Wanajeshi 1000 wa Korea Kaskazin wameuawa mpaka sasa. Wanakosa mbinu za Kisasa

Minjingu Jingu

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2023
Posts
1,072
Reaction score
2,384
Takriban wanajeshi 1,000 wa Korea Kaskazini wameuawa na 3,000 kujeruhiwa wakati wa vita vya Urusi dhidi ya Ukraine katika kipindi cha miezi mitatu.

Korea Kaskazini inaaminika kutuma wanajeshi 11,000 kusaidia jeshi la Urusi kuwaondoa wanajeshi wa Ukraine walioko eneo la Kursk kusini magharibi.

Wanajeshi wa Korea Kaskazini wanaripotiwa kuwa hawana mafunzo ya kutosha na wanapigana kwa mbinu za kizamani, wakiwa hatarini kushambuliwa na ndege zisizo na rubani zinazotumiwa na Ukraine.

 
mtu aliyeuliwa vitani picha mpaka ikufikie wewe za kazi gani? huwezi kufurahia habari hizi lakini ndio hali halisi
Hamna kitu kama hicho, nimetafta hizo picha katika Channel nyingi za Ukraine sijaona hata moja, hivo hizi habari ni kuwa nazo makini, target hapo ni kutusha tu.
 
Ila mkuu Wakorea waliokwenda Russia ni 600 hao 1000 waliokufa mme watoa wap
 

Attachments

  • IMG_20241109_220001.jpg
    96.7 KB · Views: 4
Hamna kitu kama hicho, nimetafta hizo picha katika Channel nyingi za Ukraine sijaona hata moja, hivo hizi habari ni kuwa nazo makini, target hapo ni kutusha tu.
Basi maaskari wa N.korea ni maroboti hawafi vitani
 
Ila mkuu Wakorea waliokwenda Russia ni 600 hao 1000 waliokufa mme watoa wap
Nakuuliza,uliwahesabu?
 
Endelea kula pilipili huko India, na ukishamaliza nenda ukakae chooni masaa sita hiyo ndio Kazi unaweza pekee kwenye propaganda waachie wengine
 
Sio mbaya wanaendelea kupata experience kwenye uwanja wa mapambano. Wakifa more than 10k watakua tayari wameiva kivita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…