la Kiswahili.

Hapana sifahamu chuo/shule wanaposomea. Hii video nimekutana nayo tu kwenye youtube nikasema nilete jamvini wanajamvi waone lugha yetu inavyokua.
 
Back
Top Bottom