WanaJF nipeni kazi au kibarua, maisha ya malezi yasije nishinda kuhudumia

WanaJF nipeni kazi au kibarua, maisha ya malezi yasije nishinda kuhudumia

Msumb

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2022
Posts
3,452
Reaction score
5,372
Habari za humu ndugu wana JF natumaini wazima wa afya na tunasonga mbele, kama kichwa cha habari kinavyosomeka,

Wadau nipeni kazi / kibarua nifanye nipate pesa za matumizi za kupata mahitaji ya mtoto mwaka kesho anaanza shule darasa la awali, chekechea, baadhi ya vifaa nimenunua kama kitambaa, t-shirt, begi,

Kilichobaki ni viatu, soksi, ada na mashonesho ya kaptura kwa fundi, kichwa kinapata moto huu mwisho wa mwaka vitu vitapanda bei, wadau nipeni kazi/kibarua nifanye mtu hawezi kukupa hela hivi hivi bure bila kumfanyia kazi!? Nipeni kazi,

Nb: location nipo musoma, sina ujuzi wowote zaidi ya kuelekezwa tu, nipeni kazi/kibarua nijikwamue adha hii😔🙏
 
Watu watakupa kazi sio Kwa Sababu ya shida zako za nyumbani. Bali Kwa sababu unaujuzi na uzoefu na kazi hiyo ili uwazalishie utajiri sio ili unufaike wewe.

Ukishasema unaomba kazi kisa sijui umsaidie mtoto sijui Mama au Baba YAKO, mpaka hapo umekosa hiyo kazi
Sawa motivational speaker
 
Back
Top Bottom