Wanalalamika biashara ya usafirishaji ni hasara ila kila siku wanazidi kuleta magari

Smith Rowe

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2018
Posts
4,319
Reaction score
9,003
Bila salamu,

Haya makampuni ya usafirishaji kila siku barabarani wanaleta chuma mpya, mfano unakuta mtu alianza na fuso moja anatoa ndizi Moshi anashusha Dar baada ya miezi sita analeta chuma nyingine.

Mtu alikuwa anagari mbili route ya Iringa to Dar baada ya mwaka ana gari sita. Bado sisi wapiga debe(sarange) tunasema hii ni biashara kichaa.

Jamaa alikuwa na mende nne zinabeba mizigo Tanzania to Kenya sahivi namkuta ana mende kumi.
(au ni njia za kusafishia fedha big NO).

Jamaa wanamiliki Shuttle zaidi ya 20 route ya Moshi to Rombo sisi madogo tunasema ukifanya usafirishaji utakufa na presha.

Kila siku BM, ABOOD, SHABIBY wanashusha chuma barabarani. USHTUKE hamna biashara yenye faida tuu tuhangaishe kichwa popote hela inapoonekana.

Yale mashamba ya uridhi kule Rombo nauza, ile nyumba kibororoni napeleka hati bank pamoja na ile ya uchira DO OR DIE naweka chuma route ya Moshi Arusha ( nikitoboa Amen nikifilisika baridi tuu).
 
inabidi uwe na roho mbaya ndio ufanikiwe kwenye biashara za mabus na malori
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…