Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Wananchi wa Kata ya Kia (Wilaya ya Hai, Kilimanjaro), Majengo (wilayani Arumeru, Arusha), na Naisinyai (wilayani Simanjiro, Manyara) wameandamana na kufunga barabara ya Mirerani hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), wakishinikiza Serikali kutatua changamoto ya eneo korofi linalosababisha mafuriko ya mara kwa mara katika maeneo yao.
Wananchi hao wamesema mafuriko katika mpaka wa Kata za Majengo, Naisinyai, na Kia yamesababisha vifo na uharibifu wa mazao ya chakula, hivyo maandamano yao yamelenga kutoa ujumbe wa amani kwa mamlaka husika.
Maandamano hayo yalifanyika leo, Jumanne Februari 11, 2025, ambapo barabara hiyo ilifungwa kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa 2:44 asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Amir Mkalipa, alifika eneo hilo na kuzungumza na wananchi, akiwaomba kufungua barabara ili kuruhusu abiria waliokwama kuendelea na safari zao.
Aidha, DC Mkalipa aliwahakikishia wananchi kuwa kesho kutafanyika kikao cha pamoja kati ya wakuu wa wilaya hizo tatu, madiwani, pamoja na wenyeviti wa vijiji husika kwa lengo la kujadiliana na Bonde la Pangani kuhusu utatuzi wa tatizo hilo.
Wananchi hao wamesema mafuriko katika mpaka wa Kata za Majengo, Naisinyai, na Kia yamesababisha vifo na uharibifu wa mazao ya chakula, hivyo maandamano yao yamelenga kutoa ujumbe wa amani kwa mamlaka husika.
Maandamano hayo yalifanyika leo, Jumanne Februari 11, 2025, ambapo barabara hiyo ilifungwa kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa 2:44 asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Amir Mkalipa, alifika eneo hilo na kuzungumza na wananchi, akiwaomba kufungua barabara ili kuruhusu abiria waliokwama kuendelea na safari zao.
Aidha, DC Mkalipa aliwahakikishia wananchi kuwa kesho kutafanyika kikao cha pamoja kati ya wakuu wa wilaya hizo tatu, madiwani, pamoja na wenyeviti wa vijiji husika kwa lengo la kujadiliana na Bonde la Pangani kuhusu utatuzi wa tatizo hilo.