Wanafunzi wa Kisabato Wafukuzwa TEKU kwa Kukataa Kufanya Mitihani Siku ya Sabato naomba muongozo wa kisheria

Wanafunzi wa Kisabato Wafukuzwa TEKU kwa Kukataa Kufanya Mitihani Siku ya Sabato naomba muongozo wa kisheria

Nikirejea Ibara ya 19 ya Katiba yetu ya JMT ya Mwaka 1977 inatoia Uhuru wa Mtu Kuabudu.......

Hali kwa Chuo Kikuu cha Theophile Kisanji ni Tofauti kwani wanafunzi wapatao 8 wamefukuzwa Chuoni hapo kwa madai ya kutofanya mitihani iliyopangwa kufanyika siku ya Jumamosi Sabato kwamba kwa kanuni za Chuo hicho hiyo si sababu ya kumfanya mwanafunzi asifanye mitihani

Wanafunzi hao wapo mitaani kwa sasa wakisaka msaada wa kisheria


  1. Je yamkini wakati wanafunzi hao wanapokelewa hilo halikuwekwa bayana?
  2. Mbona Mitihani isiwe Jumapili?
  3. Wapi Uhuru wa Kuabudu kwa mujibu wa Katiba JMT na sheria?

Je mnawashauri nini wanajamvi?

Ninavyojua...kama dini haioni umuhimu wa elimu..eti kwa kigezo cha siku..huu ni utaahira...opeum..ile ya marx...ntarudia tena opium..enhe..then ...wasifanye pepa jumamosi...wafanye lini...hawajui kuwa hapa dunia tunaspecific limit of time to stay here on the world ..we need to usr this time we get intensively..ndo maana kwa wao no sleep every time time kwao nii bada..from alfajir mpaka...alfajr seven day..mwaka mzima...huku elimu ikiwa pembeni..reading..na kutafuta rizq till we die...mh...mh..
 
umemailizia tu vibaya lakn ulishuka vizuri
siyo kazi ya chuo kujuwa wewe ni sabato, mkristo. muislam, mpagani au la wewe unatakiwa kufuata sheria na taratibu unazozikuta pale, na unapokuwa unaaply chuoni jaribuni kusoma taratibu na mjitahidi hata kuwaulizia wenzenu walio watangulia kujuwa utaratibu wa chuo husika, siyo kuanza kuleta masuala ya ikitadi vyuoni, leo sabato, kesho masjid, keshokutwa kanisani,n.k sasa shule itapatikana kweli, sasa kama unaona huwezi kufanyakazi jumamosi unasoma ili iweje? ukiitwa kazini jumamosi kwamba kuna dharula inamaana hutaenda kuhudumia jamii, achene ujinga nyie someni kwanza
 
binafsi but public kumbuka
.......................................................................................................................................


Asante sana Maswala kwa mchango wako mzuri...nami nina ya kuongea kidogo kuhusu hili...

Ndugu zangu kwanza tuelewe kile ni chuo cha BINAFSI na sio cha serikali....hivyo basi kina taratibu zake na kanuni zake na sheria zake. Hii ina maana yeyote anayejiunga na chuo ambacho ni binafsi shurti akubaliane na kanuni, taratibu na sheria za mahali hapo...HAIWEZWKANI UENDE MAHALI SIO KWAKO HALAFU UANZISHE SHERIA ZAKO....HAIWEZEKANI.. Haina tofauti na wanafunzi wa kiislamu wanaoenda kusomea udaktari wa mifugo (akiwemo nguruwe) halafu wanagoma kumtibu au kumshika nguruwe kisa ni "haramu" kwa imani yao...HUU NI UJINGA.

Haiwezekani wewe mkristo uende ukasome au umpeleke mwanao shule za kiislamu halafu mwanao aache kuvaa hijabu...maana hizo ndizo taratibu zao...Haiwezekani wewe muislamu uende ukasome au umpeleke mwanao akasome ktk shule za seminary za kikristo aache kwenda kanisani jumapili au kuingia vipindi vya maombi kila alfajiri...NASEMA HAIWEZEKANI.

Tukianza ku-entertain haya mambo ina maanisha... kama ni mashuleni au vyuoni basi masomo yafundishwe jumatatu hadi alhamisi tu na mitihani itungwe ndani ya siku hizo tu maana Ijumaa-Waislamu, Jumamosi-Wasabato na Jumapili-RC/Protestants...Hii kitu HAIWEZEKANI. Pia hatutaishia vyuoni...tutasogea hadi makazini...na kwenye semina n.k n.k n.k...NASEMA HAIWEZEKANI.

Umekuja kunitembelea kwangu au umekuja kukaa kwangu NI LAZIMA NA SIO OMBI (LABDA MIMI NDIO NIONE HURUMA) UFUATE TARATIBU ZA NYUMBA YANGU... Sio umekuja leo kesho utarudi usiku wa manane...ukitegemea tutakufungulia mlango...kwako hapa? Vivyohivyo na hili la wasabato...kama wameona kile chuo hakitendi haki waende ktk vyuo vyao (Vya kisabato) alaa!!!
 
Suala la imani hutatuliwa kwa busara tu ,kuna vyuo vingi ambavyo vinawanafunzi wa kisabato lakini matatizo hayajitokezi mi ningeshauri chuo kiongozwe la roho wa Mungu na busara itumike kama baadhi ya vyuo ambavyo vinatoa hata room /vyumba kwa wanafunzi wa madhehebu mbali mbali kuabudu.ASANTENI
 
Aina hii ya watu ndo waliokwenda airport kusubiri ndege ya kwenda mbinguni.
 
Catholic Church imejifanya mungu mtu duniani kujiona bora kuliko wengine, kama ilivyo Ijumaa kuifanya siku ya kazi ipo siku haki itatendeka
 
Na seminarini ukila parachichi la paroko tu shule huna...Nidhamu kwanza. wewe unakwenda kwenye chuo chenye taratibu zake unataka uweke taaratibu zako? Kila mmoja akifanya hivyo kwa kisingizio cha UHURU WA KUABUDU na kwa jinsi hizi dini zinavyofumuka utajakuta hata wengine wanakataza kufanya kazi j3 je, tutafanyaje?.
Sisi bwenini ilikuwa ukila matango ya sister Huna shule
 
Suala la imani hutatuliwa kwa busara tu ,kuna vyuo vingi ambavyo vinawanafunzi wa kisabato lakini matatizo hayajitokezi mi ningeshauri chuo kiongozwe la roho wa Mungu na busara itumike kama baadhi ya vyuo ambavyo vinatoa hata room /vyumba kwa wanafunzi wa madhehebu mbali mbali kuabudu.ASANTENI
Hill ni kawaida tu Mbona hats pale chuo kikuu cha mwenge nipo moshi waliwa disco wasabato kadhaa pale kwa kukacha kufanya D's test
 
Kuna jamaa yangu ni msabato na anaishi na demu wake geto moja.linapofika swala la kufanya mitihani au presentation jumamosi alikua anagombana sana na ma doctor.siku moja nikamwambia mbona unaishi na mwanamke na mnazini huoni hiyo ni dhambi au dhambi ni kufanya kazi jumamosi?amenichukia mpaka leo.wakati mwingine haya mambo ya imani tunajichanganya sana.


Hao katika msururu wa Amri za Mungu iliyo kuu, kwao ni "kuitunza sabato"! Wamefundishwa na kusisitizwa kuwa "ukiishika" sabato hata kama uko mwizi, mseng'enyi na mzinzi basi Mbinguni badoi halali yako
 
Back
Top Bottom