Wanajeshi wa Urusi wakamata mji muhimu wa bandari Ukraine

Wanajeshi wa Urusi wakamata mji muhimu wa bandari Ukraine

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Wanajeshi wa Urusi wameukamata mji mmoja muhimu wa bandari wa Ukraine na kuuzingira mwingine kama sehemu ya juhudi za kuitenganisha nchi hiyo na Pwani yake.

Jeshi la Urusi limesema limechukua udhibiti wa Kherson na maafisa wa Ukraine katika eneo hilo wamethibitisha kuwa wanajeshi wamechukua udhibiti wa makao makuu ya serikali ya mitaa katika mji huo wa bandari ya Bahari Nyeusi wenye wakazi 280,000.

Kherson sasa ndiyo mji wa kwanza mkubwa kuanguka tangu kuanza uvamizi wa Urusi wiki moja iliyopita. Kwingineko, Warusi wameendelea na mashambulizi yao katika maeneo kadhaa, ijapokuwa msafara wa vifaru na magari mengine unaripotiwa kukwama kwa siku kadhaa nje ya Mji Mkuu Kyiv.

Mapigano makali yameendelea leo viungani mwa mji mwingine muhimu wa bandari katika Bahari ya Azov, Mariupul na kuutumbukiza gizani. Umeme na mawasiliano ya simu vimekatwa, na makazi na maduka yanakabiliwa na uhaba wa chakula na maji.

Chanzo: DW

_123491722_kherson_reuters.jpg

 
Tuliambiwa bado kilomita 9 kufika Kyiv imekuwa vp hawafiki tu
1.Waisrael walitumia miaka 40 kwa safari ya siku 7

2. Marekani alitumia miaka 20 Afghanitan japo aliondoka kwa aibu

3.Marekani alitumia sku 21 kuingia Baghdad

Unashangaa nini?

Utaua nyuki wote ndipo umumfikie malkia wao

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
 
Safi ,kazi iendelee.rais wa Ukraine kilaza Sana,waliomdanganya wako mbali wanamuangalia ,anavyohangaika kupambania roho yake! Wote wamemsusa . Sio kila mtu anayekukenulia meno yuko pamoja na wewe !!
 
Hizi ndio habari nazopenda kuzisikia Mkuu
Jawa jamaa ndio wanaume waliobaki dunuani wakifuatiwa na mchina wengine moska washirikiane.Wazungu waoga sana, bila ushirika wanatawaliwa hata na mwarabu. Sikutegemea wanaume wa urusi kuinua miguu kuingia vitani na west.
 
Safi ,kazi iendelee.rais wa Ukraine kilaza Sana,waliomdanganya wako mbali wanamuangalia ,anavyohangaika kupambania roho yake! Wote wamemsusa . Sio kila mtu anayekukenulia meno yuko pamoja na wewe !!
Kwa nini asijiuzulu kuokoa watu wake! Huenda Mrusi akapunguza maangamizi. Ni kama Amini dhidi ya Nyerere, mwishowe alikimbia nchi sasa huyu kwa nini hasomu historia ya vita kama hivyo !
 
1.Waisrael walitumia miaka 40 kwa safari ya siku 7

2. Marekani alitumia miaka 20 Afghanitan japo aliondoka kwa aibu

3.Marekani alitumia sku 21 kuingia Baghdad

Unashangaa nini?

Utaua nyuki wote ndipo umumfikie malkia wao

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
Nakupinga hapo namba 2,
 
Back
Top Bottom