Wanamichezo na wadau wa mpira wa miguu njooni tujadili nini kifanyike ili timu yetu ya Taifa ipige hatua zaidi?

Next time kocha achague wachezaji nje ya Simba na yanga
 
Watanzania bwana mnajifanya mnajua kupata tuu kukosa anhhhhh??
 
Tuache kubeba mabango ya Wanasiasa kwenye michezo. Pia Viongozi wa kisiasa wahudhurie TU kama mashabiki bila ku-influence mambo ya mipira. Yule jamaa kila akiwepo lazima tufungwe!
 
Nakumbuka maneno ya kocha mmoja wa Uganda sio huyu micho baada ya kuifunga timu ya Tanzania kwenye kuwania kuingia kombe la CHAN alihojiwa na mwandishi wa habari. Mwandishi wa habari alimuuliza unahisi ni mbinu Gani ulitumia kushinda mechi na Tanzania walifeli wapi. Yule kocha alimjibu, Tanzania wamewekeza zaidi kwenye hamasa kuliko kwenye mbinu za mpira.
 
Wachezaji waache kutegemea uchawi.. unaficha uwezo wao halisi
 
mashabiki wa mpira wetu wa miguu tujadili mbinu namna gani tunaweza kuipa uhai timu yetu ya taifa (taifa stars).
Hizi ni dakika mbaya sana 90+1 wengine wanaita dakika za lala salama, na tumelala salama shikamoo Uganda, kuna mchawi (siku hizi wachawi sio wazee) mmoja leo asubuhi alikua anasema ataenda kuwanga tufungwe ili tuendelee na ligi za ndani maana nje hatupawezi kweli yametimia 90+1 Rogers Mato anaiandikia bao Uganda

Tanzania 0-1 Uganda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…