Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulonga huko kwenye hiyo jamhuri.

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini wasitende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
 
Twitter japo mnaiponda lakini inawakera, mnatamani isiwepo kabisa.

Hilo nimethibitisha leo kwenye hotuba ya jamaa aliposema "haki huendana na wajibu", tena akarudia mara mbili na kusisitiza nadhani nimeeleweka, hapo alikuwa anawajibu wale wasumbufu kule twitter.

Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri mkilala usiku na ndicho kinachokupata Ngabu.
 
..nadhani wanaogopa MITUTU.

..hawawaogopi Ngosha na Mambosasa.

..fuatilia sakata la madiwani wa jiji la Dsm.

..pale ulipigwa mkono, mano-a-mano.

..baada ya kupokea kichapo, madiwani wa ccm walienda kuwalilia Polisi.
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulong

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini waait etende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Holy Crap!
By Rev Masanilo.
 
Twitter japo mnaiponda lakini inawakera, mnatamani isiwepo kabisa; hilo nimethibitisha leo kwenye hotuba ya jamaa aliposema "haki huendana na wajibu", tena akarudia mara mbili na kusisitiza nadhani nimeeleweka, hapo alikuwa anawajibu wale wasumbufu kule twitter.

Sauti ya mtu huwezi kuidharau, hata mkiwepo mia moja na kati yenu akawepo mmoja anaewapinga mtamsikia tu, na atawakera pamoja na nguvu zenu, matokeo yake hamtapata usingizi mzuri usiku mkilala.
Ingia barabarani kamanda.
 
..nadhani wanaogopa MITUTU.

..hawawaogopi Ngosha na Mambosasa.

..fuatilia sakata la madiwani wa jiji la Dsm.

..pale ulipigwa mkono, mano-a-mano.

..baada ya kupokea kichapo, madiwani wa ccm walienda kuwalilia Polisi.
JokaKuu wewe ushawahi kuandamana popote pale?

Au huwa unaandamana JF tu?
 
Ni kutokuwa serious kwa waitisha maandamano. Laiti wote na famili + koo zao wangeingia barabarani tayari unazungumzia watu 100+. Wakakaa mstari wa mbele wananchi tungejitokeza.
 
Miaka minne ilopita nilitoa maoni kuwa, endapo wale jamaa wa UKUTA wangenywea na kutokufanya maandamano yao waliyokuwa wameyapania, basi huo ungekuwa ni ushindi mkubwa kwa Rais Magufuli. Si tu ushindi uonekanao kwa macho, bali ushindi wa kisaikolojia pia.

Niliandika hapa:


Maandamano hayo hayakufanyika. Rais Magufuli aliwaambia hao walokuwa wamepanga hayo maandamano kuwa yeye ‘hajaribiwi’.

Nadhani walimwelewa alichokisema.

Miaka 2 baadaye kukapangwa tena kuwe na maandamano makubwa ambayo yangefanyika siku ya muungano. Haya hayakuitishwa na chama chochote cha kisiasa. Yaliitishwa na dada’ake na Salary Slip 🤣.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani.

Mwaka huu tena vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA baada ya kushindwa uchaguzi mkuu na kudai kuwa vimefanyiwa hujuma, viongozi wake wakaitisha maandamano ya amani nchi nzima, yasiyo na kikomo, ya kupinga matokeo.

Hakuna hata mtu mmoja aliyeingia barabarani na kuthubutu kuandamana.

Huwa naona sana humu wale akina dada wa Twitter, wale wanaharakati wa Jamhuri ya Twitter, Shangazi na yule mwezake Binti Maria wakisifiwa sana wanapo longalonga huko kwenye hiyo jamhuri yao. Halafu kuna huyu raia mpya aitwaye Amsterdam. Naye naona anapenda sana kulong

Kwamba eti ni majasiri sana. Hawamwogopi mtu, blah blah blah.

Sasa, kama kweli hawamwogopi mtu na hawaogopi kitu, kwa nini sasa huwa wanaishia kupiga mayowe kwenye hiyo jamhuri yao? Kwa nini waait etende kwa vitendo hayo maneno yao kwa kuingia barabarani na mabango yao na vipaza sauti kumpinga huyo wasiyempenda?

Jibu ni moja tu: na wao wanajua kuwa huyo Ngosha hajaribiwi. Akisema kitu akiwa amekasirika huwa anamaanisha. Aliposema hajaribiwi, naamini wote walioisikia hiyo kauli, waliielewa.

Kelele zipigwazo jamhuri ya Twitter haziwezi kubadili chochote kilichopo huku uraiani.

Kauli ya Ngosha na virungu vya kamanda Mambosasa, vimewapa watu uhamisho toka Tanzania kwenda Jamhuri ya watu wa Twitter.
Na bado huko twitter tutawafuata...sijui watajifichia wapi?
 
Nyani Ngabu,

..kwanini unadhani wapinzani wa Tz ambao hawana silaha, wanaweza kukabiliana na chama tawala ambacho kina silaha?

..au kwanini unadhani Ngosha ana ubavu wakati anachofanya ni kutuma wenye silaha kupiga wasio na silaha?
Acha uoga mazee.

Huko kwingineko Mbona watu huwa wanazipiga na polisi wenye silaha...

 
Back
Top Bottom