Wanajeshi wetu wanajisikiaje??

Wanajeshi wetu wanajisikiaje??

Ghaddaf naye alianza kuiga ushenzi huo anapotembelea nchi za waafrika wenzake anawapa kero na yale mahema yake ya kibedui. Eti naye alijionesha ana ulinzi imara kuliko wa nchi mwenyeji wake. Cha ajabu aliuwawa kama paka mwizi pasipo na huo ulinzi, tena kifo cha kutia huruma kana kwamba hakuwahi kumiliki majeshi na vikosi imara nchini mwake. Hawa wamerekani wana dharau na kiburi kwa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi zetu, hawajakutana na rais wa nchi asiyependa dharau kwa majeshi yake ya ulinzi, hao wanajeshi wao watawekwa kando watulie nchi mwenyeji isimamie shoo nzima ya ulinzi na usalama. Rais wao akiwa anatua na yale madege yao air force wanakuwa na wasiwasi hata na vitu visivyo hai wanavikazia macho kana kwamba ni hatari. Wanapenda kufunuafunua lile zulia jekundu mpaka wanakera. Wakiona kikaratasi kidogo kinapeperushwa na upepo wanakitolea macho na kukikaribia kujua ni kitu gani. Kama tumewakaribisha nyumbani kwetu watuamini mwanzo hadi mwisho hata sisi tunajua ulinzi na usalama kama wao, tuheshimiane
Aliyekuzidi kakuzidi tu,kiongoz wa Marekani ana maadui wengi ndio maana ulinzi wake uko juu,...huwezi shindana na mtu aliyekuzidi...Marekani ni dunia.
 
Salaam ndugu zangu kuna jambo limenifikirisha kidogo baada ya juzi kuja huyo mgeni kutoka Usa sasa baada ya kutua tu kila kitu cha ulinzi kilikuwa chini ya wageni kuanzia Airport mpka sehemu alipokuwa huyo mgeni na mpaka anaondoka wanajeshi wa kigeni ndio walikuwa wanaosimamia show nzima ya ulinzi ya viongozi wote wawili,
Sasa najiuliza hivi wanajeshi wetu wanajisikia kuona nchi yao inalinda na wengine ina maana wao hawaaminiki??
Kwa hiyo dar es salaam ndiyo nchi!?..hao mabwana zako walilinda mipaka ya ngara?!
 
Mtoa mada jaribu kuwa serious kidogo ya mtu apasue jiwe Kwa kichwa Kila 9 Dec ,alafu awe mlinzi wa Rais wa marekani!? Acha ujinga bwana
 
Back
Top Bottom