Wanafunzi zaidi ya 600 wanasomea chini jijini Mwanza

Wanafunzi zaidi ya 600 wanasomea chini jijini Mwanza

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Zaidi ya wanafunzi 600 katika shule za msingi mbili za Kayenze na Chasubi zilizopo kata ya Kayenze halmashauri ya Ilemela wanasoma wakiwa chini kutokana na ukosefu wa madawati.

Aidha, changamoto nyingine inayotajwa katika shule zote mbili ni upungufu wa walimu ambapo jumla ya wanafunzi ni 3100 lakini walimu waliopo ni 25 pekee, hali inayopelekea ufundishaji kuwa mgumu na wanafunzi kukosa baadhi ya masomo kutokana na upungufu wa walimu uliopo katika shule zote mbili.

Wakati hayo yakijiri, huko Muleba nako hali si shwari. Ambapo shule ya msingi Burungura yenye wanafunzi 868 na walimu watano, inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na uhaba wa walimu hususani wa kike hali inayosababisha utoro kwa wanafunzi wa kike kwa kushindwa kuhudhuria masomo yao wakati wa hedhi.
1628422670637.png


Credit to ITV-Tanzania
 
WAZIRI WA TAMISEMI YUPO KAZI KULEMBUA NA KULIOANAPOSHO ZA VIAKO DAR BADALA YA KUFANYIA DODOMA ILI HERA ZIENDE KUPUNGUZA MATATIZO KAMA HAYO.KWANI HIZO SHULE ZINAHITAKA KAMA SH NGAPI?UTAKUATA HATA BILLION MOJA INATOSHA.


Zaidi ya wanafunzi 600 katika shule za msingi mbili za Kayenze na Chasubi zilizopo kata ya Kayenze halmashauri ya Ilemela wanasoma wakiwa chini kutokana na ukosefu wa madawati.

Aidha, changamoto nyingine inayotajwa katika shule zote mbili ni upungufu wa walimu ambapo jumla ya wanafunzi ni 3100 lakini walimu waliopo ni 25 pekee, hali inayopelekea ufundishaji kuwa mgumu na wanafunzi kukosa baadhi ya masomo kutokana na upungufu wa walimu uliopo katika shule zote mbili.

Wakati hayo yakijiri, huko Muleba nako hali si shwari. Ambapo shule ya msingi Burungura yenye wanafunzi 868 na walimu watano, inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na uhaba wa walimu hususani wa kike hali inayosababisha utoro kwa wanafunzi wa kike kwa kushindwa kuhudhuria masomo yao wakati wa hedhi.

Credit to ITV-Tanzania
 
UVCCM hizi habari hawapendi kuzisikia
Wanakuambia sasa ni muda wa MATOKEO MAKUBWA SASA!!utapataje matokeo makubwa wakati vitu vidogo vidogo kama mashimo ya vyoo, vyumba vya madarasa tu bado ni shida!!!yaani ukisikia viongozi kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa wanavyozungumzia mambo makubwa utadhania mambo madogo yote wameshayamaliza!!na kipindi cha mwenda zake ilikuwa kosa la jinai kutoa habari hizi.
 
UVCCM hizi habari hawapendi kuzisikia
Wanakuambia sasa ni muda wa MATOKEO MAKUBWA SASA!!utapataje matokeo makubwa wakati vitu vidogo vidogo kama mashimo ya vyoo, vyumba vya madarasa tu bado ni shida!!!yaani ukisikia viongozi kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa wanavyozungumzia mambo makubwa utadhania mambo madogo yote wameshayamaliza!!na kipindi cha mwenda zake ilikuwa kosa la jinai kutoa habari hizi.
 
Wanakuambia sasa ni muda wa MATOKEO MAKUBWA SASA!!utapataje matokeo makubwa wakati vitu vidogo vidogo kama mashimo ya vyoo, vyumba vya madarasa tu bado ni shida!!!yaani ukisikia viongozi kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa wanavyozungumzia mambo makubwa utadhania mambo madogo yote wameshayamaliza!!na kipindi cha mwenda zake ilikuwa kosa la jinai kutoa habari hizi.
Ukiwaambia haya watakuona wewe ni Gaidi
 
Zaidi ya wanafunzi 600 katika shule za msingi mbili za Kayenze na Chasubi zilizopo kata ya Kayenze halmashauri ya Ilemela wanasoma wakiwa chini kutokana na ukosefu wa madawati.

Aidha, changamoto nyingine inayotajwa katika shule zote mbili ni upungufu wa walimu ambapo jumla ya wanafunzi ni 3100 lakini walimu waliopo ni 25 pekee, hali inayopelekea ufundishaji kuwa mgumu na wanafunzi kukosa baadhi ya masomo kutokana na upungufu wa walimu uliopo katika shule zote mbili.

Wakati hayo yakijiri, huko Muleba nako hali si shwari. Ambapo shule ya msingi Burungura yenye wanafunzi 868 na walimu watano, inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na uhaba wa walimu hususani wa kike hali inayosababisha utoro kwa wanafunzi wa kike kwa kushindwa kuhudhuria masomo yao wakati wa hedhi.

Credit to ITV-Tanzania
Siku hizi wanaziita Satelite schools eti

Satelite School itoke wapi huko Ilemela ?
 
Wanakuambia sasa ni muda wa MATOKEO MAKUBWA SASA!!utapataje matokeo makubwa wakati vitu vidogo vidogo kama mashimo ya vyoo, vyumba vya madarasa tu bado ni shida!!!yaani ukisikia viongozi kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa wanavyozungumzia mambo makubwa utadhania mambo madogo yote wameshayamaliza!!na kipindi cha mwenda zake ilikuwa kosa la jinai kutoa habari hizi.
Bila kuboresha mazingira ya kusomea na kujifunzia MATOKEO MAKUBWA yatabaki kuwa ndoto
 
Miaka 60 ya uhuru bado

1. Wanafunzi wanakaa chini,
2. Bado kuna uhaba wa madarasa na vyoo,
3. Bado kuna uhaba wa walimu
4. Bado na bado

Miaka 60 ya uhuru
Inasikitisha sana ni kama hatuna mpango na elimu nchi hii maana kila kiongozi anayeingia haonyeshi kujali suala la elimu labda kwa kwakuwa watoto wao hawasomi shule za kidumu na mfagio!!
 
Back
Top Bottom